< Danieli 2 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Nebukadneza, alikuwa na ndoto. Akili yake ilisumbuka, na hakuweza kulala.
I sit andet Regeringsaar drømte Nebukadnezar, og hans Sind blev uroligt, saa han ikke kunde sove.
2 Ndipo mfalme alipowaita waganga na wale wenye kuongea na wafu. Lakini pia aliwaita wachawi na watu wenye hekima. Aliwataka wamwambie juu ya ndoto zake. Basi walikuja na kusimama mbele za mfalme.
Saa lod Kongen Drømmetyderne, Manerne, Sandsigerne og Kaldæerne kalde, for at de skulde sige ham, hvad han havde drømt. Og de kom og traadte frem for Kongen.
3 Mfalme akawambia, “Nilikuwa na ndoto, na akili yangu ina mashaka nataka kujua ndoto hiyo nini maana yake.”
Da sagde Kongen til dem: »Jeg har haft en Drøm, og mit Sind falder ikke til Ro, før jeg faar at vide, hvad den betyder.«
4 Kisha watu wenye hekima wakamwambia mfalme katika Kiaramaiki, “Mfalme, aishi milele! Twambie sisi ndoto, watumishi wako, nasi tutaifunua maana yake.”
Kaldæerne svarede Kongen (paa Aramaisk): »Kongen leve evindelig! Sig dine Trælle Drømmen, saa skal vi tyde den.«
5 Mfalme akawajibu watu wenye hekima, “Jambo hili limeshamalizika. Kama hamtaweza kuiweka wazi ndoto kwangu na kuitafsiri, miili yenu itakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vichuguu vya uchafu.
Men Kongen svarede Kaldæerne: »Mit Ord staar fast! Hvis I ikke baade kundgør mig Drømmen og tyder den, skal I hugges sønder og sammen og eders Huse gøres til Skarndynger;
6 Lakini kama mtaniambia ndoto na maana yake, mtapokea zawadi kutoka kwangu, thawabu, na heshima kubwa. Basi niambie ndoto na maana yake.”
men gengiver I mig Drømmen og tyder den, faar I Skænk og Gave og stor Ære af mig. Gengiv mig, derfor Drømmen og tyd den!«
7 Wakamjibu tena na kusema, “Mfalme na atuambie, watumishi wake, ndoto nasi tukwambia maana yake.”
De svarede atter: »Kongen sige sine Trælle Drømmen, saa skal vi tyde den.«
8 Mfalme akawajibu, “Ninajua kwa hakika mnahitaji muda zaidi kwasababu mmeona maamuzi yangu ni magumu kuhusu jambo hili.
Kongen svarede: »Nu ved jeg for vist, at I kun søger at vinde Tid, fordi I ser, mit Ord staar fast,
9 Lakini kama hamtaweza kuniambia ndoto, kuna sentensi moja tu kwa ajili yenu. Mmeamua kuandaa uongo na maneno ya kudanganya ambayo mmekubaliana kwa pamoja kuniambia mpaka pale nitakapobadili akili zangu. Basi, niambieni ndoto, na kisha nitajua kuwa mnaweza kuitafsiri kwa ajili yangu.”
saa eders Dom kun kan blive een, hvis I ikke kundgør mig Drømmen, og at I derfor er blevet enige om at lyve for mig og føre mig bag Lyset, til der kommer andre Tider. Sig mig derfor Drømmen, saa jeg kan vide, at I ogsaa kan tyde mig den.«
10 Watu wenye hekima wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu katika dunia anayeweza kutimiza matakwa ya mfalme. Hakuna mfalme yoyote mkuu na mwenye nguvu ambaye alishataka jambo kama hilo kutoka kwa wachawi, wala wenye kuongea na wafu, wala mwenye hekima.
