< Danieli 2 >
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Nebukadneza, alikuwa na ndoto. Akili yake ilisumbuka, na hakuweza kulala.
Druge godine Nabukodonozorova kraljevanja usni Nabukodonozor sanje: njegov se duh zbog toga uznemiri, a san ga ostavi.
2 Ndipo mfalme alipowaita waganga na wale wenye kuongea na wafu. Lakini pia aliwaita wachawi na watu wenye hekima. Aliwataka wamwambie juu ya ndoto zake. Basi walikuja na kusimama mbele za mfalme.
Kralj naredi da se pozovu čarobnici i gataoci, zaklinjači i zvjezdari da protumače kralju njegove sanje.
3 Mfalme akawambia, “Nilikuwa na ndoto, na akili yangu ina mashaka nataka kujua ndoto hiyo nini maana yake.”
Dođoše dakle te stadoše pred kralja. Kralj im reče: “Usnih jednu sanju i moj se duh uznemiri od želje da razumijem sanju.”
4 Kisha watu wenye hekima wakamwambia mfalme katika Kiaramaiki, “Mfalme, aishi milele! Twambie sisi ndoto, watumishi wako, nasi tutaifunua maana yake.”
Kaldejci odgovoriše kralju (aramejski): “O kralju, živ bio dovijeka! Pripovjedi svoju sanju slugama svojim, a mi ćemo ti otkriti njezino značenje.”
5 Mfalme akawajibu watu wenye hekima, “Jambo hili limeshamalizika. Kama hamtaweza kuiweka wazi ndoto kwangu na kuitafsiri, miili yenu itakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vichuguu vya uchafu.
Kralj odgovori i reče zvjezdarima: “Moja je odluka neopoziva: ako mi ne kažete što sam snio i što san znači, bit ćete rastrgani u komade, a vaše će kuće postati smetišta.
6 Lakini kama mtaniambia ndoto na maana yake, mtapokea zawadi kutoka kwangu, thawabu, na heshima kubwa. Basi niambie ndoto na maana yake.”
No ako mi otkrijete moju sanju i njezino značenje, dobit ćete od mene darove i poklone i velike časti. Otkrijte mi dakle što sam snio i što san znači.”
7 Wakamjibu tena na kusema, “Mfalme na atuambie, watumishi wake, ndoto nasi tukwambia maana yake.”
Oni opet odgovoriše: “Neka kralj rekne svoju sanju slugama svojim, a mi ćemo mu otkriti njezino značenje.”
8 Mfalme akawajibu, “Ninajua kwa hakika mnahitaji muda zaidi kwasababu mmeona maamuzi yangu ni magumu kuhusu jambo hili.
A kralj: “Dobro ja znam da želite dobiti na vremenu jer znate da je moja odluka neopoziva.
9 Lakini kama hamtaweza kuniambia ndoto, kuna sentensi moja tu kwa ajili yenu. Mmeamua kuandaa uongo na maneno ya kudanganya ambayo mmekubaliana kwa pamoja kuniambia mpaka pale nitakapobadili akili zangu. Basi, niambieni ndoto, na kisha nitajua kuwa mnaweza kuitafsiri kwa ajili yangu.”
Ako mi ne kažete što sam snio, znači da me namjeravate obmanjivati varavim riječima i izmišljotinama dok nekako ne prođe vrijeme. Stoga, recite mi moj san, pa ću znati da li mi možete kazati i njegovo značenje!”
10 Watu wenye hekima wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu katika dunia anayeweza kutimiza matakwa ya mfalme. Hakuna mfalme yoyote mkuu na mwenye nguvu ambaye alishataka jambo kama hilo kutoka kwa wachawi, wala wenye kuongea na wafu, wala mwenye hekima.
Zvjezdari odgovoriše pred kraljem: “Nema na svijetu čovjeka koji bi takvo što mogao otkriti kralju. I stoga nijedan kralj, ma kako velik i moćan, takvo što ne traži od čarobnika, gataoca ili zvjezdara.
11 Kile anachokitaka mfalme ni kigumu, na hakuna yeyote awezaye kumwambia mfalme isipokuwa miungu, ambayo haishi miongoni mwa watu.”
Što tražiš, kralju, teško je, i nema ga tko bi to mogao otkriti kralju osim bogova, koji ne borave među smrtnicima.”
12 Jambo hili lilimfanya mfalme akasirike na kughadhabika sana, na alitoa amri kuwaangamiza wale wote waliojulikana kuwa ni wenye hekima zao katika Babeli.
Tada se kralj silno razgnjevi i razbjesni te naredi da se pogube svi mudraci babilonski.
