< Danieli 12 >

1 Katika kipindi hicho, Mikaeli, jemedari mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwa na wakati wa mateso ambao haujawahi kutokea tangu mwanzo wa taifa lolote mpaka kipindi hicho. Katika muda huo watu wako wataokolewa, yeyote ambaye jina lake litapatikana katika kitabu.
[The angel also said to me, ] “After those things happen, the great angel Michael, who protects the [Israeli] people, will appear. Then there will be a time when there will be great troubles/suffering. The troubles will be greater than any troubles/suffering since the nations began. At that time, all of your people whose names have been written in the book [containing the names of those who have eternal life] will be saved.
2 Na wengi wa wale waliolala katika mavumbi ya dunia watainuka. baadhi kwa uzima wa milele na baadhi kwa ajili ya fedheha na matwezo ya milele.
Many of those who have died [EUP] will become alive again. Some of them will live eternally [with God], and some will be eternally shamed/disgraced [in hell]. (questioned)
3 Wale wenye hekima watang'ara kama mng'ao wa anga la juu, na wale wenye kuwaelekeza wengine katika haki, watakuwa kama nyota milele na milele.
Those who were wise will shine as brightly as the sky [is bright when the sun is shining]. And those who have shown to others the way to live righteously will shine forever, like the stars [SIM].
4 Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya; kihifadhi kitabu kikiwa kimetiwa chapa mpaka nyakati za mwisho. Watu wengi watakimbia huku na kule, na maarifa yataongezeka.
But as for you, Daniel, close up the scroll [on which you are writing], and seal it [in order that no one can open it] until the end [of the world] is near. [Before that happens, ] many people will travel rapidly here and there, learning more and more [about many things].”
5 Kisha mimi, Danieli, nilitazama, na kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama. Mmoja alisimama katika upande huu wa ukingo wa mto, na mwingine alisimama katika ukingo wa upande mwingine wa mto.
When [that angel finished speaking], I, Daniel, looked up, and suddenly I saw two other [angels]. One was standing on the side of the river [where I was], and one was standing on the other side.
6 Mmoja wao alimwambia mtu aliyevaa nguo za kitani, yeye aliyekuwa juu ya mkondo wa mto, “Je itachukua muda gani mpaka mwisho wa matukio haya ya kushangaza?”
One of them [called to] the other one, who was wearing linen/white clothes, who was now standing further up (OR, above) the river, “How long will it be until these amazing/frightening events end?”
7 Nilimsikia mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu katika mkondo wa mto, aliinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni na kuapa kwa yeye aishiye milele kwamba itakuwa kwa wakati, nyakati, na nusu wakati. Na wakati nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimeshaharibiwa, mambo haya yote yatakuwa yamemalizika.
The angel who was on the other side of (OR, above) the river raised his hands toward the sky, and solemnly promised, with the authority [MTY] of God, who lives forever, “It will be three and a half years. All these things will end after God’s people stop fighting against those who (persecute/cause trouble for/cause suffering for) them.”
8 Nilisikia, lakini sikufahamu. Basi nikamwuliza, “Bwana wangu, mambo haya yote yatakuwa na matokeo gani?”
I heard [what he said], but I did not understand it. So I asked, “Sir, what will be the result when these things end?”
9 Alisema, “Nenda zako Danieli, kwa kuwa maneno yamefungwa na kutiwa chapa mpaka wakati wa mwisho.
He replied, “Daniel, you must leave now. [I cannot answer your question] because what it means must (be kept secret/not be revealed) [DOU] until the time when everything ends.
10 Watu wengi watakuwa wametakaswa, wameoshwa, na kusafishwa, lakini waovu wataenenda katika uovu.
Many people will thoroughly purify their inner beings [DOU]. But wicked people will not understand these things. They will continue to be wicked. Only those who are wise will understand [these things].
11 Katika muda ule ambapo sadaka ya kawaida ya kuteketezwa itakapokuwa imeondolewa na chukizo la uharibifu liliosababisha ukiwa limesimamishwa, kutakuwa na siku zipatazo 1, 290.
[But I can tell you that before everything ends, ] there will be 1,290 days, from the time that people are prevented from offering sacrifices each day, that is, from the time that the abominable/disgusting thing is put in the temple.
12 Ana heri mtu yule anayengojea mpaka mwisho wa siku 1, 335.
God will be pleased with those who remain faithful until 1,335 days are ended.
13 Unapaswa uondoke uende njia yako hata mwisho, na kisha utapumzika. Utainuka katika sehemu uliyopewa, mwishoni mwa siku.”
So [now I say] to you, continue to faithfully [trust God] until [your life on earth] ends. You will die [EUP], but when everything ends, you will receive your reward [from God].”

< Danieli 12 >