Kaldæerne svarede Kongen: »Der findes ikke et Menneske paa Jorden, som kan sige, hvad Kongen ønsker at vide; aldrig har jo heller nogen Konge, hvor stor og mægtig han end var, krævet sligt af nogen Drømmetyder, Maner eller Kaldæer;
11 Kile anachokitaka mfalme ni kigumu, na hakuna yeyote awezaye kumwambia mfalme isipokuwa miungu, ambayo haishi miongoni mwa watu.”
hvad Kongen kræver, er umuligt, og der er ingen, som kan sige Kongen det, undtagen Guderne, og de bor ikke hos de dødelige.«
12 Jambo hili lilimfanya mfalme akasirike na kughadhabika sana, na alitoa amri kuwaangamiza wale wote waliojulikana kuwa ni wenye hekima zao katika Babeli.
Herover blev Kongen vred og saare harmfuld, og han bød, at alle Babels Vismænd skulde henrettes.
13 Hivyo, amri ilitoka kwamba wale wote waliojulikana kwa hekima yao ni lazima wauawe. Na kwa sababu ya amri hii, walimtafuta Daniel na rafiki zake ili kwamba wauawe.
Da nu Befalingen var udgaaet, og man skulde til at slaa Vismændene ihjel, ledte man ogsaa efter Daniel og hans Venner for at slaa dem ihjel.
14 Ndipo Daniel alipomjibu kwa busara na umakini, Arioki, kamanda wa walinzi wa mfalme, ambaye alikuwa amekuja kuwaua wale wote waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
Da henvendte Daniel sig med kloge og vel overvejede Ord til Arjok, Øversten for Kongens Livvagt, som var draget ud for at slaa Babels Vismænd ihjel.
15 Danieli alimwuliza kamanda wa mfalme, “Kwanini amri ya mfalme ni ya haraka hivyo?” Hivyo, Arioki akamwambia Danieli kile kilichotokea.
Han tog til Orde og spurgte Arjok, Kongens Høvedsmand: »Hvorfor er saa skarp en Befaling udgaaet fra Kongen?« Og da Arjok havde sat ham ind i Sagen,
16 Ndipo Danieli aliingia ndani na akaomba ahadi ya muda wa kuonana na mfalme ili kwamba aweze kuwasilisha tafsiri kwa mfalme.
gik Daniel ind til Kongen og bad ham give sig en Frist, saa skulde han tyde Kongen Drømmen.
17 Kisha Danieli aliingia ndani ya nyumba na aliwaelezea Hanania, Mishaeli, na Azaria, kile kilichotokea.
Saa gik Daniel hjem og satte sine Venner Hananja, Misjael og Azarja ind i Sagen,
18 Aliwasihi kutafuta rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusiana na siri hii ili kwamba yeye na wao wasije wakauawa pamoja na watu wengine waliosalia waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
og han paalagde dem at bede Himmelens Gud om Barmhjertighed, saa han aabenbarede Hemmeligheden, for at ikke Daniel og hans Venner skulde blive henrettet med Babels andre Vismænd.
19 Usiku ule siri ilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Kisha Danieli akamtukuza Mungu wa mbinguni
Da blev Hemmeligheden aabenbaret Daniel i et Nattesyn; og Daniel priste Himmelens Gud,
20 na kusema, “Litukuzwa jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na nguvu ni zake.
tog til Orde og sagde: »Lovet være Guds Navn fra Evighed og til Evighed, thi ham tilhører Visdom og Styrke!
21 Anabadili wakati na majira; anaondoa wafalme na kuweka wafalme katika viti vyao vya enzi. Anawapa hekima wenye hekima na ufahamu kwa wenye weledi.
Han lader Tider og Stunder skifte, afsætter og indsætter Konger, giver de vise deres Visdom og de indsigtsfulde deres Viden;
22 Hufunua vitu vya chini na vilifichika kwa sababu anajua kile kilicho gizani, naye anaishi pamoja na mwanga.
han aabenbarer det dybe og lønlige; han ved, hvad Mørket gemmer, og Lyset bor hos ham.
