< Danieli 4 >

1 Mfalme Nebukadneza aliituma amri hii kwa watu wote, mataifa, na lugha walioishi katika nchi: “Na amani yenu na iongezeke.
Nebuchadnezzar, the king, to all peoples, nations, and languages, who dwell in the whole world, may peace be increased with you.
2 Imeonekana vizuri kwangu kuwaambia juu ya ishara na maajabu ambayo Mungu Mkuu Aliye juu amenifanyia.
The supreme God has accomplished signs and wonders with me. Therefore, it has pleased me to proclaim
3 Ni kwa namna gani Ishara zake ni kubwa, na ni kwa namna gani maajabu yake yana nguvu! Ufalme wake ni ufalme unaodumu milele, na utawala wake hudumu kizazi hadi kizazi.”
his signs, which are great, and his wonders, which are mighty. For his kingdom is an everlasting kingdom, and his power continues from generation to generation.
4 Mimi, Nebukadneza, nilikuwa ninaishi kwa furaha katika nyumba yangu, na nilikuwa nikifurahia mafanikio katika ikulu yangu.
I, Nebuchadnezzar, was content in my house and prospering in my palace.
5 Lakini ndoto niliyoiota ilifanya niogope. Nilipokuwa nimejilaza pale, taswira niliyoiona na maono katika akili yangu yalinitaabisha.
I saw a dream that terrified me, and my thoughts on my bed and the visions in my head disturbed me.
6 Basi nilitoa agizo la kuwaleta mbele yangu watu wote wa Babeli waliokuwa na hekima ili kwamba waweze kunitafsiria ndoto.
And so a decree was established by me, that all of the wise men of Babylon should be brought in before me, and that they should reveal to me the answer to the dream.
7 Kisha walikuja wachawi, wale ambao hudai kuzungumza na wafu, watu wenye hekima, na wasoma nyota. Niliwaambia juu ya ndoto, lakini hawakuweza kunitafsiria.
Then the seers, the astrologers, the Chaldeans, and the soothsayers entered, and I explained about the dream in their presence, but they did not reveal its answer to me.
8 Bali mwishoni Danieli aliingia ndani - yeye ambaye huitwa Belteshaza jina la mungu wangu, na ambaye ndani yake kuna roho ya miungu mitakatifu - na nilimwambia juu ya ndoto.
And then their colleague came in before me, Daniel, (whose name is Belteshazzar according to the name of my god, ) who has the spirit of the holy gods within his very self, and I told the dream directly to him.
9 “Belteshaza, mkuu wa wachawi, ninajua kuwa roho ya miungu watakatifu iko ndani yako na ya kwamba hakuna siri iliyo ngumu kwako. Niambie kile nilichokiona katika ndoto yangu na nini maana yake.
Belteshazzar, leader of the seers, since I know that you have in you the spirit of the holy gods, and that no mystery is unreachable to you, explain to me the visions of my dreams, which I saw, and the solution to them.
10 Haya ndiyo niliyoyaona katika akili zangu nilipokuwa nimejilaza katika kitanda changu: Nilitazama, na kulikuwa na mti katikati ya dunia, na urefu wake ulikuwa ni mkubwa sana.
This was the vision of my head on my bed. I looked, and behold, a tree in the middle of the earth, and its height was exceedingly great.
11 Mti ulikua na ukawa wenye nguvu. Na sehemu ya juu yake ilifika mbinguni, uliweza kuonekana kutoka miisho ya dunia yote.
The tree was great and strong, and its height reached up to heaven. It could be seen all the way to the ends of the entire earth.
12 Majani yake yalikuwa mazuri, matunda yake yalikuwa ni mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Wanyama wa mwituni walipata kivuli chini yake, na ndege wa angani waliisha katika matawi yake. Viumbe vyote hai vililishwa katika mti huo.
Its leaves were very beautiful, and its fruit was very abundant, and in it was food for the whole world. Under it, animals and beasts were dwelling, and in its branches, the birds of the sky were sheltered, and from it, all flesh was fed.
13 Nilipokuwa nimelala kitandani kwangu, niliona katika akili zangu, mjumbe mtakatifu alishuka kutoka mbinguni.
I saw in the vision of my head upon my blanket, and behold, a watcher and a holy one descended from heaven.
14 Alipiga kelele na kusema, 'Ukateni mti na yafyekeni matawi yake, yapukutisheni majani yake, na kuyasambaza matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege wapae mbali kutoka katika matawi yake.
He cried out loudly, and he said this: “Cut down the tree and prune its branches; shake off its leaves and scatter its fruits; let flee the beasts, which are under it, and the birds from its branches.
15 Mkiache kisiki cha mizizi yake katika nchi, mkifunge na fungu la chuma na shaba, katikati ya mche mororo wa shambani. Na kilowanishwe na umande wa kutoka mbinguni. Kiacheni kiishi na wanyama kati ya mimea ya ardhini.
Nevertheless, leave the stump of its roots in the earth, and let it be bound with a band of iron and brass among the plants, which are close by, and let it be touched by the dew of heaven, and let its place be with the wild animals among the plants of the earth.
