< Danieli 6 >

1 Ilimpendeza Dario kuchagua juu ya ufalme magavana wa majimbo 120 ambao wangetawala juu ya ufalme wote.
Svidjelo se Dariju da postavi nad svojim kraljevstvom stotinu i dvadeset satrapa da budu nad svim kraljevstvom.
2 Juu yao kulikuwa na watawala wakuu watatu, na Daniel alikuwa mmoja wao. Hawa watawala waliwekwa ili waweze kuwasimamia magavana wa majimbo, ili kwamba mfalme asipate hasara.
Njima na čelo stavi tri pročelnika - Daniel bijaše jedan od njih - kojima će satrapi polagati račun da se ne bi dosađivalo kralju.
3 Danieli alipambanuliwa juu ya watawala wakuu na juu ya magavana wa majimbo kwasababu alikuwa na roho isiyo ya kawaida. Mfalme alikuwa akipanga kumweka juu ya ufalme wote.
Daniel se toliko isticaše svojim izvanrednim duhom iznad pročelnika i satrapa te kralj mišljaše da ga postavi nad svim kraljevstvom.
4 Basi watawala wakuu wengine na magavana wa majimbo walitafuta makosa katika kazi ambazo Danieli alizifanya kwa ufalme, lakini hawakuweza kuona ufisadi au kushindwa katika majukumu yake kwasababu alikuwa mwaminifu. Hakuna kosa au uzembe uliopatikana ndani yake.
Tada pročelnici i satrapi stadoše tražiti povod, štogod oko državne uprave, zbog čega bi mogli optužiti Daniela; ali ne mogoše na njemu naći ništa takvo, ništa zbog čega bi ga prekorili, jer bijaše vjeran, na njemu ni nemara ni ogrešenja.
5 Kisha watu hawa wakasema, “Hatukuweza kupata sababu yoyote ya kumshitaki huyu Danieli isipokuwa tukitafuta kitu fulani dhidi yake kuhusiana na sheria za Mungu wake.'”
Ti ljudi rekoše tada: “Nećemo naći nikakva povoda protiv Daniela, osim da nađemo nešto protiv njega u zakonu njegova Boga.”
6 Ndipo watawala hawa na magavana walileta mpango mbele ya mfalme. Walimwambia, “Mfalme Dario, uishi milele!
Tada pročelnici i satrapi navališe na kralja te mu rekoše: “O kralju Darije, živ bio dovijeka!
7 Watawala wote wakuu wa ufalme, magavana wa mikoa, na magavana wa majimbo, washauri, na magavana wameshauriana kwa pamoja na kuamua kuwa wewe, mfalme, unapaswa kupitisha amri na kuitekeleza, ili kwamba mtu yeyote anayefanya dua kwa mungu yeyote au mtu kwa siku thelathini, isipokuwa wewe mfalme, mtu huyo lazima atupwe katika tundu la simba.
Svi pročelnici kraljevstva, predstojnici i satrapi, savjetnici i namjesnici složiše se u tome da bi trebalo da kralj izda naredbu i zabranu: svaki onaj koji bi u roku od trideset dana upravio molbu bilo na kojega boga ili čovjeka, osim na tebe, o kralju, bit će bačen u lavsku jamu.
8 Sasa mfalme, litoe agizo na utie saini nyaraka ili kwamba isije ikabadilika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi, hivyo haiweze ikabatilishwa.
O kralju, potvrdi tu zabranu i potpiši naredbu da bude neopoziva prema nepromjenljivom medijsko-perzijskom zakonu!”
9 Basi, mfalme Dario alitia saini nyaraka kwa kuifanya amri kuwa sheria.
Nato kralj Darije potpisa pismo i zabranu.
10 Danieli alipojua kuwa nyaraka imekwisha kusainiwa kuwa sheria, alienda ndani ya nyumba yake (madirisha yake katika chumba cha juu yalikuwa wazi kuelekea Yerusalemu), na alipiga magoti yake, kama alivyokuwa akifanya mara tatu kwa siku, na aliomba na kushukuru mbele ya Mungu wake, kama alivyofanya hapo kabla.