23 Mungu wa baba zetu, ninakushukuru na kukutukuza wewe kwa ajili ya hekima na nguvu uliyonipa. Sasa umeyafanya yawe wazi kwetu yale tuliyokuomba; umetujulisha mambo yamhusuyo mfalme.”
Dig, mine Fædres Gud, takker og priser jeg, fordi du gav mig Visdom og Styrke, og nu har du kundgjort mig, hvad vi bad dig om; thi hvad Kongen vil vide, har du kundgjort os!«
24 Ndipo Danieli alienda kumwona Arioki ( yule ambaye mfalme alimchagua kuua kila mtu aliyekuwa na hekima katika Babeli). Alimwendea na kumwambia, “Usiwauwe watu wenye hekima katika Babeli. Nipeleke kwa mfalme na nitamwonesha mfalme tafsiri ya ndoto yake.”
Derfor gik Daniel til Arjok, hvem Kongen havde paalagt at henrette Babels Vismænd, og sagde til ham: »Henret ikke Babels Vismænd, men før mig frem for Kongen, saa vil jeg tyde ham Drømmen!«
25 Kisha Arioki kwa haraka alimleta Danieli mbele za mfalme na kusema, “Nimempata miongoni wa watu wa mateka wa Yuda mtu ambaye atafunua maana ya ndoto ya mfalme.”
Saa førte Arjok i Hast Daniel frem for Kongen og sagde til ham: »Jeg har blandt de bortførte Judæere fundet en Mand, som vil tyde Kongen Drømmen!«
26 Mfalme akamwambia Danieli (ambaye alikuwa akiitwa Beliteshaza), “Je unaweza kunimbia ndoto niliyoiona na maana yake?”
Kongen tog til Orde og spurgte Daniel, som havde faaet Navnet Beltsazzar: »Er du i Stand til at kundgøre mig den Drøm, jeg har haft, og tyde den?«
27 Danieli alimjibu mfalme na kusema, “Siri ambayo mfalme ameiomba haiwezi kufunuliwa na watu wenye hekima, wala wale wenye kuongea na wafu, wala wachawi, na wala wataalamu wa nyota.
Daniel svarede Kongen: »Den Hemmelighed, Kongen ønsker at vide, kan Vismænd, Manere, Drømmetydere og Stjernetydere ikke sige Kongen;
28 Isipokuwa kuna Mungu ambaye anaishi mbinguni, ambaye hufunua siri, na amekwisha kukujulisha wewe, mfalme Nebukadneza, kile kitakachotokea katika siku zijazo. Hizi ndizo Ndoto na maono ya akili zako uliyoyaona wakati ulipokuwa umelala kitandani mwako.
men der er en Gud i Himmelen, som aabenbarer Hemmeligheder, og han har kundgjort Kong Nebukadnezar, hvad der skal ske i de sidste Dage:
29 Na kwako Wewe, mfalme, mawazo yako kitandani mwako yalikuwa ni juu ya mambo yajayo, na yule afichuaye siri ameifanya ijulikane kwako kuhusu kile kilicho karibu kutokea.
Du tænkte, o Konge, paa dit Leje over, hvad der skal ske i Fremtiden, og han, som aabenbarer Hemmeligheder, kundgjorde dig, hvad der skal ske.
30 Na kuhusu mimi, siri hii haikufunuliwa kwangu kwa sababu ya hekima yoyote niliyo nayo zaidi ya mtu yoyote anayeishi. Siri hii imefunliwa kwangu ili kwamba wewe, mfalme, uweze kufahamu maana, na ili kwamba ujuwe mawazo yaliyo ndani mwako.
Og mig er denne Hemmelighed aabenbaret, ikke ved nogen Visdom, som jeg har forud for alle andre levende Væsener, men for at Drømmen kan blive tydet Kongen, saa du kan kende dit Hjertes Tanker.
