< Danieli 5 >

1 Mfalme Belshaza alifanya sherehe kubwa kwa kwa ajili ya wakuu wake wa kuheshimiwa wapatao elfu moja, na alikunywa divai mbele yao wote watu elfu moja.
Цар Валтасар учини велику гозбу хиљади кнезова својих, и пијаше вино пред хиљадом њих.
2 Wakati Belshaza alipokuwa akionja divai, alitoa agizo la kuleta vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu au kwa fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka katika hekalu huko Yerusalemu, ambavyo yeye, na wakuu wake, na wake zake, na masuria waliweza kuvinywea.
Напив се вина Валтасар заповеди да се донесу судови златни и сребрни, које беше однео Навуходоносор отац му из цркве јерусалимске, да из њих пију цар и кнезови му и жене његове и иноче његове.
3 Watumishi walivileta vyombo ya dhahabu vilivyokuwa vimechukulia katika hekalu, nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Mfalme na wakuu wake, na wake zake na masuria walivinywea.
И донесоше златне судове које беху однели из цркве дома Господњег у Јерусалиму, и пијаху из њих цар и кнезови његови, жене његове и иноче његове.
4 Walikunywa divai na kuzisifu sanamu zao zilizotengenezwa kwa dhahabu na fedha, shaba, chuma, mbao na mawe.
Пијаху вино, и хваљаху богове златне и сребрне и бронзане и дрвене и камене.
5 Kwa wakati huo huo vidole vya mkono wa mtu vilionekana mbele ya kinara cha taa na kuandika katika ukuta uliopigwa lipu katika ikulu ya mfalme. Mfalme aliweza kuona sehemu ya mkono ulipokuwa unaandika.
У тај час изиђоше прсти руке човечије и писаху према свећњаку по окреченом зиду од царског двора, и цар виде руку која писаше.
6 Ndipo uso wa mfalme ulibadilika na mawazo yake yalimwogopesha; miguu yake haikuweza kumfanya asimame, na magoti yake yalikuwa yakigongana kwa pamoja.
Тада се промени лице цару, и мисли га његове узнемирише и појас се око њега распаса и колена му удараху једно о друго.
7 Mfalme alitoa agizo kwa kupiga kelele, waletwe ndani wale ambao hudai wanaweza kuzungumza na wafu, watu wenye hekima, na wataalamu wa nyota. Mfalme akawaambia wale waliojulikana kwa hekima katika Babeli, “Yeyote atakayeyaeleza maandishi haya na maana yake atavikwa nguo za zambarau na atavikwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake. Naye atakuwa mtawala wa tatu wa juu kwa mamlaka katika ufalme.”
Повика цар гласно, те доведоше звездаре, Халдеје и гатаре; и проговори цар и рече мудрацима вавилонским: Ко прочита ово писмо и каже ми шта значи, онај ће се обући у скерлет, и носиће златну верижицу о врату, и биће трећи господар у царству.
8 Ndipo watu wote wa mfalme walikuwa wakijulikana kwa hekima yao waliingia ndani, lakini hawakuweza kuyasoma maandishi wala kueleza maana yake kwa mfalme.
Тада приступише сви мудраци цареви; али не могоше прочитати писма нити казати цару шта значи.
9 Kisha mfalme Belshaza alishitushwa sana na mwonekano wa uso wake ulibadilika. Wakuu wake nao walishangazwa sana.
Тада се цар Валтасар врло узнемири, и лице му се сасвим измени; и кнезови се његови препадоше.
10 Ndipo sasa malkia alikuja katika nyumba ya sherehe kwasababu ya kile ambacho mfalme na wakuu wake walikuwa wamekisema. Malkia akasema, “Mfalme na aishi milele! Usiache mawazo yako yakakusumbua. Usiruhusu mwonekano wa uso wako ubadilike.
Дође царица ради тога што се догоди цару и кнезовима његовим у кућу где беше гозба, и проговори царица и рече: Царе, да си жив довека! Да те не узнемирују мисли твоје, и да ти се лице не мења.
