< Danieli 12 >

1 Katika kipindi hicho, Mikaeli, jemedari mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwa na wakati wa mateso ambao haujawahi kutokea tangu mwanzo wa taifa lolote mpaka kipindi hicho. Katika muda huo watu wako wataokolewa, yeyote ambaye jina lake litapatikana katika kitabu.
and in/on/with time [the] he/she/it to stand: rise Michael [the] ruler [the] great: large [the] to stand: appoint upon son: descendant/people people your and to be time distress which not to be from to be nation till [the] time [the] he/she/it and in/on/with time [the] he/she/it to escape people your all [the] to find to write in/on/with scroll: book
2 Na wengi wa wale waliolala katika mavumbi ya dunia watainuka. baadhi kwa uzima wa milele na baadhi kwa ajili ya fedheha na matwezo ya milele.
and many from sleeping land: soil dust to awake these to/for life forever: enduring and these to/for reproach to/for abhorrence forever: enduring
3 Wale wenye hekima watang'ara kama mng'ao wa anga la juu, na wale wenye kuwaelekeza wengine katika haki, watakuwa kama nyota milele na milele.
and [the] be prudent to shine like/as brightness [the] expanse and to justify [the] many like/as star to/for forever: enduring and perpetuity
4 Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya; kihifadhi kitabu kikiwa kimetiwa chapa mpaka nyakati za mwisho. Watu wengi watakimbia huku na kule, na maarifa yataongezeka.
and you(m. s.) Daniel to close [the] word and to seal [the] scroll: book till time end to rove many and to multiply [the] knowledge
5 Kisha mimi, Danieli, nilitazama, na kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama. Mmoja alisimama katika upande huu wa ukingo wa mto, na mwingine alisimama katika ukingo wa upande mwingine wa mto.
and to see: see I Daniel and behold two another to stand: stand one here/thus to/for lip: shore [the] stream and one here/thus to/for lip: shore [the] stream
6 Mmoja wao alimwambia mtu aliyevaa nguo za kitani, yeye aliyekuwa juu ya mkondo wa mto, “Je itachukua muda gani mpaka mwisho wa matukio haya ya kushangaza?”
and to say to/for man to clothe [the] linen which from above to/for water [the] stream till how end [the] wonder
7 Nilimsikia mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu katika mkondo wa mto, aliinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni na kuapa kwa yeye aishiye milele kwamba itakuwa kwa wakati, nyakati, na nusu wakati. Na wakati nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimeshaharibiwa, mambo haya yote yatakuwa yamemalizika.
and to hear: hear [obj] [the] man to clothe [the] linen which from above to/for water [the] stream and to exalt right his and left his to(wards) [the] heaven and to swear in/on/with alive [the] forever: enduring for to/for meeting: time appointed meeting: time appointed and half and like/as to end: finish to shatter hand: power people holiness to end: finish all these
8 Nilisikia, lakini sikufahamu. Basi nikamwuliza, “Bwana wangu, mambo haya yote yatakuwa na matokeo gani?”
and I to hear: hear and not to understand and to say [emph?] lord my what? end these
9 Alisema, “Nenda zako Danieli, kwa kuwa maneno yamefungwa na kutiwa chapa mpaka wakati wa mwisho.
and to say to go: journey Daniel for to close and to seal [the] word till time end
10 Watu wengi watakuwa wametakaswa, wameoshwa, na kusafishwa, lakini waovu wataenenda katika uovu.
to purify and to whiten and to refine many and be wicked wicked and not to understand all wicked and [the] be prudent to understand
11 Katika muda ule ambapo sadaka ya kawaida ya kuteketezwa itakapokuwa imeondolewa na chukizo la uharibifu liliosababisha ukiwa limesimamishwa, kutakuwa na siku zipatazo 1, 290.
and from time to turn aside: remove [the] continually and to/for to give: put abomination be desolate: destroyed day thousand hundred and ninety
12 Ana heri mtu yule anayengojea mpaka mwisho wa siku 1, 335.
blessed [the] to wait and to touch to/for day thousand three hundred thirty and five
13 Unapaswa uondoke uende njia yako hata mwisho, na kisha utapumzika. Utainuka katika sehemu uliyopewa, mwishoni mwa siku.”
and you(m. s.) to go: journey to/for end and to rest and to stand: stand to/for allotted your to/for end [the] day

< Danieli 12 >