< Danieli 3 >

1 Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu ambayo ilikuwa na urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa sita. Aliiweka katika uwanda wa Dura katika jimbo la Babeli.
Nebuchadnezzar the king has made an image of gold, its height sixty cubits, its breadth six cubits; he has raised it up in the Valley of Dura, in the province of Babylon;
2 Kisha Nebukadneza alituma ujumbe wa kuwaita pamoja magavana wote wa majimbo, magavana wa mikoa, na magavana wa vijiji, pamoja na na washauiri, wahazini, waamuzi, mahakimu, na maafisa wengine wakuu wa majimbo ili waje kwa ajili ya uzinduzi wa sanamu aliyokuwa ameiweka.
and Nebuchadnezzar the king has sent to gather the satraps, the prefects, and the governors, the counselors, the treasurers, the judges, the magistrates, and all the rulers of the province, to come to the dedication of the image that Nebuchadnezzar the king has raised up.
3 Ndipo magavana wa majimbo, magavana wa mikoa, na magavana wa vijiji, pamoja na washauri, wahasibu, waamuzi, mahakimu, na maafisa wa juu wa majimbo walikusanyika kwa pamoja katika uzinduzi wa sanamu ambayo Nebukadneza aliyokuwa ameiweka. Walisimama mbele yake.
Then are gathered the satraps, the prefects, and the governors, the counselors, the treasurers, the judges, the magistrates, and all the rulers of the province, to the dedication of the image that Nebuchadnezzar the king has raised up: and they are standing before the image that Nebuchadnezzar has raised up.
4 Kisha mtangazaji alipiga kelele, “Enyi watu, mataifa, na lugha mmeamriwa
And a crier is calling mightily: “They are saying to you: O peoples, nations, and languages!
5 kwamba mtakaposikia sauti za pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinubi na zumari na aina zote za muziki, ni sharti kuanguka na kuisujudia ninyi wenyewe sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameiweka.
At the time that you hear the voice of the horn, the flute, the harp, the lyre, the stringed instrument, the symphony, and all kinds of music, you fall down and pay respect to the golden image that Nebuchadnezzar the king has raised up:
6 Na yeyote asiyeanguka na kuiabuda, kwa wakati huo huo atatupwa katika tanuru la moto.”
and whoever does not fall down and pay respect, in that hour he is cast into the midst of a burning fiery furnace.”
7 Basi watu walilposikia sauti za pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinubi na zumari na aina zote za muziki, watu wote, mataifa na lugha walianguka na kuisujudia wao wenyewe sanamu ya dhahabu ambayo Nebukadneza mfalme alikuwa ameiweka.
Therefore at that time, when all the peoples are hearing the voice of the horn, the flute, the harp, the lyre, the stringed instrument, and all kinds of music, falling down are all the peoples, nations and languages, worshiping the golden image that Nebuchadnezzar the king has raised up.
8 Wakati huu baadhi ya Walkadayo walikuja na kuleta mashitaka kinyume na Wayahudi.
Therefore at that time certain Chaldeans have drawn near, and accused the Jews;
9 Walimwambia mfalme Nebukadneza, “mfalme aishi milele!
they have answered, indeed, they are saying to Nebuchadnezzar the king, “O king, live for all ages!
10 Ewe mfalme, umeweka amri kwamba kila mtu aisikiye sauti ya pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinubi na zumari, na aina zote za muziki, lazima kuanguka na kuisujudia sanamu ya dhahabu.
You, O king, have made a decree that every man who hears the voice of the horn, the flute, the harp, the lyre, the stringed instrument, and the symphony, and all kinds of music, falls down and pays respect to the golden image;
11 Mtu yeyote asiyeanguka na kuiabudu sharti atupwe katika tanuru linalowaka moto.
and whoever does not fall down and pay respect, is cast into the midst of a burning fiery furnace.