11 Kuna mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu watakatifu dani yake. Katika siku za baba yako, mwanga na weledi na hekima ya miungu ilipatikana ndani yake. Mfalme Nebukadneza, baba yako mfalme, alimfanya kuwa mkuu wa waganga, pamoja na mkuu wa wale wanazungumza na wafu, na wa wenye hekima, na wa wataalamu wa nyota.
Има човек у твом царству, у коме је дух светих богова; и у време оца твог нађе се у њега видело и разум и мудрост, каква је у богова, и цар Навуходоносор, отац твој, царе, постави га главарем врачарима, звездарима, Халдејима и гатарима;
12 Roho bora, ufahamu, weledi, kutafsiri ndoto, kufafanua mafumbo na kutatua matatizo - hizi ni sifa zilizopatikana kwa mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Sasa mwiteni Danieli naye atawaambia maana ya kile kilichoandikwa.”
Јер велик дух и знање и разум за казивање снова и погађање загонетки и размршивање замршених ствари нађе се у Данила, коме цар наде име Валтасар; нека сада дозову Данила, и он ће казати шта значи.
13 Ndipo Danieli alipoletwa mbele ya mfalme. Mfalme akamwambia, “Wewe ni yule Danieli, mmoja kati ya watu wa mateka wa Yuda, ambao baba yangu mfalme aliwaleta kutoka Yuda.
Тада Данило би доведен пред цара. Цар проговори Данилу и рече: Јеси ли ти Данило између робља Јудина, које доведе из јудејске цар отац мој?
14 Nimesikia habari kukuhusu wewe, kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na ya kwamba mwanga na ufahamu na hekima bora inapatikana ndani yako.
Чух за тебе да је дух светих богова у теби, и видело и разум и мудрост велика да се нађе у тебе.
15 Na sasa watu wanaojulikana kwa hekima na wale wanaozungumza na wafu, wamekwisha kuletwa mbele yangu, ili kusoma maandishi haya na kunijulisha maana ya tafsiri yake, lakini hawakuweza kunijulisha tafsiri yake.
А сада су доведени преда ме мудраци, звездари, да прочитају писмо и кажу ми шта значи; али не могу да кажу шта то значи.
16 Nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo. Sasa kama utaweza kusoma maandishi na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na kuwa na kuvalishwa mkufu wa dhahabu shingoni mwako, na utakuwa mtawala wa tatu mwenye mamlaka katika ufalme.”
А за тебе ја чух да можеш протумачити и замршене ствари размрсити. Ако, дакле, можеш прочитати ово писмо и казати ми шта значи, обући ћеш се у скерлет, и златну верижицу носићеш о врату, и бићеш трећи господар у царству.
17 Kisha Danieli akajibu mbele ya mfalme, “Zawadi yako na iwe kwa ajili yako mwenyewe, na thawabu yako na umpe mtu mwingine. Hata hivyo, mfalme, nitakusomea maandishi na nitakwaambia maana.
Тада одговори Данило и рече пред царем: Дарови твоји нека теби, и подај другом поклоне своје; а писмо ћу ја прочитати цару и казати шта значи.
18 Na juu yako, Ewe mfalme, Mungu Aliye juu sana alimpa Nebukadneza baba yako ufalme, ukuu, heshima na enzi.
Царе, Бог Вишњи даде царство величину и славу и част Навуходоносору, оцу твом.
19 Na kwasababu ya ukuu huo, Mungu alimpa watu wote, mataifa, na lugha walimtetemekea na kumwogopa. Aliwauwa wale aliotaka wafe na aliwaacha hai wale aliotaka waishi. Aliwainua wale aliowataka, na aliwashusha wale aliowataka.
И од величине коју му даде сви народи, племена и језици дрхтаху пред њим и бојаху га се; убијаше кога хоћаше, и остављаше у животу кога хоћаше, узвишаваше кога хоћаше, и понижаваше кога хоћаше.