16 Akili yake na ibadilishwe kutoka akili ya kibinadamu, na apewe akili ya mnyama mpaka ipite miaka saba.
Let his heart be changed from being human, and let the heart of a wild animal be given to him, and let seven periods of time pass over him.
17 Uamuzi huu ni kutokana na amri iliyotolewa na mjumbe. Ni uamuzi uliofanya na yeye aliye mtakatifu ili kwamba hao walio hai wajue kwamba Mungu aliye juu sana anatawala juu ya falme za watu na huwapa kwa kila mmoja apendaye kumweka juu yao, hata kwa watu wale wanyenyekevu sana.'
This is the decree from the judgment of the watchers, and the decision and proclamation of the holy ones, until the living shall know that the Supreme One is ruler in the kingdom of men, and that he will give it to whomever he wills, and he will appoint the lowest man over it.”
18 Mimi, Mfalme Nebukadneza nilipata ndoto hii. Sasa, wewe Belteshaza, niambie tafsiri yake, kwasababu hakuna mtu mwenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunitafsiria. Lakini wewe unaweza kufanya hivyo, kwa kuwa roho ya miungu watakatifu iko ndani yako.”
I, king Nebuchadnezzar, saw this dream. And so you, Belteshazzar, must quickly explain to me the interpretation because all the wise men of my kingdom are not able to declare the meaning of it to me. But you are able because the spirit of the holy gods is in you.
19 Ndipo Danieli aliyeitwa pia Belteshaza, alihuzunishwa kwa muda, na mawazo yake yalimshitua. Mfalme akasema, “Belteshaza, usifadhaishwe na ndoto au tafsiri yake.” Belteshaza akajibu, “Bwana wangu, ndoto hii na iwe kwa ajili ya watu wanaokuchukia, na tafsiri yake na iwe kwa ajili ya adui zako.
Then Daniel, whose name was Belteshazzar, began silently to think within himself for about one hour, and his thoughts troubled him. But the king responded, saying, “Belteshazzar, do not let the dream and its interpretation disturb you.” Belteshazzar answered and said, “My lord, the dream is for those who hate you, and its interpretation may be for your enemies.
20 Mti ule uliouona - uliokua na ukawa na wenye nguvu, na ambao sehemu yake ya juu ilifika hata mbinguni, na ambao waweza kuonekana kutoka miisho ya dunia yote -
The tree that you saw was lofty and strong; its height reached toward heaven, and it could be seen throughout the whole world.
21 ambao majani yake ni mazuri, na matunda yake yalikuwa ni mengi, ili kwamba ndani yake kulikuwa na chakula cha wote, na chini yake wanyama wa mwituni walipata kivuli, na ndani yake ndege wa angani waliishi -
And its branches were very beautiful, and its fruit very abundant, and in it was food for all. Under it, dwelt the beasts of the field, and in its branches, the birds of the air stayed.
22 huu mti ni wewe, mfalme, wewe uliyekua na kuwa na nguvu. Ukuu wako umeongezeka na kufika mbinguni, na mamlaka yako yamefika hata miisho ya dunia.
It is you, O king, who has been greatly esteemed, and you have grown strong. And you have increased your power, and it reaches towards heaven, and your rule is to the ends of the whole earth.
23 Ewe mfalme, ulimwona mjumbe akishuka kutoka mbinguni na akisema, “Ukateni mti na uteketezeni, lakni kiacheni kisiki cha mizizi yake katika nchi, kifungeni kwa ukanda wa chuma na shaba, katikati ya mche mororo katika shamba. Na kilowanishwe na umande kutoka mbinguni. Kiache kiishi katika wanyama wa mwituni katika mashamba mpaka ipite miaka saba.'
Yet the king also saw a watcher and a holy one descend from heaven and say: ‘Cut down the tree and scatter it; however, leave the stump of its roots in the earth, and let it be bound with iron and brass, among the surrounding plants, and let it be sprinkled with the dew of heaven, and let his feeding be with the wild beasts, until seven periods of time pass over him.’
24 Mfalme, hii ni tafsiri yake. Ni agizo la Yeye Aliye Juu ambalo limekufikia, bwana wangu mfalme.
This is the interpretation of the judgment of the Most High, which has reached my lord, the king.
25 Utafukuzwa utoke miongoni mwa watu, na utaishi pamoja na wanyama wa mwituni huko mashambani. Utafanywa uwe unakula majani kama ng'ombe, na utalowanishwa na umande wa kutoka mbinguni, miaka saba itapita mpaka pale utakapokiri kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme zote za watu na ya kwamba yeye humpa falme hizo mtu yeyote amtakaye.
They will expel you from among men, and your dwelling will be with the beasts and the wild animals, and you will eat hay like an ox, and you will be drenched with the dew of heaven. Likewise, seven periods of time will pass over you, until you know that the Supreme One rules over the kingdom of men, and he gives it to whomever he wills.
