< Danieli 2 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Nebukadneza, alikuwa na ndoto. Akili yake ilisumbuka, na hakuweza kulala.
In the secounde yeer of the rewme of Nabugodonosor, Nabugodonosor siy a dreem; and his spirit was aferd, and his dreem fledde awei fro hym.
2 Ndipo mfalme alipowaita waganga na wale wenye kuongea na wafu. Lakini pia aliwaita wachawi na watu wenye hekima. Aliwataka wamwambie juu ya ndoto zake. Basi walikuja na kusimama mbele za mfalme.
Therfor the kyng comaundide, that the dyuynours, and astronomyens, and witchis, and Caldeis schulden be clepid togidere, that thei schulden telle to the kyng hise dremys; and whanne thei weren comun, thei stoden bifor the king.
3 Mfalme akawambia, “Nilikuwa na ndoto, na akili yangu ina mashaka nataka kujua ndoto hiyo nini maana yake.”
And the king seide to hem, Y siy a dreem, and Y am schent in mynde, and Y knowe not what Y siy.
4 Kisha watu wenye hekima wakamwambia mfalme katika Kiaramaiki, “Mfalme, aishi milele! Twambie sisi ndoto, watumishi wako, nasi tutaifunua maana yake.”
And Caldeis answeriden the kyng bi Sirik langage, Kyng, liue thou with outen ende; seie thi dreem to thi seruauntis, and we schulen schewe to thee the expownyng therof.
5 Mfalme akawajibu watu wenye hekima, “Jambo hili limeshamalizika. Kama hamtaweza kuiweka wazi ndoto kwangu na kuitafsiri, miili yenu itakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vichuguu vya uchafu.
And the kyng answeride, and seide to Caldeis, The word is goen awei fro me; if ye schewen not to me the dreem, and expownyng therof, ye schulen perische, and youre housis schulen be forfetid.
6 Lakini kama mtaniambia ndoto na maana yake, mtapokea zawadi kutoka kwangu, thawabu, na heshima kubwa. Basi niambie ndoto na maana yake.”
Forsothe if ye tellen the dreem, and the expownyng therof, ye schulen take of me meedis and yiftis, and myche onour; therfor schewe ye to me the dreem, and the interpretyng therof.
7 Wakamjibu tena na kusema, “Mfalme na atuambie, watumishi wake, ndoto nasi tukwambia maana yake.”
Thei answeriden the secounde tyme, and seiden, The kyng seie the dreem to hise seruauntis, and we schulen schewe the interpretyng therof.
8 Mfalme akawajibu, “Ninajua kwa hakika mnahitaji muda zaidi kwasababu mmeona maamuzi yangu ni magumu kuhusu jambo hili.
The kyng answeride, and seide, Certis Y woot, that ye ayenbien the tyme, and witen that the word is goen awei fro me.
9 Lakini kama hamtaweza kuniambia ndoto, kuna sentensi moja tu kwa ajili yenu. Mmeamua kuandaa uongo na maneno ya kudanganya ambayo mmekubaliana kwa pamoja kuniambia mpaka pale nitakapobadili akili zangu. Basi, niambieni ndoto, na kisha nitajua kuwa mnaweza kuitafsiri kwa ajili yangu.”
Therfor if ye schewen not to me the dreem, o sentence is of you, for ye maken an interpretyng bothe fals and ful of disseit, that ye speke to me til the tyme passe; therfor seie ye the dreem to me, that Y wite, that ye speke also the veri interpretyng therof.
10 Watu wenye hekima wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu katika dunia anayeweza kutimiza matakwa ya mfalme. Hakuna mfalme yoyote mkuu na mwenye nguvu ambaye alishataka jambo kama hilo kutoka kwa wachawi, wala wenye kuongea na wafu, wala mwenye hekima.
Therfor Caldeis answeriden bifor the kyng, and seiden, Kyng, no man is on erthe, that mai fille thi word; but nether ony greet man and myyti of kyngis axith siche a word of ony dyuynour, and astronomyen, and of a man of Caldee.
11 Kile anachokitaka mfalme ni kigumu, na hakuna yeyote awezaye kumwambia mfalme isipokuwa miungu, ambayo haishi miongoni mwa watu.”
For the word which thou, kyng, axist, is greuouse, nether ony schal be foundun, that schal schewe it in the siyt of the king, outakun goddis, whos lyuyng is not with men.
12 Jambo hili lilimfanya mfalme akasirike na kughadhabika sana, na alitoa amri kuwaangamiza wale wote waliojulikana kuwa ni wenye hekima zao katika Babeli.
And whanne this word was herd, the kyng comaundide, in woodnesse and in greet ire, that alle the wise men of Babiloyne schulden perische.
