< Danieli 2 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Nebukadneza, alikuwa na ndoto. Akili yake ilisumbuka, na hakuweza kulala.
And in the second year of the reign of Nebuchadnezzar, Nebuchadnezzar dreamed dreams, whereat his spirit was troubled, and his sleep that was upon him was gone.
2 Ndipo mfalme alipowaita waganga na wale wenye kuongea na wafu. Lakini pia aliwaita wachawi na watu wenye hekima. Aliwataka wamwambie juu ya ndoto zake. Basi walikuja na kusimama mbele za mfalme.
Then said the king to call the magicians, and the astrologers and the sorcerers, and the Chaldeans, to solve for the king his dreams: and they came and placed themselves before the king.
3 Mfalme akawambia, “Nilikuwa na ndoto, na akili yangu ina mashaka nataka kujua ndoto hiyo nini maana yake.”
And the king said unto them, I have dreamed a dream, and my spirit is troubled to know the dream.
4 Kisha watu wenye hekima wakamwambia mfalme katika Kiaramaiki, “Mfalme, aishi milele! Twambie sisi ndoto, watumishi wako, nasi tutaifunua maana yake.”
Then spoke the Chaldeans to the king in Aramic, O king, live for ever: recite the dream to thy servants, and we will tell the interpretation.
5 Mfalme akawajibu watu wenye hekima, “Jambo hili limeshamalizika. Kama hamtaweza kuiweka wazi ndoto kwangu na kuitafsiri, miili yenu itakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vichuguu vya uchafu.
The king answered and said to the Chaldeans, The decree is firmly resolved on by me: If ye do not make known unto me the dream with its interpretation, ye shall be cut in pieces, and your houses shall be changed into a dunghill.
6 Lakini kama mtaniambia ndoto na maana yake, mtapokea zawadi kutoka kwangu, thawabu, na heshima kubwa. Basi niambie ndoto na maana yake.”
But if ye tell the dream and its interpretation, then shall ye receive gifts and rewards and great honor from me. Therefore tell me the dream and its interpretation.
7 Wakamjibu tena na kusema, “Mfalme na atuambie, watumishi wake, ndoto nasi tukwambia maana yake.”
They answered the second time and said, Let the king recite the dream to his servants, and we will tell its interpretation.
8 Mfalme akawajibu, “Ninajua kwa hakika mnahitaji muda zaidi kwasababu mmeona maamuzi yangu ni magumu kuhusu jambo hili.
The king answered and said, I know of a certainty that ye wish to gain time, because ye see the decree is firmly resolved on by me:
9 Lakini kama hamtaweza kuniambia ndoto, kuna sentensi moja tu kwa ajili yenu. Mmeamua kuandaa uongo na maneno ya kudanganya ambayo mmekubaliana kwa pamoja kuniambia mpaka pale nitakapobadili akili zangu. Basi, niambieni ndoto, na kisha nitajua kuwa mnaweza kuitafsiri kwa ajili yangu.”
That if ye do not make known unto me the dream, there is but one sentence for you; for ye have prepared lying and deceptive words to speak before me, till the time be changed. Therefore relate to me the dream, and I shall know that ye can tell me its interpretation.
10 Watu wenye hekima wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu katika dunia anayeweza kutimiza matakwa ya mfalme. Hakuna mfalme yoyote mkuu na mwenye nguvu ambaye alishataka jambo kama hilo kutoka kwa wachawi, wala wenye kuongea na wafu, wala mwenye hekima.
The Chaldeans answered before the king, and said, There is not a man upon the habitable earth that can tell the king's matter: wherefore no mighty and powerful king ever hath asked such a thing of any magician, or astrologer, or Chaldean.
11 Kile anachokitaka mfalme ni kigumu, na hakuna yeyote awezaye kumwambia mfalme isipokuwa miungu, ambayo haishi miongoni mwa watu.”
And the matter which the king requireth is difficult, and there is no other that can tell it before the king, except the gods, whose dwelling is not with flesh.
12 Jambo hili lilimfanya mfalme akasirike na kughadhabika sana, na alitoa amri kuwaangamiza wale wote waliojulikana kuwa ni wenye hekima zao katika Babeli.
For all this cause the king became angry, and very furious; and he commanded to destroy all the wise men of Babylon.
13 Hivyo, amri ilitoka kwamba wale wote waliojulikana kwa hekima yao ni lazima wauawe. Na kwa sababu ya amri hii, walimtafuta Daniel na rafiki zake ili kwamba wauawe.