26 Kama ilivyoamriwa kwamba kukiacha kisiki cha mizizi ya mti, kwa njia hii ufalme wako utarudishiwa katika kipindi ambacho utajifunza kwamba mbingu inatawala.
But, since he commanded that the stump of its roots, that is, of the tree, should be left behind, your kingdom will be left for you, after you have realized that power is from divinity.
27 Hivyo basi, mfalme, ushauri wangu na ukubalike kwako. Acha kutenda dhambi na utende haki. Geuka uache uovu wako wa kuonesha huruma kwa walionewa, na itakuwa kwamba mafanikio yako yataongezwa.”
Because of this, O king, let my counsel be acceptable to you. And redeem your sins with alms, and your iniquities with mercy towards the poor. Perhaps he will forgive your offenses.”
28 Vitu hivi vyote vilitokea kwa mfalme Nebukadneza.
All these things came upon king Nebuchadnezzar.
29 Baada ya miezi wa kumi na miwili alipokuwa akitembea juu ya dari la ikulu ya kifalme katika Babeli,
After the end of twelve months, he was taking a walk in the palace of Babylon.
30 na alisema, “Je hii si Babeli kuu, ambayo nimeijenga kwa ajili ya makao yangu ya kifalme, kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
And the king spoke out loud, saying, “Isn’t this the great Babylon, which I have built, as the home of the kingdom, by the strength of my power and in the glory of my excellence?”
31 Wakati maneno yakali katika midomo ya mfalme, sauti ilisikika kutoka mbinguni: “Mfalme Nebukadneza, imetangazwa kwako kwamba ufalme huu umeondolewa kutoka kwako.
And while the words were still in the king’s mouth, a voice rushed down from heaven, “To you, O king Nebuchadnezzar, it is said: ‘Your kingdom will be taken away from you,
32 Utafukuziwa mbali kutoka miongoni mwa watu, na makao yao yatakuwa pamoja na wanyama wa mwitu katika mashamba. Utafanywa kulamajani kama ng'ombe. Miaka saba itapita mpaka pale utakapokiri kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme za watu na humpa falme mtu yeyote amtakaye.”
and they will expel you from among men, and your dwelling will be with the beasts and the wild animals. You will eat hay like an ox, and seven times will pass over you, until you know that the Supreme One rules in the kingdom of men, and he gives it to whomever he wills.’”
33 Agizo hili kinyume na Nebukadneza lilitekelezwa ghafla. Aliondolewa miongoni mwa watu. Alikula majani kama ng'ombe, na mwili wake ulilowa kwa umande wa kutoka mbinguni. Nywele zake zilirefuka kama manyoa ya tai, na makucha yake yalikuwa kama makucha ya ndege.
The same hour, the sentence was fulfilled upon Nebuchadnezzar, and he was driven away from among men, and he ate hay like an ox, and his body was drenched with the dew of heaven, until his hair increased like the feathers of eagles, and his nails like those of birds.
34 Na katika mwisho wa siku, mimi, Nebukadneza niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, utimamu wa akili nilirudishiwa. “Nilimsifu Mungu Aliye Juu sana, na nilimheshimu na kumtukuza yeye aishiye milele. Kwa kuwa utawala wake ni wa milele, na ufalme wake unadumu katoka katika vizazi vyote hadi vizazi vyote.
Therefore, at the end of these days, I, Nebuchadnezzar, lifted up my eyes to heaven, and my mind was restored to me. And I blessed the Most High, and I praised and glorified him who lives forever. For his power is an everlasting power, and his kingdom is from generation to generation.
35 Wenyeji wote wa duniani huhesabiwa na yeye kuwa bure; hufanya lolote limpendezalo miongoni mwa jeshi la mbinguni na wakazi wa dunia. Hakuna hata mmoja awezaye kumzuia au kumpa changamoto. Hakuna hata mmoja awezaye kumwambia, “Mbona umefanya hivi?”
And all the inhabitants of the earth are reputed as nothing before him. For he acts according to his own will, with the inhabitants of the earth just as with the holy inhabitants of heaven. And there is no one who can resist his hand, or say to him, “Why have you done this?”
36 Kwa wakati ule ule utimamu wa akili zangu uliponirudia, utukufu wangu na fahari yangu ilinirudia kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na watu wenye heshima walitafuta msaada wangu. Nilirudishwa kwenye kiti changu cha enzi, na nilipewa ukuu zaidi.
At the same time, my mind returned to me, and I arrived at the honor and glory of my kingdom. And my appearance was given back to me. And my nobles and my magistrates needed me. And I was restored to my kingdom, and even greater majesty was added to me.
37 Sasa basi, mimi Nebukadneza, ninamsifu, ninamtukuza na kumheshimu mfalme wa mbinguni, kwa kuwa matendo yake yote ni ya haki, na njia zake ni za adili. Anaweza kuwashusha wale wanaotembea katika kiburi chao wenyewe.
Therefore I, Nebuchadnezzar, now praise, and magnify, and glorify the King of heaven, because all his works and the judgments of his way are true, and those who go forth in arrogance, he is able to bring low.

< Danieli 4 >