31 Mfalme, uliangalia juu na ukaona sanamu kubwa. Sanamu hii ambayo ilikuwa yenye nguvu na yenye kung'aa, ilisimama mbele yako. Mng'ao wake ulikuwa unatisha.
Du saa, o Konge, for dig en vældig Billedstøtte; denne Billedstøtte var stor og dens Glans overmaade stærk; den stod foran dig, og dens Udseende var forfærdeligt.
32 Kichwa cha sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi. Matiti yake na mikono ilikuwa ya fedha. Sehemu ya katikati na mapaja yake yalikuwa yametengenezwa kwa shaba,
Billedstøttens Hoved var af fint Guld, Bryst og Arme af Sølv, Bug og Lænder af Kobber,
33 na miguu yake ilikuwa imetengenezwa kwa chuma. Miguu yake ilikuwa ilitengenezwa kwa sehemu chuma na sehemu kwa udongo.
Benene af Jern og Fødderne halvt af Jern og halvt af Ler.
34 Ulitazama juu, na jiwe lilikuwa limechongwa, ingawa si kwa mikono ya wanadamu, na liliipiga sanamu katika miguu yake ya chuma na udongo, na ponda ponda.
Saaledes skuede du, indtil en Sten reves løs, dog ikke ved Menneskehænder, og ramte Billedstøttens Jern— og Lerfødder og knuste dem;
35 Kisha chuma, udongo, fedha, na dhahabu zilivunjwa katika vipande vipande kwa wakati mmoja na yakawa kama makapi yaliyo katika sakafu za kupuria kipindi cha kiangazi. Upepo huyapeperushia mbali na hakuna alama inayoachwa. Lakini jiwe lililoipiga sanammu likawa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote.
og paa een Gang knustes Jern, Ler, Kobber, Sølv og Guld og blev som Avner fra Somrens Tærskepladser, og Vinden bar det sporløst bort; men Stenen, som ramte Billedstøtten, blev til et stort Bjerg, der fyldte hele Jorden.
36 Hii ndiyo ilikuwa ndotoyako. Na sasa tutamwambia mfalme maana yake.
Saaledes var Drømmen, og nu vil vi tyde Kongen den:
37 Wewe, mfalme, ni mfalme wa wafalme kwa wale ambao Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, nguvu, uweza na heshima.
Du, o Konge, Kongernes Konge, hvem Himmelens Gud gav Kongedømme, Magt, Styrke og Ære,
38 Amevitia mkononi mwako sehemu ambazo binadamu huishi. Amekupa wanyama wa mwituni na ndege wa angani katika mkono wako, na amekufanya wewe utawale juu yao wote. Wewe u kichwa cha dhahabu cha sanamu.
i hvis Haand han gav Menneskene, saa vide de bor, Markens Dyr og Himmelens Fugle, saa han gjorde dig til Hersker over dem alle, — du er Hovedet, som var af Guld.
39 Baada yako, ufalme mwingine utainuka ambao ni mdogo kwako, na hata ufalme wa tatu wa shaba utatawala juu ya dunia yote.
Men efter dig skal der komme et andet Rige, ringere end dit, og derpaa atter et tredje Rige, som er af Kobber, og hvis Herredømme skal strække sig over hele Jorden.
40 Kutakuwa na ufalme wa tatu, wenye nguvu kama chuma, kwa kuwa chuma huvunja vipande vipande vitu vingine na kuponda ponda kila kitu. Itaviharibu vitu hivi vyote na kuvisaga.
Siden skal der komme et fjerde Rige, stærkt som Jern; thi Jern knuser og søndrer alt; og som Jern sønderslaar, skal det knuse og sønderslaa alle hine Riger.
41 Kama vile ulivyoona, miguu na vidole vilikuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo na kwa sehemu vimefanywa kwa chuma, hivyo utakuwa ni ufalme uliogawanyika; baadhi ya nguvu za chuma zitakuwa ndani yake, kama tu ulivyoona kuwa chuma kimechanganyikana na udongo laini.
