< Danieli 5 >
1 Mfalme Belshaza alifanya sherehe kubwa kwa kwa ajili ya wakuu wake wa kuheshimiwa wapatao elfu moja, na alikunywa divai mbele yao wote watu elfu moja.
Le roi Balthasar donna un grand festin à ses grands, au nombre de mille; et, en présence de ces mille, il buvait du vin.
2 Wakati Belshaza alipokuwa akionja divai, alitoa agizo la kuleta vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu au kwa fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka katika hekalu huko Yerusalemu, ambavyo yeye, na wakuu wake, na wake zake, na masuria waliweza kuvinywea.
Sous l’influence de la boisson, Balthasar ordonna d’apporter les vases d’or et d’argent, que son père Nabuchodonosor avait enlevés du temple de Jérusalem, afin que le roi, ses grands, ses épouses et ses concubines s’en servissent pour boire.
3 Watumishi walivileta vyombo ya dhahabu vilivyokuwa vimechukulia katika hekalu, nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Mfalme na wakuu wake, na wake zake na masuria walivinywea.
Aussitôt on apporta les vases d’or qui avaient été enlevés de l’enceinte du temple de Dieu à Jérusalem. Le roi, ses grands, ses épouses et ses concubines s’en servirent pour boire.
4 Walikunywa divai na kuzisifu sanamu zao zilizotengenezwa kwa dhahabu na fedha, shaba, chuma, mbao na mawe.
Ils burent du vin et glorifièrent les Dieux d’or et d’argent, d’airain, de fer, de bois et de pierre.
5 Kwa wakati huo huo vidole vya mkono wa mtu vilionekana mbele ya kinara cha taa na kuandika katika ukuta uliopigwa lipu katika ikulu ya mfalme. Mfalme aliweza kuona sehemu ya mkono ulipokuwa unaandika.
Au même moment, des doigts d’une main d’homme apparurent et écrivirent, face au candélabre, sur la chaux de la paroi du palais royal, et le roi vit cette main détachée qui écrivait.
6 Ndipo uso wa mfalme ulibadilika na mawazo yake yalimwogopesha; miguu yake haikuweza kumfanya asimame, na magoti yake yalikuwa yakigongana kwa pamoja.
Alors le roi changea de couleur, son esprit fut frappé de crainte; les attaches de ses reins se détendirent et ses genoux s’entrechoquèrent.
7 Mfalme alitoa agizo kwa kupiga kelele, waletwe ndani wale ambao hudai wanaweza kuzungumza na wafu, watu wenye hekima, na wataalamu wa nyota. Mfalme akawaambia wale waliojulikana kwa hekima katika Babeli, “Yeyote atakayeyaeleza maandishi haya na maana yake atavikwa nguo za zambarau na atavikwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake. Naye atakuwa mtawala wa tatu wa juu kwa mamlaka katika ufalme.”
Le roi cria avec force qu’on amenât les sorciers, les astrologues et les augures; puis il prit la parole et dit aux sages de Babylone: "Tout homme qui lira cette inscription et m’en fera connaître le sens sera vêtu de pourpre, portera un collier d’or au cou et gouvernera en tiers le royaume."
8 Ndipo watu wote wa mfalme walikuwa wakijulikana kwa hekima yao waliingia ndani, lakini hawakuweza kuyasoma maandishi wala kueleza maana yake kwa mfalme.
Tous les sages du roi étaient entrés; mais ils ne purent lire l’inscription ni en faire connaître le sens au roi.
9 Kisha mfalme Belshaza alishitushwa sana na mwonekano wa uso wake ulibadilika. Wakuu wake nao walishangazwa sana.
Le roi Balthasar fut alors extrêmement effrayé, sa figure se décomposa, et ses grands furent bouleversés.
10 Ndipo sasa malkia alikuja katika nyumba ya sherehe kwasababu ya kile ambacho mfalme na wakuu wake walikuwa wamekisema. Malkia akasema, “Mfalme na aishi milele! Usiache mawazo yako yakakusumbua. Usiruhusu mwonekano wa uso wako ubadilike.
La reine, en raison des propos du roi et de ses grands, se rendit dans la salle du festin, elle prit la parole et dit: "Vive le roi à jamais! Que tes pensées cessent de t’épouvanter et que ton visage ne change pas de couleur!