13 Hivyo, amri ilitoka kwamba wale wote waliojulikana kwa hekima yao ni lazima wauawe. Na kwa sababu ya amri hii, walimtafuta Daniel na rafiki zake ili kwamba wauawe.
Pošto je objavljena naredba da se ubiju mudraci, potražiše i Daniela i njegove drugove da ih pogube.
14 Ndipo Daniel alipomjibu kwa busara na umakini, Arioki, kamanda wa walinzi wa mfalme, ambaye alikuwa amekuja kuwaua wale wote waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
No Daniel se mudrim i umnim riječima obrati na Arjoka, zapovjednika kraljevskih straža, koji bijaše izišao da pogubi mudrace babilonske.
15 Danieli alimwuliza kamanda wa mfalme, “Kwanini amri ya mfalme ni ya haraka hivyo?” Hivyo, Arioki akamwambia Danieli kile kilichotokea.
On reče Arjoku, zapovjedniku kraljevu: “Zašto je kralj izdao tako strogu naredbu?” Arjok pripovjedi Danielu,
16 Ndipo Danieli aliingia ndani na akaomba ahadi ya muda wa kuonana na mfalme ili kwamba aweze kuwasilisha tafsiri kwa mfalme.
a Daniel otiđe kralju i zamoli da mu dade vremena te će kralju otkriti što san znači.
17 Kisha Danieli aliingia ndani ya nyumba na aliwaelezea Hanania, Mishaeli, na Azaria, kile kilichotokea.
Daniel uđe u svoju kuću te sve kaza Hananiji, Mišaelu i Azarji, svojim drugovima,
18 Aliwasihi kutafuta rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusiana na siri hii ili kwamba yeye na wao wasije wakauawa pamoja na watu wengine waliosalia waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
da mole milosrđe u Boga Nebeskoga radi te tajne, da Daniel i njegovi drugovi ne poginu s drugim mudracima babilonskim.
19 Usiku ule siri ilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Kisha Danieli akamtukuza Mungu wa mbinguni
I objavi se tajna Danielu u noćnom viđenju. A Daniel blagoslovi Boga Nebeskoga.
20 na kusema, “Litukuzwa jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na nguvu ni zake.
Daniel prihvati riječ i reče: “Bilo ime Božje blagoslovljeno odvijeka dovijeka, njegova je mudrost i sila.
21 Anabadili wakati na majira; anaondoa wafalme na kuweka wafalme katika viti vyao vya enzi. Anawapa hekima wenye hekima na ufahamu kwa wenye weledi.
On mijenja doba i vremena, ruši i postavlja kraljeve, daje mudrost mudrima a znanje pronicavima.
22 Hufunua vitu vya chini na vilifichika kwa sababu anajua kile kilicho gizani, naye anaishi pamoja na mwanga.
On otkriva dubine i tajne, zna što je u tminama i svjetlost prebiva u njega.
23 Mungu wa baba zetu, ninakushukuru na kukutukuza wewe kwa ajili ya hekima na nguvu uliyonipa. Sasa umeyafanya yawe wazi kwetu yale tuliyokuomba; umetujulisha mambo yamhusuyo mfalme.”
Tebe, o Bože otaca mojih, slavim i hvalim što si mi dao mudrost i jakost! Evo, objavio si mi ono što smo te molili, objavio si nam što kralj traži.”
24 Ndipo Danieli alienda kumwona Arioki ( yule ambaye mfalme alimchagua kuua kila mtu aliyekuwa na hekima katika Babeli). Alimwendea na kumwambia, “Usiwauwe watu wenye hekima katika Babeli. Nipeleke kwa mfalme na nitamwonesha mfalme tafsiri ya ndoto yake.”
Daniel ode k Arjoku, kome bijaše kralj naredio da smakne mudrace babilonske. Uđe i reče mu: “Ne ubijaj mudraca babilonskih! Odvedi me kralju, pa ću mu otkriti što san znači.”
25 Kisha Arioki kwa haraka alimleta Danieli mbele za mfalme na kusema, “Nimempata miongoni wa watu wa mateka wa Yuda mtu ambaye atafunua maana ya ndoto ya mfalme.”
Arjok žurno odvede Daniela kralju i reče: “Našao sam među izgnanicima judejskim čovjeka koji će kralju kazati što san znači.”
26 Mfalme akamwambia Danieli (ambaye alikuwa akiitwa Beliteshaza), “Je unaweza kunimbia ndoto niliyoiona na maana yake?”
Kralj reče Danielu (koji se zvaše Baltazar): “Jesi li kadar kazati mi san koji sam usnio i što znači?”
