< Danieli 4 >

1 Mfalme Nebukadneza aliituma amri hii kwa watu wote, mataifa, na lugha walioishi katika nchi: “Na amani yenu na iongezeke.
Nebuchadnezzar king the to all peoples the nations the and languages the which ([are] dwelling *Q(k)*) in all earth the peace your may it increase.
2 Imeonekana vizuri kwangu kuwaambia juu ya ishara na maajabu ambayo Mungu Mkuu Aliye juu amenifanyia.
Signs the and wonders the which he has done with me God (Most High the *Q(k)*) it seemed good before me to declare.
3 Ni kwa namna gani Ishara zake ni kubwa, na ni kwa namna gani maajabu yake yana nguvu! Ufalme wake ni ufalme unaodumu milele, na utawala wake hudumu kizazi hadi kizazi.”
[are] signs His how much! great and [are] wonders his how much! strong kingdom his [is] a kingdom of perpetuity and dominion his [is] with generation and generation.
4 Mimi, Nebukadneza, nilikuwa ninaishi kwa furaha katika nyumba yangu, na nilikuwa nikifurahia mafanikio katika ikulu yangu.
I Nebuchadnezzar at ease I was in house my and flourishing in palace my.
5 Lakini ndoto niliyoiota ilifanya niogope. Nilipokuwa nimejilaza pale, taswira niliyoiona na maono katika akili yangu yalinitaabisha.
A dream I saw and it made afraid me and imaginings on bed my and [the] visions of head my they alarmed me.
6 Basi nilitoa agizo la kuwaleta mbele yangu watu wote wa Babeli waliokuwa na hekima ili kwamba waweze kunitafsiria ndoto.
And from me it was made a decree to bring in before me all [the] wise men of Babylon that [the] interpretation of dream the they will make known to me.
7 Kisha walikuja wachawi, wale ambao hudai kuzungumza na wafu, watu wenye hekima, na wasoma nyota. Niliwaambia juu ya ndoto, lakini hawakuweza kunitafsiria.
Then ([were] going in *Q(k)*) magicians the conjurers the (Chaldeans the *Q(K)*) and astrologers the and dream the [was] saying I before them and interpretation its not [they were] making known to me.
8 Bali mwishoni Danieli aliingia ndani - yeye ambaye huitwa Belteshaza jina la mungu wangu, na ambaye ndani yake kuna roho ya miungu mitakatifu - na nilimwambia juu ya ndoto.
And until at last he came in before me Daniel who name his [is] Belteshazzar like [the] name of god my and who a spirit of gods holy [is] in him and dream the before him I said.
9 “Belteshaza, mkuu wa wachawi, ninajua kuwa roho ya miungu watakatifu iko ndani yako na ya kwamba hakuna siri iliyo ngumu kwako. Niambie kile nilichokiona katika ndoto yangu na nini maana yake.
O Belteshazzar [the] chief of magicians the whom - I I know that a spirit of gods holy [is] in you and any secret not [is] oppressing you [the] visions of dream my which I saw and interpretation its tell!
10 Haya ndiyo niliyoyaona katika akili zangu nilipokuwa nimejilaza katika kitanda changu: Nilitazama, na kulikuwa na mti katikati ya dunia, na urefu wake ulikuwa ni mkubwa sana.
And [the] visions of head my on bed my seeing I was and lo! a tree in [the] midst of land the and height its [was] great.
11 Mti ulikua na ukawa wenye nguvu. Na sehemu ya juu yake ilifika mbinguni, uliweza kuonekana kutoka miisho ya dunia yote.
It grew great tree the and it grew strong and height its it reached to heavens the and [the] sight of it [was] to [the] end of all land the.
12 Majani yake yalikuwa mazuri, matunda yake yalikuwa ni mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Wanyama wa mwituni walipata kivuli chini yake, na ndege wa angani waliisha katika matawi yake. Viumbe vyote hai vililishwa katika mti huo.