12 Sasa kuna baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu masuala ya jimbo la Babeli; majina yao ni Shadraka, Meshaki, na Abednego. Mfalme, hawa watu hawakutii wewe. Hawataiabudu, kuitumikia wala kuisujudia wenyewe sanamu ya dhahabu ambayo umeiweka.”
There are certain Jews whom you have appointed over the work of the province of Babylon—Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, these men have not made of you, O king, [any] regard; your gods they are not serving, and to the golden image you have raised up—are not making worship.”
13 Ndipo Nebukadneza alijawa na hasira na ghadhabu, aliagiza kwamba Shadraka, Meshaki na Abednego waletwe kwake. Hivyo, waliwalete hawa watu mbele ya mfalme.
Then Nebuchadnezzar, in anger and fury, has said to bring in Shadrach, Meshach, and Abed-Nego. Then these men have been brought in before the king.
14 Nebukadneza aliwaambia, “Je mmejipanga katika akili zenu, enyi Shadraka, Meshaki na Abedinego, kwamba hamtaiabudu miungu yangu wala kuisujudia wenyewe sanamu ile ya dhahabu ambayo nimeiweka?
Nebuchadnezzar has answered and said to them, “Is [it] a laid plan, O Shadrach, Meshach, and Abed-Nego—my gods you are not serving, and to the golden image that I have raised up you are not worshiping?
15 Basi sasa kama mko tayari - mtakaposikia sauti pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinumbi na zumari, aina zote za muziki - kuanguka chini na kuisujudia wenyewe sanamu ile ambayo nimeitengeneza, mambo yote yatakuwa mazuri. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa mara katika tanuru la moto. Ni mungu gani atakayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?”
Now behold, you are ready, so that at the time that you hear the voice of the horn, the flute, the harp, the lyre, the stringed instrument, and the symphony, and all kinds of music, you fall down and pay respect to the image that I have made! But if you do not worship—in that hour you are cast into the midst of a burning fiery furnace; who is that God who delivers you out of my hands?”
16 Shadraka, Meshaki, na Abednego wakamjibu mfalme, “Nebukadneza, hatuhitaji kukujibu wewe katika jambo hili.
Shadrach, Meshach, and Abed-Nego have answered, indeed, they are saying to King Nebuchadnezzar, “We have no need concerning this matter to answer you.
17 Kama kuna jibu, ni kwamba Mungu wetu ambaye tunamtumikia anaweza kutuhifadhi sisi salama katika katika tanuru la moto, na atatuokoa sisi katika mkono wako, mfalme.
Behold, it is; our God whom we are serving, is able to deliver us from a burning fiery furnace; and from your hand, O king, He delivers.
18 Kama sivyo, na ijulikane kwako, wewe mfalme, kwamba hatutaiabudu miungu yako, na wala hatutaisujudia wenyewe sanamu ya dhahabu uliyoiweka.
And behold—not! Be it known to you, O king, that we are not serving your gods, and we do not worship the golden image you have raised up.”
19 Ndipo Nebukadneza alijawa na ghadhabu; mwonekano wa uso wake ulibadilika kinyume na Shadraka, Meshaki na Abedinego. Aliagiza kuwa tanuru lichochewe ukali mara saba zaidi kuliko lilivyokuwa kawaida.
Then Nebuchadnezzar has been full of fury, and the expression of his face has been changed concerning Shadrach, Meshach, and Abed-Nego; he answered and said to heat the furnace seven times above that which it is seen to be heated;
20 Kisha aliwaamuru baadhi ya watu wenye nguvu katika jeshi lake kuwafunga Shadraka, Meshaki na Abednego na kuwatupa katika tanuru liwakalo moto.
and to certain mighty men who [are] in his force he has said to bind Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, to cast into the burning fiery furnace.
21 Walifungwa akali wakiwa wamevaa nguo zao, kanzu, kilemba, na mavazi mengine, na walitupa katika tanuru liwakalo moto.
Then these men have been bound in their coats, their tunics, and their turbans, and their clothing, and have been cast into the midst of the burning fiery furnace.
