< Danieli 12 >

1 Katika kipindi hicho, Mikaeli, jemedari mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwa na wakati wa mateso ambao haujawahi kutokea tangu mwanzo wa taifa lolote mpaka kipindi hicho. Katika muda huo watu wako wataokolewa, yeyote ambaye jina lake litapatikana katika kitabu.
And at that time shall Michael arise, the great prince that standeth up for the sons of thy people; and there shall be a time of trouble, such as never was since there was a nation even to that time; and at that time shall thy people be delivered, every one that is found written in the book.
2 Na wengi wa wale waliolala katika mavumbi ya dunia watainuka. baadhi kwa uzima wa milele na baadhi kwa ajili ya fedheha na matwezo ya milele.
And many of them that sleep in the dust of the earth shall awake, some to everlasting life, and some to shame, to everlasting contempt.
3 Wale wenye hekima watang'ara kama mng'ao wa anga la juu, na wale wenye kuwaelekeza wengine katika haki, watakuwa kama nyota milele na milele.
And they that are wise shall shine as the brightness of the firmament; and they that turn the many to righteousness, as the stars for ever and ever.
4 Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya; kihifadhi kitabu kikiwa kimetiwa chapa mpaka nyakati za mwisho. Watu wengi watakimbia huku na kule, na maarifa yataongezeka.
But thou, Daniel, shut up these words, and seal this book even to the time of the end. Many shall run eagerly through it, and much knowledge shall be gained.
5 Kisha mimi, Danieli, nilitazama, na kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama. Mmoja alisimama katika upande huu wa ukingo wa mto, na mwingine alisimama katika ukingo wa upande mwingine wa mto.
And I Daniel looked, and behold, two others stood there, one on this side of the bank of the river, and the other on that side of the bank of the river.
6 Mmoja wao alimwambia mtu aliyevaa nguo za kitani, yeye aliyekuwa juu ya mkondo wa mto, “Je itachukua muda gani mpaka mwisho wa matukio haya ya kushangaza?”
And one of them said to the man clothed in linen, who was upon the waters of the river, How long shall it be to the end of these wonders?
7 Nilimsikia mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu katika mkondo wa mto, aliinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni na kuapa kwa yeye aishiye milele kwamba itakuwa kwa wakati, nyakati, na nusu wakati. Na wakati nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimeshaharibiwa, mambo haya yote yatakuwa yamemalizika.
And I heard the man clothed in linen, who was upon the waters of the river, and he lifted up his right hand and his left hand to heaven, and swore by Him that liveth forever, that in a time, times, and a half, even when the dispersion of a portion of the holy people should be at an end, all these things should be fulfilled.
8 Nilisikia, lakini sikufahamu. Basi nikamwuliza, “Bwana wangu, mambo haya yote yatakuwa na matokeo gani?”
And I heard but understood not; and I said, My lord, what is the latter end of these things?
9 Alisema, “Nenda zako Danieli, kwa kuwa maneno yamefungwa na kutiwa chapa mpaka wakati wa mwisho.
And he said, Go thy way, Daniel, for the words are closed up and sealed till the time of the end.
10 Watu wengi watakuwa wametakaswa, wameoshwa, na kusafishwa, lakini waovu wataenenda katika uovu.
Many shall be cleansed, and made white, and purified, and the wicked will do wickedly; and none of the wicked will understand, but the wise will understand.
11 Katika muda ule ambapo sadaka ya kawaida ya kuteketezwa itakapokuwa imeondolewa na chukizo la uharibifu liliosababisha ukiwa limesimamishwa, kutakuwa na siku zipatazo 1, 290.
And from the time when the daily sacrifice shall be taken away, and the abomination of the destroyer set up, there shall be a thousand two hundred and ninety days.
12 Ana heri mtu yule anayengojea mpaka mwisho wa siku 1, 335.
Happy is he that waiteth and cometh to a thousand three hundred and thirty-five days!
13 Unapaswa uondoke uende njia yako hata mwisho, na kisha utapumzika. Utainuka katika sehemu uliyopewa, mwishoni mwa siku.”
But go thou thy way even to the end; for thou shalt rest, and rise up to thy lot at the end of the days.

< Danieli 12 >