27 Danieli alimjibu mfalme na kusema, “Siri ambayo mfalme ameiomba haiwezi kufunuliwa na watu wenye hekima, wala wale wenye kuongea na wafu, wala wachawi, na wala wataalamu wa nyota.
Daniel odgovori pred kraljem: “Tajnu koju istražuje kralj ne mogahu kralju otkriti mudraci, čarobnici, gataoci i zaklinjači;
28 Isipokuwa kuna Mungu ambaye anaishi mbinguni, ambaye hufunua siri, na amekwisha kukujulisha wewe, mfalme Nebukadneza, kile kitakachotokea katika siku zijazo. Hizi ndizo Ndoto na maono ya akili zako uliyoyaona wakati ulipokuwa umelala kitandani mwako.
ali ima na nebu Bog koji objavljuje tajne i on je saopćio kralju Nabukodonozoru ono što će biti na svršetku dana. Evo tvoje sanje i onoga što ti se prividjelo na postelji:
29 Na kwako Wewe, mfalme, mawazo yako kitandani mwako yalikuwa ni juu ya mambo yajayo, na yule afichuaye siri ameifanya ijulikane kwako kuhusu kile kilicho karibu kutokea.
O kralju, na tvojoj ti postelji dođoše misli o tome što će se dogoditi kasnije, a Otkrivatelj tajna saopćio ti je ono što će biti.
30 Na kuhusu mimi, siri hii haikufunuliwa kwangu kwa sababu ya hekima yoyote niliyo nayo zaidi ya mtu yoyote anayeishi. Siri hii imefunliwa kwangu ili kwamba wewe, mfalme, uweze kufahamu maana, na ili kwamba ujuwe mawazo yaliyo ndani mwako.
Iako nemam mudrosti više nego ostali smrtnici, ta mi je tajna objavljena samo zato da njezino značenje saopćim kralju i da upoznaš misli svoga srca.
31 Mfalme, uliangalia juu na ukaona sanamu kubwa. Sanamu hii ambayo ilikuwa yenye nguvu na yenye kung'aa, ilisimama mbele yako. Mng'ao wake ulikuwa unatisha.
Ti si, o kralju, imao viđenje: gle, kip, golem kip, vrlo blistav, stajaše pred tobom, strašan za oči.
32 Kichwa cha sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi. Matiti yake na mikono ilikuwa ya fedha. Sehemu ya katikati na mapaja yake yalikuwa yametengenezwa kwa shaba,
Tome kipu glava bijaše od čistog zlata, prsa i ruke od srebra, trbuh i bedra od mjedi,
33 na miguu yake ilikuwa imetengenezwa kwa chuma. Miguu yake ilikuwa ilitengenezwa kwa sehemu chuma na sehemu kwa udongo.
gnjati od željeza, a stopala dijelom od željeza, dijelom od gline.
34 Ulitazama juu, na jiwe lilikuwa limechongwa, ingawa si kwa mikono ya wanadamu, na liliipiga sanamu katika miguu yake ya chuma na udongo, na ponda ponda.
Ti si promatrao: iznenada se odvali kamen a da ga ne dodirnu ruka, pa udari u kip, u stopala od željeza i gline te ih razbi.
35 Kisha chuma, udongo, fedha, na dhahabu zilivunjwa katika vipande vipande kwa wakati mmoja na yakawa kama makapi yaliyo katika sakafu za kupuria kipindi cha kiangazi. Upepo huyapeperushia mbali na hakuna alama inayoachwa. Lakini jiwe lililoipiga sanammu likawa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote.
Tada se smrvi najednom željezo i glina, mjed, srebro i zlato, i sve postade kao pljeva na gumnu ljeti i vjetar sve odnese bez traga. A kamen koji bijaše u kip udario postade veliko brdo te napuni svu zemlju.
36 Hii ndiyo ilikuwa ndotoyako. Na sasa tutamwambia mfalme maana yake.
To bijaše sanja; a njezino ćemo značenje reći pred kraljem.”
37 Wewe, mfalme, ni mfalme wa wafalme kwa wale ambao Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, nguvu, uweza na heshima.
“Ti, o kralju, kralju kraljeva, komu Bog Nebeski dade kraljevstvo, silu moć i slavu -
38 Amevitia mkononi mwako sehemu ambazo binadamu huishi. Amekupa wanyama wa mwituni na ndege wa angani katika mkono wako, na amekufanya wewe utawale juu yao wote. Wewe u kichwa cha dhahabu cha sanamu.
i u čije je ruke stavio, gdje god se našli, sinove ljudske, životinje poljske, ptice nebeske i postavio te gospodarom nad svim time - ti si glava od zlata.
