< Danieli 12 >

1 Katika kipindi hicho, Mikaeli, jemedari mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwa na wakati wa mateso ambao haujawahi kutokea tangu mwanzo wa taifa lolote mpaka kipindi hicho. Katika muda huo watu wako wataokolewa, yeyote ambaye jina lake litapatikana katika kitabu.
At that time Michael the great prince, the protector of your people, will stand up and there will be a time of trouble like never before, since nations first existed. But at that time your people will be saved, all whose names are written in the book.
2 Na wengi wa wale waliolala katika mavumbi ya dunia watainuka. baadhi kwa uzima wa milele na baadhi kwa ajili ya fedheha na matwezo ya milele.
Millions sleeping in the ground in death will awake, some to eternal life, and some to eternal shame and disgrace.
3 Wale wenye hekima watang'ara kama mng'ao wa anga la juu, na wale wenye kuwaelekeza wengine katika haki, watakuwa kama nyota milele na milele.
Those who are wise will shine as bright as the sky; those who have shown many the right way to live will shine as bright as the stars forever and ever.
4 Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya; kihifadhi kitabu kikiwa kimetiwa chapa mpaka nyakati za mwisho. Watu wengi watakimbia huku na kule, na maarifa yataongezeka.
But as for you, Daniel, keep this message secret, and seal the book closed until the time of the end. Many will search this way and that way, and knowledge will grow greater and greater.”
5 Kisha mimi, Danieli, nilitazama, na kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama. Mmoja alisimama katika upande huu wa ukingo wa mto, na mwingine alisimama katika ukingo wa upande mwingine wa mto.
Then I, Daniel, noticed two others, each standing on opposite sides of the river.
6 Mmoja wao alimwambia mtu aliyevaa nguo za kitani, yeye aliyekuwa juu ya mkondo wa mto, “Je itachukua muda gani mpaka mwisho wa matukio haya ya kushangaza?”
One of then asked the man dressed in linen who was above the river's waters, “How long before these outrageous things come to an end?”
7 Nilimsikia mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu katika mkondo wa mto, aliinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni na kuapa kwa yeye aishiye milele kwamba itakuwa kwa wakati, nyakati, na nusu wakati. Na wakati nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimeshaharibiwa, mambo haya yote yatakuwa yamemalizika.
The man dressed in linen, who was above the river's waters, lifted both hands to heaven made a solemn promise by the One who lives eternally. I heard him say, “It will last for a time, times, and half a time. When the scattering of the power of the holy people has come to an end, then all these things will also come to an end.”
8 Nilisikia, lakini sikufahamu. Basi nikamwuliza, “Bwana wangu, mambo haya yote yatakuwa na matokeo gani?”
I heard the answer, but I didn't understand it. So I asked, “My lord, what's the final result of all this?”
9 Alisema, “Nenda zako Danieli, kwa kuwa maneno yamefungwa na kutiwa chapa mpaka wakati wa mwisho.
“Daniel, you can go on your way now,” he replied, “for this message is secret and kept sealed until the time of the end.
10 Watu wengi watakuwa wametakaswa, wameoshwa, na kusafishwa, lakini waovu wataenenda katika uovu.
Many will be purified and cleansed and refined, but the wicked will go on being wicked. None of the wicked will understand, but the wise will understand.
11 Katika muda ule ambapo sadaka ya kawaida ya kuteketezwa itakapokuwa imeondolewa na chukizo la uharibifu liliosababisha ukiwa limesimamishwa, kutakuwa na siku zipatazo 1, 290.
From the time the continual ministry is stopped in order to set up the idolatry that causes devastation will be one thousand two hundred and ninety days.
12 Ana heri mtu yule anayengojea mpaka mwisho wa siku 1, 335.
Blessed are those who patiently wait for and reach the one thousand three hundred and thirty-five days.
13 Unapaswa uondoke uende njia yako hata mwisho, na kisha utapumzika. Utainuka katika sehemu uliyopewa, mwishoni mwa siku.”
But as for you, go your way until your life ends, and then rest. You will rise to receive your reward at the end of time.”

< Danieli 12 >