Foliage its [was] beautiful and fruit its [was] plentiful and food for all [was] on it under it it had shade - [the] animal[s] of field the and in branches its (they nested *Q(K)*) [the] birds of heavens the and from it it fed all flesh.
13 Nilipokuwa nimelala kitandani kwangu, niliona katika akili zangu, mjumbe mtakatifu alishuka kutoka mbinguni.
Seeing I was in [the] visions of head my on bed my and lo! a watcher and a holy [one] from heavens the [was] coming down.
14 Alipiga kelele na kusema, 'Ukateni mti na yafyekeni matawi yake, yapukutisheni majani yake, na kuyasambaza matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege wapae mbali kutoka katika matawi yake.
[he was] proclaiming With power and as follows [he was] saying cut down! tree the and cut off! branches its strip off! foliage its and scatter! fruit its let it flee animal[s] the from under it and birds the from branches its.
15 Mkiache kisiki cha mizizi yake katika nchi, mkifunge na fungu la chuma na shaba, katikati ya mche mororo wa shambani. Na kilowanishwe na umande wa kutoka mbinguni. Kiacheni kiishi na wanyama kati ya mimea ya ardhini.
Nevertheless [the] stump of roots its in ground the leave! and with a fetter of iron and bronze in grass the of field the and with [the] dew of heavens the let it become wet and [be] with animal[s] the portion its in [the] grass of earth the.
16 Akili yake na ibadilishwe kutoka akili ya kibinadamu, na apewe akili ya mnyama mpaka ipite miaka saba.
Heart its away from (human the *Q(k)*) let it be changed and [the] heart of an animal let it be given to it and seven times let them pass over it.
17 Uamuzi huu ni kutokana na amri iliyotolewa na mjumbe. Ni uamuzi uliofanya na yeye aliye mtakatifu ili kwamba hao walio hai wajue kwamba Mungu aliye juu sana anatawala juu ya falme za watu na huwapa kwa kila mmoja apendaye kumweka juu yao, hata kwa watu wale wanyenyekevu sana.'
[is] by [the] decree of Watchers command the and [is by the] word of holy [ones] affair the to [the] cause that they will know living [people] the that [is] having mastery (Most High the *Q(k)*) over [the] kingdom of (human the *Q(k)*) and to whomever whom he will be pleased he will give it and a lowly [one] of humankind he will set up (over it. *Q(k)*)
18 Mimi, Mfalme Nebukadneza nilipata ndoto hii. Sasa, wewe Belteshaza, niambie tafsiri yake, kwasababu hakuna mtu mwenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunitafsiria. Lakini wewe unaweza kufanya hivyo, kwa kuwa roho ya miungu watakatifu iko ndani yako.”
This dream the I saw I king the Nebuchadnezzar (and you *Q(k)*) O Belteshazzar interpretation its - tell! as to because that - all [the] wise men of kingdom my not [are] able interpretation the to make known to me (and you *Q(k)*) [are] able who a spirit of gods holy [is] in you.
19 Ndipo Danieli aliyeitwa pia Belteshaza, alihuzunishwa kwa muda, na mawazo yake yalimshitua. Mfalme akasema, “Belteshaza, usifadhaishwe na ndoto au tafsiri yake.” Belteshaza akajibu, “Bwana wangu, ndoto hii na iwe kwa ajili ya watu wanaokuchukia, na tafsiri yake na iwe kwa ajili ya adui zako.
Then Daniel who name his [was] Belteshazzar he was appalled about a moment one and thoughts his they alarmed him [was] replying king the and [was] saying O Belteshazzar dream the and interpretation its may not it alarm you [was] replying Belteshazzar and [was] saying (O lord my *Q(k)*) dream the ([be] for enemy your *Q(K)*) and interpretation its ([be] for adversaries your. *Q(k)*)
20 Mti ule uliouona - uliokua na ukawa na wenye nguvu, na ambao sehemu yake ya juu ilifika hata mbinguni, na ambao waweza kuonekana kutoka miisho ya dunia yote -
Tree the which you saw which it grew great and it grew strong and height its it reached to heavens the and [the] sight of it [was] to all land the.