Men naar du saa Fødderne og Tæerne halvt af Pottemagerler og halvt af Jern, betyder det, at det skal være et Rige uden Sammenhold; dog skal det have noget af Jernets Fasthed, thi du saa jo, at Jern var blandet med Ler.
42 Kama vile vidole vya miguuni vilivyokuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa chuma na kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo, ndivyo ufalme utakuwa kwa sehemu una nguvu na kwa sehemu utakuwa dhaifu.
Og at Tæerne var halvt af Jern og halvt af Ler, betyder, at Riget delvis skal være stærkt, delvis svagt.
43 Kama ulivyoona chuma kimechanganywa na udongo laini, na hivyo na watu watakuwa wamechanganyikana; hawakaa kwa pamoja, kama vile chuma kisivyoweza kushikamana na udongo
Og naar du saa, at Jernet var blandet med Ler, betyder det, at de skal indgaa Ægteskaber med hverandre, men dog ikke indbyrdes holde sammen, saa lidt som Jern kan blandes med Ler.
44 Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaweza kuangushwa, wala kushindwa na watu wengine. Utazivunja falme zingine vipande vipande na kuzikomesha zote, nao utadumu milele.
Men i hine Kongers Dage vil Himmelens Gud oprette et Rige, som aldrig i Evighed skal forgaa, og Herredømmet skal ikke gaa over til noget andet Folk; det skal knuse og tilintetgøre alle hine Riger, men selv staa i al Evighed;
45 Kama tu ulivyoona, jiwe lilichongwa kutoka katika mlima, lakini si kwa mikono ya wanadamu. Lilivunja vunja chuma, shaba, udongo, fedha, na dhahabu katika vipande vipande. Mungu mkuu amekujulisha wewe, mfalme, kile kitakachotokea baada ya haya. Ndoto ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.
thi du saa jo, at en Sten reves løs fra Klippen, dog ikke ved Menneskehænder, og knuste Jern, Ler, Kobber, Sølv og Guld. En stor Gud har kundgjort Kongen, hvad der skal ske herefter; og Drømmen er sand og Tydningen troværdig.«
46 Mfalme Nebukadneza alianguka kifudifudi mbele ya Daniel na alimweshimu; aliamuru kwamba sadaka zitolewe na manukato yatolewe kwake.
Saa faldt Kong Nebukadnezar paa sit Ansigt og bøjede sig for Daniel, og han bød, at man skulde bringe ham Ofre og Røgelse.
47 Mfalme alimwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, Bwana wa wafalme, na ambaye hufunua mafumbo, kwa kuwa umekuwa ukiweza kufumbua mafumbo haya.”
Og Kongen tog til Orde og sagde til Daniel: »I Sandhed, eders Gud er Gudernes Gud og Kongernes Herre, og han kan aabenbare Hemmeligheder, siden du har kunnet aabenbare denne Hemmelighed.«
48 Ndipo mfalme alimfanya Danieli kuwa wa kuheshiwa sana na alimpa zawadi nyingi nzuri. Alimfanya kuwa mtawala juu ya jimbo lote la Babeli. Danieli akawa liwali mkuu juu watu wenye hekima wa Babeli.
Derpaa ophøjede Kongen Daniel og gav ham mange store Gaver, og han satte ham til Herre over hele Landsdelen Babel og til Overherre over alle Babels Vismænd.
49 Danieli alipeleka ombi kwa mfalme, na mfalme aliwateua Shadraka, Meshaki na Abedinego kuwa watawala juu ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli alisalia katika ikulu ya mfalme.
Men paa Daniels Bøn overdrog Kongen Sjadrak, Mesjak og Abed-Nego at styre Landsdelen Babel, medens Daniel selv blev i Kongens Gaard.

< Danieli 2 >