13 Hivyo, amri ilitoka kwamba wale wote waliojulikana kwa hekima yao ni lazima wauawe. Na kwa sababu ya amri hii, walimtafuta Daniel na rafiki zake ili kwamba wauawe.
And bi the sentence goon out, the wise men weren slayn; and Danyel and hise felows weren souyt, that thei schulden perische.
14 Ndipo Daniel alipomjibu kwa busara na umakini, Arioki, kamanda wa walinzi wa mfalme, ambaye alikuwa amekuja kuwaua wale wote waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
Thanne Danyel axide of the lawe and sentence, of Ariok, prynce of chyualrie of the kyng, that was gon out to sle the wise men of Babiloyne.
15 Danieli alimwuliza kamanda wa mfalme, “Kwanini amri ya mfalme ni ya haraka hivyo?” Hivyo, Arioki akamwambia Danieli kile kilichotokea.
And he axide hym, that hadde take power of the kyng, for what cause so cruel a sentence yede out fro the face of the kyng. Therfor whanne Ariok hadde schewid the thing to Danyel,
16 Ndipo Danieli aliingia ndani na akaomba ahadi ya muda wa kuonana na mfalme ili kwamba aweze kuwasilisha tafsiri kwa mfalme.
Danyel entride, and preyede the kyng, that he schulde yyue tyme to hym to schewe the soilyng to the kyng.
17 Kisha Danieli aliingia ndani ya nyumba na aliwaelezea Hanania, Mishaeli, na Azaria, kile kilichotokea.
And he entride in to his hous, and schewide the nede to Ananye, and to Misael, and Asarie,
18 Aliwasihi kutafuta rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusiana na siri hii ili kwamba yeye na wao wasije wakauawa pamoja na watu wengine waliosalia waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
hise felowis, that thei schulden axe merci of the face of God of heuene on this sacrament; and that Danyel and hise felowis schulden not perische with othere wise men of Babiloyne.
19 Usiku ule siri ilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Kisha Danieli akamtukuza Mungu wa mbinguni
Thanne the priuyte was schewid to Danyel bi a visioun in nyyt. And Danyel blesside God of heuene, and seide,
20 na kusema, “Litukuzwa jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na nguvu ni zake.
The name of the Lord be blessid fro the world, and til in to the world, for wisdom and strengthe ben hise;
21 Anabadili wakati na majira; anaondoa wafalme na kuweka wafalme katika viti vyao vya enzi. Anawapa hekima wenye hekima na ufahamu kwa wenye weledi.
and he chaungith tymes and ages, he translatith rewmes and ordeyneth; he yyueth wisdom to wise men, and kunnyng to hem that vndurstonden techyng, ether chastisyng;
22 Hufunua vitu vya chini na vilifichika kwa sababu anajua kile kilicho gizani, naye anaishi pamoja na mwanga.
he schewith deepe thingis and hid, and he knowith thingis set in derknessis, and liyt is with hym.
23 Mungu wa baba zetu, ninakushukuru na kukutukuza wewe kwa ajili ya hekima na nguvu uliyonipa. Sasa umeyafanya yawe wazi kwetu yale tuliyokuomba; umetujulisha mambo yamhusuyo mfalme.”
God of oure fadris, Y knowleche to thee, and Y herie thee, for thou hast youe wisdom and strengthe to me; and now thou hast schewid to me tho thingis, whiche we preieden thee, for thou hast openyd to vs the word of the kyng.
24 Ndipo Danieli alienda kumwona Arioki ( yule ambaye mfalme alimchagua kuua kila mtu aliyekuwa na hekima katika Babeli). Alimwendea na kumwambia, “Usiwauwe watu wenye hekima katika Babeli. Nipeleke kwa mfalme na nitamwonesha mfalme tafsiri ya ndoto yake.”
Aftir these thingis Danyel entride to Ariok, whom the kyng hadde ordeyned, that he schulde leese the wise men of Babiloyne, and thus he spak to hym, Leese thou not the wise men of Babiloyne; leede thou me in bifor the siyt of the kyng, and Y schal telle the soilyng to the kyng.
25 Kisha Arioki kwa haraka alimleta Danieli mbele za mfalme na kusema, “Nimempata miongoni wa watu wa mateka wa Yuda mtu ambaye atafunua maana ya ndoto ya mfalme.”
Thanne Ariok hastynge ledde in Danyel to the kyng, and seide to him, Y haue foundun a man of the sones of passyng ouer of Juda, that schal telle the soilyng to the kyng.
26 Mfalme akamwambia Danieli (ambaye alikuwa akiitwa Beliteshaza), “Je unaweza kunimbia ndoto niliyoiona na maana yake?”
The kyng answeride, and seide to Danyel, to whom the name was Balthasar, Whethir gessist thou, that thou maist verili schewe to me the dreem which Y siy, and the interpretyng therof?