And the law went forth and [some of] the wise men were slain: and they sought Daniel and his companions to slay them.
14 Ndipo Daniel alipomjibu kwa busara na umakini, Arioki, kamanda wa walinzi wa mfalme, ambaye alikuwa amekuja kuwaua wale wote waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
Then made Daniel representations with intelligence and prudence to Aryoch the captain of the king's guard, who was gone forth to slay the wise men of Babylon.
15 Danieli alimwuliza kamanda wa mfalme, “Kwanini amri ya mfalme ni ya haraka hivyo?” Hivyo, Arioki akamwambia Danieli kile kilichotokea.
He commenced and said to Aryoch the king's commander, Wherefore is the law so hasty from the king? Then made Aryoch the matter known to Daniel.
16 Ndipo Danieli aliingia ndani na akaomba ahadi ya muda wa kuonana na mfalme ili kwamba aweze kuwasilisha tafsiri kwa mfalme.
But Daniel went in, and requested of the king that he would give him time, that he might tell the interpretation to the king.
17 Kisha Danieli aliingia ndani ya nyumba na aliwaelezea Hanania, Mishaeli, na Azaria, kile kilichotokea.
Then went Daniel to his house, and made the matter known to Chananyah, Mishael, and 'Azaryah, his companions.
18 Aliwasihi kutafuta rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusiana na siri hii ili kwamba yeye na wao wasije wakauawa pamoja na watu wengine waliosalia waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
In order that they might pray for mercy of the God of heaven concerning this secret: so that Daniel and his companions might not be destroyed with the rest of the wise men of Babylon.
19 Usiku ule siri ilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Kisha Danieli akamtukuza Mungu wa mbinguni
Thereupon was the secret revealed unto Daniel in a vision of the night. Then did Daniel bless the God of heaven.
20 na kusema, “Litukuzwa jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na nguvu ni zake.
Daniel commenced and said, May the name of God be blessed from eternity and to all eternity; for wisdom and might are his;
21 Anabadili wakati na majira; anaondoa wafalme na kuweka wafalme katika viti vyao vya enzi. Anawapa hekima wenye hekima na ufahamu kwa wenye weledi.
And he changeth times and seasons; he removeth kings, and raiseth up kings: he giveth wisdom unto the wise, and knowledge to those that possess understanding.
22 Hufunua vitu vya chini na vilifichika kwa sababu anajua kile kilicho gizani, naye anaishi pamoja na mwanga.
He it is that revealeth what is deep and secret; he knoweth what is in the darkness, and the light dwelleth with him.
23 Mungu wa baba zetu, ninakushukuru na kukutukuza wewe kwa ajili ya hekima na nguvu uliyonipa. Sasa umeyafanya yawe wazi kwetu yale tuliyokuomba; umetujulisha mambo yamhusuyo mfalme.”
To thee, O God of my father, do I give thanks, and I praise thee, who hast given me wisdom and might, and because thou hast made known unto me what we prayed for of thee; for thou hast made known unto us the king's matter.
24 Ndipo Danieli alienda kumwona Arioki ( yule ambaye mfalme alimchagua kuua kila mtu aliyekuwa na hekima katika Babeli). Alimwendea na kumwambia, “Usiwauwe watu wenye hekima katika Babeli. Nipeleke kwa mfalme na nitamwonesha mfalme tafsiri ya ndoto yake.”
Therefore did Daniel go in unto Aryoch, whom the king had ordered to destroy the wise men of Babylon, He went and said thus unto him, the wise men of Babylon must thou not destroy: bring me before the king, and I will tell unto the king the interpretation.
25 Kisha Arioki kwa haraka alimleta Danieli mbele za mfalme na kusema, “Nimempata miongoni wa watu wa mateka wa Yuda mtu ambaye atafunua maana ya ndoto ya mfalme.”
Then did Aryoch bring Daniel before the king in haste, and thus he said unto him, Here have I found a man out of the children of the exiles of Judah, who will make known unto the king the interpretation.
26 Mfalme akamwambia Danieli (ambaye alikuwa akiitwa Beliteshaza), “Je unaweza kunimbia ndoto niliyoiona na maana yake?”
The king answered and said to Daniel, whose name was Belteshazzar, Art thou able to make known unto me the dream which I have seen, and its interpretation?