Saznavši Daniel da je spis potpisan, otiđe u svoju kuću. Prozori gornje sobe bijahu otvoreni prema Jeruzalemu. Tu je on tri puta na dan padao na koljena blagoslivljajući, moleći i hvaleći Boga, kako je uvijek činio.
11 Kisha watu hawa walikuwa wameunda hila kwa pamoja walimwona Danieli akiomba na kutafuta msaada kutoka kwa Mungu.
Oni ljudi nahrupiše i nađoše Daniela gdje moli i zaziva svoga Boga.
12 Ndipo walipomwendea mfalme na kuongea naye kuhusiana na amri yake: “Je haukuweka amri kwamba mtu yeyote akayefanya maombi kwa mungu mwingine au kwa binadamu ndani ya siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, mfalme, lazima mtu huyo atupwe katika tundu la simba? Mfalme akajibu, “Jambo hili ni la hakika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi; ambazo haziwezi zikabatilishwa.”
Tada odoše i pred kraljem se pozvaše na kraljevsku zabranu: “Zar ti nisi potpisao zabranu prema kojoj će svaki onaj koji bi u vremenu od trideset dana upravio molbu na nekoga boga ili čovjeka, osim na tebe, o kralju, biti bačen u lavsku jamu?” Kralj odgovori: “Tako je odlučeno po nepromjenljivom medijsko-perzijskom zakonu.”
13 Kisha wakamjibu mfalme, “Mtu yule Daniel, ambaye ni mmoja wa watu wa mateka kutoka Yuda, hakutii wewe, mfalme wala maagizo yako uliyoyasaini. Yeye humwomba Mungu wake mara tatu kwa siku.”
Tada rekoše kralju: “Daniel, onaj od izgnanika judejskih, ne mari za tebe, o kralju, ni za tvoju zabranu koju si potpisao: tri puta na dan obavlja svoju molitvu.”
14 Mfalme aliposikia haya, alisikitishwa sana, alitumia akili jinsi ya kumwokoa kutoka katika utawala huu. Alisumbuka sana mpaka wakati wa kuzama kwa jua akijaribu kumwokoa Danieli.
Čuvši te riječi, kralj se vrlo ražalosti i odluči spasiti Daniela. Sve do sunčeva zalaza nastojaše da ga spasi.
15 Kisha watu hawa waliokuwa wamepanga njama walikusanyika kwa pamoja na mfalme, na wakamwambia, “Ujue mfalme kwamba ni sheria ya Wamedi na Waajemi kwamba hakuna amri au sanamu ambayo mfalme anaipitisha yaweza kubadilishwa.”
Ali oni ljudi navališe na kralja govoreći: “Znaj, o kralju, da prema medijsko-perzijskom zakonu nijedna kraljevska zabrana ili odluka ne može biti opozvana!”
16 Ndipo mfalme alitoa agizo, na walimleta ndani Danieli, na kisha wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako, ambaye unamtumikia daima, na akuokoe.''
Tada kralj naredi da dovedu Daniela i da ga bace u lavsku jamu. Kralj reče Danielu: “Bog tvoj, kome tako postojano služiš, neka te izbavi.”
17 Jiwe lililetwa katika mlango wa tundu, na mfalme alilitia muhuri wa pete yake mwenyewe na pamoja na muhuri wa wakuu wake ili kwamba chochote kisiweze kubadilishwa kuhusiana na Danieli.
Donesoše kamen i staviše ga jami na otvor. Kralj ga zapečati prstenom svojim i prstenom svojih velikaša, da se ništa ne mijenja za Daniela.
18 Basi mfalme alienda kwenye ikulu yake na usiku ule alikuwa na mfungo. Hakuna starehe yoyote iliyoletwa mbele yake, nao usingizi ulimkimbia.