20 Lakini wakati moyo ulipokuwa na kiburi na roho yake ilifanywa kuwa mgumu na kwasababu hiyo alitenda kwa kiburi, alishushwa kutoka kiti chake cha enzi cha kifalme, na waliiondoa enzi yake.
Али када му се подиже срце и дух му се посили у охолости, би сметнут с царског престола свог, и узеше му славу.
21 Aliondolewa katika ubinadamu, alikuwa na akili za mnyama, na aliishi na punda wa mwituni. Alikula majani kama ng'ombe. Mwili wake ulilowanishwa kwa umande wa kutoka mbinguni mpaka pale alipojifunza kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme za watu na ya kwamba humweka mtu yeyote amtakaye juu yake.
И би прогнан између људи и срце му поста као у звери, и стан му беше с дивљим магарцима, хранише га травом као говеда, и роса небеска кваси му тело, докле позна да Бог Вишњи влада царством људским, и кога хоће поставља над њим.
22 Wewe mwana wake, Belshaza, haujaunyenyekeza moyo wako, ingawa aliyajua haya yote.
А ти, Валтасаре, сине његов, ниси понизио срца свог премда си знао све ово.
23 Umejiinua mwenyewe kinyume cha Bwana wa mbinguni. Katika nyumba yake walikuletea vyombo ambavyo wewe, wakuu wako, wake zako na masuria wako walivinywea, na kisha ukaisifia sana sanamu zilitengenezwa kwa fedha na dhahabu, shaba, chuma, mbao, na mawe - sanamu ambazo haziwezi kuona, kusikia wa kujua kitu chochote. Haujamheshimu Mungu ambaye anaishikilia pumzi yako katika mkono wake na ambaye anazijua njia zako zote.
Него си се подигао на Господа небеског, и судове дома Његовог донесоше преда те, и писте из њих вино ти и кнезови твоји, жене твоје и иноче твоје, и ти хвали богове сребрне и златне, бронзане, гвоздене, дрвене и камене, који не виде нити чују, нити разумеју, а не слави Бога, у чијој је руци душа твоја и сви путеви твоји.
24 Ndipo Mungu aliutuma mkono kutoka katika makao yake na maandishi haya yaliandikwa.
Зато од Њега би послана рука и ово писмо би написано.
25 Haya ndiyo maandishi ambayo yaliandikwa: 'Mene, Mene, Tekeli na Peresin.'
А ово је писмо написано: МЕНЕ, МЕНЕ, ТЕКЕЛ, УФАРСИН.
26 Maana yake ni: 'Mene,' 'Mungu ameuhesabu ufalme wako na ameukomesha.'
А ово значе те речи: МЕНЕ, бројао је Бог твоје царство и до краја избројао.
27 'Tekeli' 'umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.'
ТЕКЕЛ, измерен си на мерила, и нашао си се лак.
28 'Peresi' 'ufalme wako umegawanyika na wamepewa Wamedi na Waajemi.'”
ФЕРЕС, раздељено је царство твоје, и дано Мидијанима и Персијанима.
29 Ndipo Belshaza alitoa agizo, na walimvalisha Danieli mavazi ya zambarau. Mkufu wa dhahabu walimvisha shingoni, na mfalme alitoa tamko juu ya Danieli kuwa atakuwa mtawala mwenye mamlaka ya nafasi ya tatu katika ufalme.
Тада заповеди Валтасар, те обукоше Данила у скерлет, и метнуше му златну верижицу око врата, и прогласише за њ да је трећи господар у царству.
30 Usiku ule Belshaza, mfalme wa Babeli aliuawa,
Исту ноћ би убијен Валтасар, цар халдејски.
31 na Dario Mwajemi aliuchukua ufalme alipokuwa na miaka ipatayo sitini na miwili.
А Дарије Мидијанин преузе царство, и беше му око шездесет и две године.

< Danieli 5 >