27 Danieli alimjibu mfalme na kusema, “Siri ambayo mfalme ameiomba haiwezi kufunuliwa na watu wenye hekima, wala wale wenye kuongea na wafu, wala wachawi, na wala wataalamu wa nyota.
Daniel answered in the presence of the king, and said, The secret which the king hath demanded no wise men, astrologers, magicians, or soothsayers, can tell unto the king;
28 Isipokuwa kuna Mungu ambaye anaishi mbinguni, ambaye hufunua siri, na amekwisha kukujulisha wewe, mfalme Nebukadneza, kile kitakachotokea katika siku zijazo. Hizi ndizo Ndoto na maono ya akili zako uliyoyaona wakati ulipokuwa umelala kitandani mwako.
But there is a God in heaven that revealeth secrets, and he hath made known to king Nebuchadnezzar what is to be in the latter days. Thy dream, and the visions of thy head upon thy couch, were these.
29 Na kwako Wewe, mfalme, mawazo yako kitandani mwako yalikuwa ni juu ya mambo yajayo, na yule afichuaye siri ameifanya ijulikane kwako kuhusu kile kilicho karibu kutokea.
As for thee, O king, thy thoughts, when thou wast on thy couch, rose [within thee] concerning what is to come to pass hereafter; and the Revealer of secrets hath made known to thee what is to come to pass.
30 Na kuhusu mimi, siri hii haikufunuliwa kwangu kwa sababu ya hekima yoyote niliyo nayo zaidi ya mtu yoyote anayeishi. Siri hii imefunliwa kwangu ili kwamba wewe, mfalme, uweze kufahamu maana, na ili kwamba ujuwe mawazo yaliyo ndani mwako.
But as for me, this secret hath not been revealed to me because of any wisdom that is in me more than in all other living; but for the sake that men might make known the interpretation to the king, and that thou mightest understand the thoughts of thy heart.
31 Mfalme, uliangalia juu na ukaona sanamu kubwa. Sanamu hii ambayo ilikuwa yenye nguvu na yenye kung'aa, ilisimama mbele yako. Mng'ao wake ulikuwa unatisha.
Thou, O king, sawest, and behold there was a large image; this image was mighty, and its brightness was excellent; it stood opposite to thee; and its form was fear-inspiring.
32 Kichwa cha sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi. Matiti yake na mikono ilikuwa ya fedha. Sehemu ya katikati na mapaja yake yalikuwa yametengenezwa kwa shaba,
As regardeth this image, its head was of fine gold, its breast and its arms were of silver, its belly and its thighs of copper,
33 na miguu yake ilikuwa imetengenezwa kwa chuma. Miguu yake ilikuwa ilitengenezwa kwa sehemu chuma na sehemu kwa udongo.
Its legs of iron, its feet part of them of iron and part of them of clay.
34 Ulitazama juu, na jiwe lilikuwa limechongwa, ingawa si kwa mikono ya wanadamu, na liliipiga sanamu katika miguu yake ya chuma na udongo, na ponda ponda.
Thou didst look on till the moment that a stone tore itself loose, not through [human] hands, and it struck the image upon its feet that were of iron and clay, and ground them to pieces.
35 Kisha chuma, udongo, fedha, na dhahabu zilivunjwa katika vipande vipande kwa wakati mmoja na yakawa kama makapi yaliyo katika sakafu za kupuria kipindi cha kiangazi. Upepo huyapeperushia mbali na hakuna alama inayoachwa. Lakini jiwe lililoipiga sanammu likawa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote.
Then were the iron, the clay, the copper, the silver, and the gold ground up together, and became like the chaff of the summer threshing-floors; and the wind carried them away, that no trace was found of them; and the stone that had stricken the image became a mighty mountain, and filled the whole earth.
36 Hii ndiyo ilikuwa ndotoyako. Na sasa tutamwambia mfalme maana yake.
This is the dream; and its interpretation will we relate before the king.
37 Wewe, mfalme, ni mfalme wa wafalme kwa wale ambao Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, nguvu, uweza na heshima.
Thou, O king, art a king of kings, to whom the God of heaven hath given kingdom, power, and strength, and honor:
38 Amevitia mkononi mwako sehemu ambazo binadamu huishi. Amekupa wanyama wa mwituni na ndege wa angani katika mkono wako, na amekufanya wewe utawale juu yao wote. Wewe u kichwa cha dhahabu cha sanamu.
And wheresoever the children of men dwell, hath he given the beasts of the field and the fowls of the heaven into thy hand, and hath made thee ruler over them all. Thou art the head of gold.