Kralj se vrati u svoj dvor i provede noć ne okusivši jela i ne dopustivši da mu dovedu suložnice. Nije mogao usnuti.
19 Kisha katika mapambazuko mfalme aliamka na kwa haraka alienda kwenye tundu la simba.
Kralj ustade u ranu zoru, kad se danilo, i pođe brzo k lavskoj jami.
20 Na alipokaribia kwenye tundu, alimwita Danieli kwa sauti ya huzuni, akimwambia Danieli, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je Mungu wako ambaye anamtumkia daima ameweza kukuokoa kutoka katika simba?
Kad se primače blizu, viknu žalosnim glasom Danielu: “Daniele, slugo Boga živoga, je li te Bog, kome postojano služiš, mogao izbaviti od lavova?”
21 Ndipo Danieli akamwambia mfalme, “Mfalme, uishi milele!
Daniel odgovori: “O kralju, živ bio dovijeka!
22 Mungu wangu amemtuma mjumbe na amevifunga vinywa vya simba, na hazijaweza kunidhuru. Kwa kuwa sikuwa na hatia yoyote mbele yake na pia mbele yako, ewe mfalme, na sijakufanyia jambo lolote la kukudhuru.”
Moj je Bog poslao svog Anđela; zatvorio je ralje lavovima te mi ne naudiše, jer sam nedužan pred njim. Pa i pred tobom, o kralju, ja sam bez krivice.”
23 Basi mfalme alikuwa na furaha sana. Alitoa agizo kwamba wanatakiwa wamtoe Danieli nje ya tundu. Hivyo Danieli aliondolewa kutoka katika tundu. Hakuna dhara lolote lililoonekana kwake, kwa kuwa alikuwa amemtumainia Mungu wake.
Kralj se vrlo obradova i naredi da Daniela izvade iz jame. Izvadiše Daniela iz jame neozlijeđena, jer se bijaše uzdao u svoga Boga.
24 Mfalme alitoa agizo, waletwe wale watu waliomshitaki Danieli na kisha akawatupa wao katika tundu la simba - wao, na watoto wao, na wake zao. Kabla hawajafika sakafuni, simba waliwararua na kuvunjavunja mifupa yao vipande vipande.
Kralj zapovjedi da dovedu one ljude koji bijahu optužili Daniela i da ih bace u lavsku jamu - njih, njihove žene i njihovu djecu: i prije nego dodirnuše tlo, lavovi ih zgrabiše i smrviše im kosti.
25 Kisha mfalme Dario aliandika ujumbe kwa watu wote, mataifa na lugha ambazo ziliishi katika dunia yote: “Amani na iongezeke kwenu.
Nato kralj Darije napisa svim plemenima, narodima i jezicima što stanuju po svoj zemlji: “Obilovali mirom!
26 Ninaagiza kwamba katika utawala wote wa ufalme wangu watu watetemeka na kumcha mbele ya Mungu wa Danieli, kwa kuwa ni Mungu aliye hai na huishi milele, na ufalme wake hauwezi kuharibiwa; utawala wake utakuwepo hadi mwisho.
Evo naredbe koju donosim: u svemu mojem kraljevstvu neka se ljudi boje i neka dršću pred Bogom Danielovim: On je Bog živi, on ostaje dovijeka! Njegovo kraljevstvo neće propasti, njegovoj vlasti nema kraja!
27 Yeye anatuhifadhi salama na kutuokoa, na anafanya ishara na maajabu mbinguni na duniani; amemhifadhi Danieli salama dhidi ya uwezo wa simba.”
On izbavlja i spasava, čini znake i čudesa na nebesima i na zemlji! On je spasio Daniela iz šapa lavljih!”
28 Na hivyo basi, Danieli alifanikiwa katika utawala wa Dario na katika utawala wa Koreshi Mwajemi.
Daniel bijaše sretan za vladanja Darija i za vladanja Kira Perzijanca.

< Danieli 6 >