21 ambao majani yake ni mazuri, na matunda yake yalikuwa ni mengi, ili kwamba ndani yake kulikuwa na chakula cha wote, na chini yake wanyama wa mwituni walipata kivuli, na ndani yake ndege wa angani waliishi -
And foliage its [was] beautiful and fruit its [was] plentiful and food for all [was] on it under it it dwelt [the] animal[s] of field the and in branches its they dwelt [the] birds of heavens the.
22 huu mti ni wewe, mfalme, wewe uliyekua na kuwa na nguvu. Ukuu wako umeongezeka na kufika mbinguni, na mamlaka yako yamefika hata miisho ya dunia.
([is] you *Q(k)*) It king O who you have grown great and you have grown strong and greatness your it has grown great and it has reached to heavens the and dominion your [is] to [the] end earth the.
23 Ewe mfalme, ulimwona mjumbe akishuka kutoka mbinguni na akisema, “Ukateni mti na uteketezeni, lakni kiacheni kisiki cha mizizi yake katika nchi, kifungeni kwa ukanda wa chuma na shaba, katikati ya mche mororo katika shamba. Na kilowanishwe na umande kutoka mbinguni. Kiache kiishi katika wanyama wa mwituni katika mashamba mpaka ipite miaka saba.'
And that he saw king the a watcher and a holy [one] coming down - from heavens the and saying cut down! tree the and destroy it nevertheless [the] stump of roots its in ground the leave! and with a fetter of iron and bronze in grass the of field the and with [the] dew of heavens the let it become wet and [be] with [the] animal[s] of field the portion its until that seven times they will pass over it.
24 Mfalme, hii ni tafsiri yake. Ni agizo la Yeye Aliye Juu ambalo limekufikia, bwana wangu mfalme.
This [is] interpretation the king O and [is] [the] decree of (Most High the *Q(k)*) it which it has reached to (lord my *Q(k)*) king the.
25 Utafukuzwa utoke miongoni mwa watu, na utaishi pamoja na wanyama wa mwituni huko mashambani. Utafanywa uwe unakula majani kama ng'ombe, na utalowanishwa na umande wa kutoka mbinguni, miaka saba itapita mpaka pale utakapokiri kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme zote za watu na ya kwamba yeye humpa falme hizo mtu yeyote amtakaye.
And you [they will be] chasing away from humankind and with [the] animal[s] of field the it will be dwelling place your and grass like oxen - to you they will feed and from [the] dew of heavens the you [they will be] making wet and seven times they will pass (over you *Q(k)*) until that you will know that [is] having mastery (Most High the *Q(k)*) over [the] kingdom of humankind and to whomever whom he will be pleased he will give it.
26 Kama ilivyoamriwa kwamba kukiacha kisiki cha mizizi ya mti, kwa njia hii ufalme wako utarudishiwa katika kipindi ambacho utajifunza kwamba mbingu inatawala.
And that they said to leave [the] stump of roots its of tree the kingdom your to you [will be] enduring from that you will know that [are] having mastery heavens the.
27 Hivyo basi, mfalme, ushauri wangu na ukubalike kwako. Acha kutenda dhambi na utende haki. Geuka uache uovu wako wa kuonesha huruma kwa walionewa, na itakuwa kwamba mafanikio yako yataongezwa.”
Therefore king O advice my let it be acceptable (to you *Q(k)*) (and sin your *Q(K)*) by right doing break off! and iniquities your by showing mercy to poor people whether it will be a prolonging of prosperity your.
28 Vitu hivi vyote vilitokea kwa mfalme Nebukadneza.
Everything it came on Nebuchadnezzar king the.
29 Baada ya miezi wa kumi na miwili alipokuwa akitembea juu ya dari la ikulu ya kifalme katika Babeli,
To [the] end of months two [plus] ten on [the] palace of kingdom the of Babylon walking about he was.
30 na alisema, “Je hii si Babeli kuu, ambayo nimeijenga kwa ajili ya makao yangu ya kifalme, kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
[was] replying King the and [was] saying ¿ not [is] this it Babylon great which I I built it to a house of a kingdom by [the] strength of power my and for [the] honor of majesty my.