39 Baada yako, ufalme mwingine utainuka ambao ni mdogo kwako, na hata ufalme wa tatu wa shaba utatawala juu ya dunia yote.
And after thee there will arise another kingdom inferior to thee; and another third kingdom of copper, which will bear rule over all the earth.
40 Kutakuwa na ufalme wa tatu, wenye nguvu kama chuma, kwa kuwa chuma huvunja vipande vipande vitu vingine na kuponda ponda kila kitu. Itaviharibu vitu hivi vyote na kuvisaga.
And the fourth kingdom will be as strong as iron; forasmuch as iron grindeth up and beateth down all things, and as iron that breaketh [every thing], will it grind up and break all these.
41 Kama vile ulivyoona, miguu na vidole vilikuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo na kwa sehemu vimefanywa kwa chuma, hivyo utakuwa ni ufalme uliogawanyika; baadhi ya nguvu za chuma zitakuwa ndani yake, kama tu ulivyoona kuwa chuma kimechanganyikana na udongo laini.
And that thou sawest the feet and toes, and part of them of potter's clay, and part of them of iron, [signifieth] that it will be a divided kingdom, although there will be in it of the strength of the iron; forasmuch as thou sawest the iron mingled with miry clay.
42 Kama vile vidole vya miguuni vilivyokuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa chuma na kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo, ndivyo ufalme utakuwa kwa sehemu una nguvu na kwa sehemu utakuwa dhaifu.
And as the toes of the feet were part of them of iron, and part of them of clay: so will the kingdom be partly strong and partly brittle.
43 Kama ulivyoona chuma kimechanganywa na udongo laini, na hivyo na watu watakuwa wamechanganyikana; hawakaa kwa pamoja, kama vile chuma kisivyoweza kushikamana na udongo
And whereas thou sawest iron mingled with miry clay: so will they mingle themselves among the seed of men; but they will not cleave firmly one to another, even as iron cannot be mingled with clay.
44 Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaweza kuangushwa, wala kushindwa na watu wengine. Utazivunja falme zingine vipande vipande na kuzikomesha zote, nao utadumu milele.
But in the days of these kings will the God of heaven set up a kingdom: which shall to eternity not be destroyed, and its rule shall not be transferred to any other people; [but] it will grind up and make an end of all these kingdoms, while it will itself endure for ever.
45 Kama tu ulivyoona, jiwe lilichongwa kutoka katika mlima, lakini si kwa mikono ya wanadamu. Lilivunja vunja chuma, shaba, udongo, fedha, na dhahabu katika vipande vipande. Mungu mkuu amekujulisha wewe, mfalme, kile kitakachotokea baada ya haya. Ndoto ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.
Whereas thou sawest that out of the mountain a stone tore itself loose, not through [human] hands, and that it ground up the iron, the copper, the clay, the silver, and the gold: the great God hath made known to the king what is to come to pass after this. And the dream is reliable, and its interpretation certain.
46 Mfalme Nebukadneza alianguka kifudifudi mbele ya Daniel na alimweshimu; aliamuru kwamba sadaka zitolewe na manukato yatolewe kwake.
Then did king Nebuchadnezzar fall upon his face, and he bowed down to Daniel, and ordered that they should offer an oblation and sweet odors unto him.
47 Mfalme alimwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, Bwana wa wafalme, na ambaye hufunua mafumbo, kwa kuwa umekuwa ukiweza kufumbua mafumbo haya.”
The king answered unto Daniel, and said, Of a truth it is, that your God is the God of gods, and the Lord of kings, and the revealer of secrets; because thou hast been able to reveal this secret.
48 Ndipo mfalme alimfanya Danieli kuwa wa kuheshiwa sana na alimpa zawadi nyingi nzuri. Alimfanya kuwa mtawala juu ya jimbo lote la Babeli. Danieli akawa liwali mkuu juu watu wenye hekima wa Babeli.
Then did the king elevate Daniel, and gave him many great presents, and made him ruler over the whole province of Babylon, and chief of the superintendents over all the wise men of Babylon.
49 Danieli alipeleka ombi kwa mfalme, na mfalme aliwateua Shadraka, Meshaki na Abedinego kuwa watawala juu ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli alisalia katika ikulu ya mfalme.
Then requested Daniel of the king, that he might appoint Shadrach, Meshach, and 'Abed-nego, over the public service of the province of Babylon; but Daniel remained in the gate of the king.

< Danieli 2 >