22 Kwasababu ya agizo la mfalme lilifuatwa na tanuru lilikuwa na joto sana, miali ya moto iliwaua watu waliowatupa Shadraka, Meshaki, na Abedinego.
Therefore, because that the word of the king is urgent, and the furnace heated exceedingly, those men who have taken up Shadrach, Meshach, and Abed-Nego—the spark of the fire has killed them.
23 Hawa wanaume watatu, Shadraka, Meshaki, na Abednego, waliangukia katika tanuru liwakalo moto wakali wamefungwa.
And these three men, Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, have fallen down in the midst of the burning fiery furnace—bound.
24 Kisha Nebukadneza mfalme alishangazwa na alisimam haraka. Aliwauliza washauri wake, “Je hatukutupa watu watatu wakiwa wamefungwa katika moto?” Nao walimjibu mfalme, “Hakika mfalme.”
Then Nebuchadnezzar the king has been astonished, and has risen in haste; he has answered and said to his counselors, “Have we not cast three men into the midst of the fire—bound?” They have answered and are saying to the king, “Certainly, O king.”
25 Alisema, “Lakini ninaona watu wanne ambao hawajafungwa wakizunguka katika moto, na hawajaumizwa. Mng'ao wa mtu wa nne ni kama mwana wa miungu.”
He answered and has said, “Behold, I am seeing four men loose, walking in the midst of the fire, and they have no hurt; and the appearance of the fourth [is] like to a son of the gods.”
26 Ndipo Nebukadneza aliposogea karibu na mlango wa tanuru liwakalo moto na akaaita, “Shadraka, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu, tokeni nje! Njooni hapa! Ndipo Shadraka, Meshaki na Abednego walitoka nje ya moto.
Then Nebuchadnezzar has drawn near to the gate of the burning fiery furnace; he has answered and said, “Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, servants of God Most High come forth, indeed, come”; then Shadrach, Meshach, and Abed-Nego come forth, from the midst of the fire;
27 Magavana wa majimbo, magavana wengine, na washauri wa mfalme waliokuwa wamekusanyika kwa pamoja waliwaona watu hawa. Moto haukuunguza miili yao; nywele katika vichwa vyao hazikuungua; mavazi yao yalikuwa hayajaharibiwa; na hawakuwa na harufu ya moto.
and gathered together, the satraps, the prefects, and the governors, and the counselors of the king, are seeing these men, that the fire has no power over their bodies, and the hair of their head has not been singed, and their coats have not changed, and the smell of fire has not passed on them.
28 Nebukadneza alisema, “Na tumsifu Mungu wa Shadraka, Meshaki na Abedinego, ambaye amemtuma mjumbe wake na amewapa ujumbe watumishi wake. Walimtumaini yeye wakati walipoikana amri yangu, na waliitoa miili yao badala ya kuabudu au kusujudia mungu mwingine isipokuwa Mungu wao.
Nebuchadnezzar has answered and has said, “Blessed [is] the God of Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, who has sent His messenger, and has delivered His servants who trusted on Him.” And the word of the king changed, and gave up their bodies that they might not serve nor pay respect to any god except to their own God.
29 Hivyo basi ninaagiza kwamba watu wote, taifa au lugha ambayo itazungumza kitu chochote kinyume na Mungu wa Shadraka, Meshaki na Abedinego lazima wakatwe vipande, na ya kwamba nyumba zao lazima zifanywe kuwa vichuguu vya uchafu kwasababu hakuna mungu mwingine anayeweza kuokoa kama hivi.”
“And by me a decree is made, that any people, nation, and language, that speaks erroneously concerning the God of Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, he is made pieces, and its house is made a dunghill, because that there is no other god who is able thus to deliver.”
30 Ndipo mfalme aliwapandisha cheo Shadraka, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.
Then the king has caused Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, to prosper in the province of Babylon.

< Danieli 3 >