31 Wakati maneno yakali katika midomo ya mfalme, sauti ilisikika kutoka mbinguni: “Mfalme Nebukadneza, imetangazwa kwako kwamba ufalme huu umeondolewa kutoka kwako.
Still word the [was] in [the] mouth of king the a voice from heavens the it fell to you [they are] saying O Nebuchadnezzar king the kingdom the it has passed away from you.
32 Utafukuziwa mbali kutoka miongoni mwa watu, na makao yao yatakuwa pamoja na wanyama wa mwitu katika mashamba. Utafanywa kulamajani kama ng'ombe. Miaka saba itapita mpaka pale utakapokiri kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme za watu na humpa falme mtu yeyote amtakaye.”
And away from humankind you [they are] about to chase and [will be] with [the] animal[s] of field the dwelling place your grass like oxen to you they will feed and seven times they will pass (over you *Q(k)*) until that you will know that [is] having mastery (Most High the *Q(k)*) over [the] kingdom of humankind and to whomever whom he will be pleased he will give it.
33 Agizo hili kinyume na Nebukadneza lilitekelezwa ghafla. Aliondolewa miongoni mwa watu. Alikula majani kama ng'ombe, na mwili wake ulilowa kwa umande wa kutoka mbinguni. Nywele zake zilirefuka kama manyoa ya tai, na makucha yake yalikuwa kama makucha ya ndege.
At it moment the word the it was fulfilled on Nebuchadnezzar and away from humankind he was chased and grass like oxen he ate and from [the] dew of heavens the body his it became wet until that hair his like eagles it grew long and nails his [were] like birds.
34 Na katika mwisho wa siku, mimi, Nebukadneza niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, utimamu wa akili nilirudishiwa. “Nilimsifu Mungu Aliye Juu sana, na nilimheshimu na kumtukuza yeye aishiye milele. Kwa kuwa utawala wake ni wa milele, na ufalme wake unadumu katoka katika vizazi vyote hadi vizazi vyote.
And to [the] end of days the I Nebuchadnezzar eye my - to heavens the I lifted and understanding my on me it returned (and Most High the *Q(k)*) I blessed and [the] [one] living of perpetuity I praised and I glorified that dominion his [is] a dominion of perpetuity and kingdom his [is] with generation and generation.
35 Wenyeji wote wa duniani huhesabiwa na yeye kuwa bure; hufanya lolote limpendezalo miongoni mwa jeshi la mbinguni na wakazi wa dunia. Hakuna hata mmoja awezaye kumzuia au kumpa changamoto. Hakuna hata mmoja awezaye kumwambia, “Mbona umefanya hivi?”
And all ([the] inhabitants of *Q(k)*) earth the [are] as not considered and as pleases he [he is] doing with [the] army of heavens the (and [the] inhabitants of *Q(k)*) earth the and not there [is] who he will strike on hand his so he may say to him what? have you done.
36 Kwa wakati ule ule utimamu wa akili zangu uliponirudia, utukufu wangu na fahari yangu ilinirudia kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na watu wenye heshima walitafuta msaada wangu. Nilirudishwa kwenye kiti changu cha enzi, na nilipewa ukuu zaidi.
At it time the understanding my - it returned to me and to [the] honor of kingdom my majesty my and splendor my it returned to me and me counselors my and nobles my they sought and over kingdom my it was established and greatness surpassing it was added to me.
37 Sasa basi, mimi Nebukadneza, ninamsifu, ninamtukuza na kumheshimu mfalme wa mbinguni, kwa kuwa matendo yake yote ni ya haki, na njia zake ni za adili. Anaweza kuwashusha wale wanaotembea katika kiburi chao wenyewe.
Now I Nebuchadnezzar [am] praising and [am] lifting up and [am] glorifying [the] king of heavens the who all deeds his [are] truth and ways his [are] justice and [those] who [are] walking in pride [he is] able to bring low.

< Danieli 4 >