27 Danieli alimjibu mfalme na kusema, “Siri ambayo mfalme ameiomba haiwezi kufunuliwa na watu wenye hekima, wala wale wenye kuongea na wafu, wala wachawi, na wala wataalamu wa nyota.
And Danyel answeride bifore the king, and seide, The priuytee which the kyng axith, wise men, and astronomyens, and dyuynours, and lokeris of auteris, moun not schewe to the kyng.
28 Isipokuwa kuna Mungu ambaye anaishi mbinguni, ambaye hufunua siri, na amekwisha kukujulisha wewe, mfalme Nebukadneza, kile kitakachotokea katika siku zijazo. Hizi ndizo Ndoto na maono ya akili zako uliyoyaona wakati ulipokuwa umelala kitandani mwako.
But God is in heuene, that schewith priuytees, which hath schewid to thee, thou king Nabugodonosor, what thingis schulen come in the laste tymes. Thi dreem and visiouns of thin heed, in thi bed, ben sich.
29 Na kwako Wewe, mfalme, mawazo yako kitandani mwako yalikuwa ni juu ya mambo yajayo, na yule afichuaye siri ameifanya ijulikane kwako kuhusu kile kilicho karibu kutokea.
Thou, kyng, bigunnest to thenke in thi bed, what was to comynge aftir these thingis; and he that schewith priuetees, schewide to thee what thingis schulen come.
30 Na kuhusu mimi, siri hii haikufunuliwa kwangu kwa sababu ya hekima yoyote niliyo nayo zaidi ya mtu yoyote anayeishi. Siri hii imefunliwa kwangu ili kwamba wewe, mfalme, uweze kufahamu maana, na ili kwamba ujuwe mawazo yaliyo ndani mwako.
And this sacrament is schewid to me, not bi wisdom which is in me more than in alle lyuynge men, but that the interpretyng schulde be maad opyn to the kyng, and thou schuldist knowe the thouytis of thi soule.
31 Mfalme, uliangalia juu na ukaona sanamu kubwa. Sanamu hii ambayo ilikuwa yenye nguvu na yenye kung'aa, ilisimama mbele yako. Mng'ao wake ulikuwa unatisha.
Thou, kyng, siyest, and lo! as o greet ymage; thilke ymage was greet, and hiy in stature, and stood bifore thee, and the loking therof was ferdful.
32 Kichwa cha sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi. Matiti yake na mikono ilikuwa ya fedha. Sehemu ya katikati na mapaja yake yalikuwa yametengenezwa kwa shaba,
The heed of this ymage was of best gold, but the brest and armes weren of siluer; certis the wombe and thies weren of bras,
33 na miguu yake ilikuwa imetengenezwa kwa chuma. Miguu yake ilikuwa ilitengenezwa kwa sehemu chuma na sehemu kwa udongo.
but the leggis weren of irun; forsothe sum part of the feet was of irun, sum was of erthe.
34 Ulitazama juu, na jiwe lilikuwa limechongwa, ingawa si kwa mikono ya wanadamu, na liliipiga sanamu katika miguu yake ya chuma na udongo, na ponda ponda.
Thou siyest thus, til a stoon was kit doun of the hil, with outen hondis, and smoot the ymage in the irun feet therof and erthene feet, and al to-brak tho.
35 Kisha chuma, udongo, fedha, na dhahabu zilivunjwa katika vipande vipande kwa wakati mmoja na yakawa kama makapi yaliyo katika sakafu za kupuria kipindi cha kiangazi. Upepo huyapeperushia mbali na hakuna alama inayoachwa. Lakini jiwe lililoipiga sanammu likawa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote.
Thanne the irun, tijl stoon, ether erthene vessel, bras, siluer, and gold, weren al to-brokun togidere, and dryuun as in to a deed sparcle of a large somer halle, that ben rauyschid of wynd, and no place is foundun to tho; forsothe the stoon, that smoot the ymage, was maad a greet hil, and fillide al erthe.
36 Hii ndiyo ilikuwa ndotoyako. Na sasa tutamwambia mfalme maana yake.
This is the dreem. Also, thou kyng, we schulen seie bifor thee the interpretyng therof.
37 Wewe, mfalme, ni mfalme wa wafalme kwa wale ambao Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, nguvu, uweza na heshima.
Thou art kyng of kyngis, and God of heuene yaf to thee rewme, strengthe, and empire, and glorie;
38 Amevitia mkononi mwako sehemu ambazo binadamu huishi. Amekupa wanyama wa mwituni na ndege wa angani katika mkono wako, na amekufanya wewe utawale juu yao wote. Wewe u kichwa cha dhahabu cha sanamu.
and he yaf in thin hond alle thingis, in whiche the sones of men, and the beestis of the feeld, and the briddis of the eir dwellen, and ordeynede alle thingis vndur thi lordschip; therfor thou art the goldun heed.