11 Kuna mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu watakatifu dani yake. Katika siku za baba yako, mwanga na weledi na hekima ya miungu ilipatikana ndani yake. Mfalme Nebukadneza, baba yako mfalme, alimfanya kuwa mkuu wa waganga, pamoja na mkuu wa wale wanazungumza na wafu, na wa wenye hekima, na wa wataalamu wa nyota.
Il est un homme dans ton royaume, qui est pénétré de l’esprit des Dieux saints, et chez qui, du temps de ton père, se sont rencontrées une perspicacité, une intelligence et une sagesse dignes des Dieux; aussi le roi Nabuchodonosor, ton père, l’a-t-il établi chef des magiciens, des devins, des astrologues et des augures, oui ton propre père, le roi!
12 Roho bora, ufahamu, weledi, kutafsiri ndoto, kufafanua mafumbo na kutatua matatizo - hizi ni sifa zilizopatikana kwa mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Sasa mwiteni Danieli naye atawaambia maana ya kile kilichoandikwa.”
Parce qu’un esprit supérieur, la science, l’intelligence, l’art d’interpréter les songes, d’éclaircir les énigmes, de résoudre les difficultés se sont rencontrés chez ce Daniel, que le roi avait surnommé Beltchaçar. Que Daniel soit donc mandé, et il dévoilera ce que cela signifie."
13 Ndipo Danieli alipoletwa mbele ya mfalme. Mfalme akamwambia, “Wewe ni yule Danieli, mmoja kati ya watu wa mateka wa Yuda, ambao baba yangu mfalme aliwaleta kutoka Yuda.
Aussitôt Daniel fut introduit devant le roi; celui-ci prit la parole et lui dit: "C’Est donc toi ce Daniel, qui fait partie du groupe des exilés de Juda que le roi mon père a emmenés de Judée!
14 Nimesikia habari kukuhusu wewe, kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na ya kwamba mwanga na ufahamu na hekima bora inapatikana ndani yako.
J’Ai ouï dire que tu es rempli de l’esprit des Dieux, et qu’il se rencontre chez toi de la perspicacité, de l’intelligence et une sagesse supérieure.
15 Na sasa watu wanaojulikana kwa hekima na wale wanaozungumza na wafu, wamekwisha kuletwa mbele yangu, ili kusoma maandishi haya na kunijulisha maana ya tafsiri yake, lakini hawakuweza kunijulisha tafsiri yake.
Or, on a amené en ma présence les sages, les devins pour lire cette inscription et m’en faire connaître le sens; mais ils sont incapables de me révéler la signification de la chose.
16 Nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo. Sasa kama utaweza kusoma maandishi na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na kuwa na kuvalishwa mkufu wa dhahabu shingoni mwako, na utakuwa mtawala wa tatu mwenye mamlaka katika ufalme.”
Mais de toi j’ai ouï dire que tu sais donner des interprétations et résoudre les difficultés. Donc, si tu peux lire cette inscription et m’en faire connaître le sens, tu seras revêtu de pourpre, un collier d’or ornera ton cou, et tu gouverneras en tiers le royaume."
17 Kisha Danieli akajibu mbele ya mfalme, “Zawadi yako na iwe kwa ajili yako mwenyewe, na thawabu yako na umpe mtu mwingine. Hata hivyo, mfalme, nitakusomea maandishi na nitakwaambia maana.
Alors Daniel répliqua en disant au roi: "Garde tes dons pour toi, et gratifie d’autres de tes présents; toutefois je lirai l’inscription au roi et je lui en ferai connaître le sens.
18 Na juu yako, Ewe mfalme, Mungu Aliye juu sana alimpa Nebukadneza baba yako ufalme, ukuu, heshima na enzi.
O roi, le Dieu suprême avait donné à ton père Nabuchodonosor royauté, grandeur, majesté et magnificence.
19 Na kwasababu ya ukuu huo, Mungu alimpa watu wote, mataifa, na lugha walimtetemekea na kumwogopa. Aliwauwa wale aliotaka wafe na aliwaacha hai wale aliotaka waishi. Aliwainua wale aliowataka, na aliwashusha wale aliowataka.
Et à cause de la grandeur qui lui avait été octroyée, nations, peuples et langues tremblaient tous de peur devant lui: il tuait qui il voulait, laissait vivre qui il voulait, élevait ou abaissait qui il voulait.