39 Baada yako, ufalme mwingine utainuka ambao ni mdogo kwako, na hata ufalme wa tatu wa shaba utatawala juu ya dunia yote.
Poslije tebe ustat će drugo kraljevstvo, slabije od tvoga, pa treće, od mjedi, koje će gospodariti svom zemljom.
40 Kutakuwa na ufalme wa tatu, wenye nguvu kama chuma, kwa kuwa chuma huvunja vipande vipande vitu vingine na kuponda ponda kila kitu. Itaviharibu vitu hivi vyote na kuvisaga.
A četvrto kraljevstvo bit će tvrdo poput željeza, poput željeza koje sve satire i mrvi; kao željezo koje razbija, skršit će i razbit sva ona kraljevstva.
41 Kama vile ulivyoona, miguu na vidole vilikuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo na kwa sehemu vimefanywa kwa chuma, hivyo utakuwa ni ufalme uliogawanyika; baadhi ya nguvu za chuma zitakuwa ndani yake, kama tu ulivyoona kuwa chuma kimechanganyikana na udongo laini.
Stopala koja si vidio, dijelom glina a dijelom željezo, jesu podijeljeno kraljevstvo; imat će nešto od čvrstoće željeza prema onome što si vidio željezo izmiješano s glinom.
42 Kama vile vidole vya miguuni vilivyokuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa chuma na kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo, ndivyo ufalme utakuwa kwa sehemu una nguvu na kwa sehemu utakuwa dhaifu.
Prsti stopala, dijelom željezo a dijelom glina: kraljevstvo će biti dijelom čvrsto a dijelom krhko.
43 Kama ulivyoona chuma kimechanganywa na udongo laini, na hivyo na watu watakuwa wamechanganyikana; hawakaa kwa pamoja, kama vile chuma kisivyoweza kushikamana na udongo
A što si vidio željezo izmiješano s glinom: oni će se miješati ljudskim sjemenom, ali se neće držati zajedno, kao što se ni željezo ne da pomiješati s glinom.
44 Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaweza kuangushwa, wala kushindwa na watu wengine. Utazivunja falme zingine vipande vipande na kuzikomesha zote, nao utadumu milele.
U vrijeme ovih kraljeva Bog Nebeski podići će kraljevstvo koje neće nikada propasti i neće prijeći na neki drugi narod. Ono će razbiti i uništiti sva ona kraljevstva, a samo će stajati dovijeka -
45 Kama tu ulivyoona, jiwe lilichongwa kutoka katika mlima, lakini si kwa mikono ya wanadamu. Lilivunja vunja chuma, shaba, udongo, fedha, na dhahabu katika vipande vipande. Mungu mkuu amekujulisha wewe, mfalme, kile kitakachotokea baada ya haya. Ndoto ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.
kao što si vidio da se kamen s brijega odvalio a da ga ne dodirnu ruka te smrvio željezo, mjed, glinu, srebro i zlato. Veliki je Bog saopćio kralju što se ima dogoditi. Sanja je istinita, a tumačenje joj pouzdano.”
46 Mfalme Nebukadneza alianguka kifudifudi mbele ya Daniel na alimweshimu; aliamuru kwamba sadaka zitolewe na manukato yatolewe kwake.
Nato kralj Nabukodonozor pade ničice i pokloni se pred Danielom. Naredi da mu prinesu dar i kad.
47 Mfalme alimwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, Bwana wa wafalme, na ambaye hufunua mafumbo, kwa kuwa umekuwa ukiweza kufumbua mafumbo haya.”
I reče kralj Danielu: “Zaista, vaš je bog Bog nad bogovima i gospodar nad kraljevima, Otkrivatelj tajna, kad si mogao otkriti ovu tajnu.”
48 Ndipo mfalme alimfanya Danieli kuwa wa kuheshiwa sana na alimpa zawadi nyingi nzuri. Alimfanya kuwa mtawala juu ya jimbo lote la Babeli. Danieli akawa liwali mkuu juu watu wenye hekima wa Babeli.
Kralj uzvisi Daniela i dariva ga mnogim blistavim darovima. Postavi ga upraviteljem sve pokrajine babilonske i starješinom svih mudraca babilonskih.
49 Danieli alipeleka ombi kwa mfalme, na mfalme aliwateua Shadraka, Meshaki na Abedinego kuwa watawala juu ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli alisalia katika ikulu ya mfalme.
Daniel zamoli kralja da odredi za upravitelje pokrajine babilonske Šadraka, Mešaka i Abed Nega, a Daniel ostade na kraljevu dvoru.