39 Baada yako, ufalme mwingine utainuka ambao ni mdogo kwako, na hata ufalme wa tatu wa shaba utatawala juu ya dunia yote.
And another rewme lesse than thou schal rise aftir thee; and the thridde rewme, an other of bras, that schal haue the empire of al erthe.
40 Kutakuwa na ufalme wa tatu, wenye nguvu kama chuma, kwa kuwa chuma huvunja vipande vipande vitu vingine na kuponda ponda kila kitu. Itaviharibu vitu hivi vyote na kuvisaga.
And the fourthe rewme schal be as irun, as irun makith lesse, and makith tame alle thingis, so it schal make lesse, and schal al to-breke alle these rewmes.
41 Kama vile ulivyoona, miguu na vidole vilikuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo na kwa sehemu vimefanywa kwa chuma, hivyo utakuwa ni ufalme uliogawanyika; baadhi ya nguvu za chuma zitakuwa ndani yake, kama tu ulivyoona kuwa chuma kimechanganyikana na udongo laini.
Forsothe that thou siest a part of the feet and fyngris of erthe of a pottere, and a part of irun, the rewme shal be departid; which netheles schal rise of the plauntyng of irun, `bi that that thou siest irun meynd with a tijl stoon of clei,
42 Kama vile vidole vya miguuni vilivyokuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa chuma na kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo, ndivyo ufalme utakuwa kwa sehemu una nguvu na kwa sehemu utakuwa dhaifu.
and the toos of the feet in parti of irun, and in parti of erthe, in parti the rewme schal be sad, and in parti to-brokun.
43 Kama ulivyoona chuma kimechanganywa na udongo laini, na hivyo na watu watakuwa wamechanganyikana; hawakaa kwa pamoja, kama vile chuma kisivyoweza kushikamana na udongo
Forsothe that thou siest irun meynd with a tiel stoon of clei, sotheli tho schulen be meynd togidere with mannus seed; but tho schulen not cleue to hem silf, as irun mai not be meddlid with tyel stoon.
44 Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaweza kuangushwa, wala kushindwa na watu wengine. Utazivunja falme zingine vipande vipande na kuzikomesha zote, nao utadumu milele.
Forsothe in the daies of tho rewmes, God of heuene shal reise a rewme, that schal not be distried with outen ende, and his rewme schal not be youun to another puple; it schal make lesse, and schal waste alle these rewmes, and it schal stonde with outen ende,
45 Kama tu ulivyoona, jiwe lilichongwa kutoka katika mlima, lakini si kwa mikono ya wanadamu. Lilivunja vunja chuma, shaba, udongo, fedha, na dhahabu katika vipande vipande. Mungu mkuu amekujulisha wewe, mfalme, kile kitakachotokea baada ya haya. Ndoto ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.
bi this that thou siest, that a stoon was kit doun of the hil with outen hondis, and maad lesse the tiel stoon, and irun, and bras, and siluer, and gold. Greet God hath schewid to the kyng, what thingis schulen come aftirward; and the dreem is trewe, and the interpretyng therof is feithful.
46 Mfalme Nebukadneza alianguka kifudifudi mbele ya Daniel na alimweshimu; aliamuru kwamba sadaka zitolewe na manukato yatolewe kwake.
Thanne king Nabugodonosor felle doun on his face, and worschipide Danyel, and comaundide sacrifices and encense to be brouyt, that tho schulden be sacrifised to hym.
47 Mfalme alimwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, Bwana wa wafalme, na ambaye hufunua mafumbo, kwa kuwa umekuwa ukiweza kufumbua mafumbo haya.”
Therfor the kyng spak, and seide to Danyel, Verili youre God is God of goddis, and Lord of kyngis, that schewith mysteries, for thou miytist opene this sacrament.
48 Ndipo mfalme alimfanya Danieli kuwa wa kuheshiwa sana na alimpa zawadi nyingi nzuri. Alimfanya kuwa mtawala juu ya jimbo lote la Babeli. Danieli akawa liwali mkuu juu watu wenye hekima wa Babeli.
Thanne the kyng reiside Danyel an hiy, and yaf many yiftis and grete to hym; and ordeynede hym prince and prefect, ether cheef iustise, ouer alle the prouynces of Babiloyne, and maister ouer alle the wise men of Babiloyne.
49 Danieli alipeleka ombi kwa mfalme, na mfalme aliwateua Shadraka, Meshaki na Abedinego kuwa watawala juu ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli alisalia katika ikulu ya mfalme.
Forsothe Danyel axide of the kyng, and ordeynede Sidrac, Misaac, and Abdenago ouer alle the werkis of the prouynce of Babiloyne; but Danyel hym silf was in the yatis of the kyng.

< Danieli 2 >