20 Lakini wakati moyo ulipokuwa na kiburi na roho yake ilifanywa kuwa mgumu na kwasababu hiyo alitenda kwa kiburi, alishushwa kutoka kiti chake cha enzi cha kifalme, na waliiondoa enzi yake.
Mais lorsque son cœur s’enorgueillit et que son esprit s’enhardit jusqu’à l’arrogance, il fut précipité de son trône royal et se vit dépouillé de sa majesté.
21 Aliondolewa katika ubinadamu, alikuwa na akili za mnyama, na aliishi na punda wa mwituni. Alikula majani kama ng'ombe. Mwili wake ulilowanishwa kwa umande wa kutoka mbinguni mpaka pale alipojifunza kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme za watu na ya kwamba humweka mtu yeyote amtakaye juu yake.
Il fut chassé de la société des hommes, et son cœur devint semblable à celui des bêtes; sa demeure fut avec les ânes sauvages, on lui donna comme aux bœufs de l’herbe pour nourriture, et son corps fut humecté par la rosée du ciel, jusqu’à ce qu’il reconnût que le Dieu suprême est maître de la royauté des hommes et qu’il y appelle qui lui plaît.
22 Wewe mwana wake, Belshaza, haujaunyenyekeza moyo wako, ingawa aliyajua haya yote.
Et toi, son fils Balthasar, tu n’as pas humilié ton cœur, bien que tu fusses instruit de tout cela.
23 Umejiinua mwenyewe kinyume cha Bwana wa mbinguni. Katika nyumba yake walikuletea vyombo ambavyo wewe, wakuu wako, wake zako na masuria wako walivinywea, na kisha ukaisifia sana sanamu zilitengenezwa kwa fedha na dhahabu, shaba, chuma, mbao, na mawe - sanamu ambazo haziwezi kuona, kusikia wa kujua kitu chochote. Haujamheshimu Mungu ambaye anaishikilia pumzi yako katika mkono wake na ambaye anazijua njia zako zote.
Tu t’es insurgé contre le maître du ciel, en faisant apporter devant toi les vases de son temple pour y boire du vin, toi, tes grands, tes épouses et tes concubines; tu as célébré les Dieux d’argent et d’or, d’airain, de fer, de bois et de pierre, qui ne voient, ni n’entendent, ni ne savent rien. Quant au Dieu qui tient ton âme en ses mains et qui dirige toutes tes voies, tu ne l’as pas honoré.
24 Ndipo Mungu aliutuma mkono kutoka katika makao yake na maandishi haya yaliandikwa.
C’Est pourquoi une main détachée a été envoyée par lui, et cette inscription a été tracée.
25 Haya ndiyo maandishi ambayo yaliandikwa: 'Mene, Mene, Tekeli na Peresin.'
Or, voici l’inscription qui a été tracée: MENÊ, MENÊ, TEKÊL, OUFARSIN.
26 Maana yake ni: 'Mene,' 'Mungu ameuhesabu ufalme wako na ameukomesha.'
Et telle est l’explication de ces mots: MENÊ Dieu a compté les jours de ta royauté et en a décidé la fin;
27 'Tekeli' 'umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.'
TEKÊL tu as été pesé dans la balance et trouvé trop léger;
28 'Peresi' 'ufalme wako umegawanyika na wamepewa Wamedi na Waajemi.'”
PERES ton royaume a été divisé et donné aux Mèdes et aux Perses."
29 Ndipo Belshaza alitoa agizo, na walimvalisha Danieli mavazi ya zambarau. Mkufu wa dhahabu walimvisha shingoni, na mfalme alitoa tamko juu ya Danieli kuwa atakuwa mtawala mwenye mamlaka ya nafasi ya tatu katika ufalme.
Aussitôt Balthasar donna l’ordre de revêtir Daniel de pourpre, de lui mettre un collier d’or au cou et de proclamer qu’il gouvernerait en tiers le royaume.
30 Usiku ule Belshaza, mfalme wa Babeli aliuawa,
Cette même nuit Balthasar, le roi Chaldéen, fut mis à mort.
31 na Dario Mwajemi aliuchukua ufalme alipokuwa na miaka ipatayo sitini na miwili.
Et Darius le Mède reçut la royauté à l’âge de soixante-deux ans.