< Danieli 12 >

1 Katika kipindi hicho, Mikaeli, jemedari mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwa na wakati wa mateso ambao haujawahi kutokea tangu mwanzo wa taifa lolote mpaka kipindi hicho. Katika muda huo watu wako wataokolewa, yeyote ambaye jina lake litapatikana katika kitabu.
“But at that time Michael will rise up, the great leader, who stands up for the sons of your people. And a time will come, such as has not been from the time that nations began, even until that time. And, at that time, your people will be saved, all who will be found written in the book.
2 Na wengi wa wale waliolala katika mavumbi ya dunia watainuka. baadhi kwa uzima wa milele na baadhi kwa ajili ya fedheha na matwezo ya milele.
And many of those who sleep in the dust of the earth will awaken: some to everlasting life, and others to a reproach that they will always see.
3 Wale wenye hekima watang'ara kama mng'ao wa anga la juu, na wale wenye kuwaelekeza wengine katika haki, watakuwa kama nyota milele na milele.
But those who have taught will shine like the brightness of the firmament, and those who instruct many towards justice, like the stars for unending eternity.
4 Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya; kihifadhi kitabu kikiwa kimetiwa chapa mpaka nyakati za mwisho. Watu wengi watakimbia huku na kule, na maarifa yataongezeka.
But you, Daniel, close the message and seal the book, until the established time. Many will pass through, and knowledge will be increased.”
5 Kisha mimi, Danieli, nilitazama, na kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama. Mmoja alisimama katika upande huu wa ukingo wa mto, na mwingine alisimama katika ukingo wa upande mwingine wa mto.
And I, Daniel, looked, and behold, similarly two others stood up, one over here, on the bank of the river, and the other over there, on the other bank of the river.
6 Mmoja wao alimwambia mtu aliyevaa nguo za kitani, yeye aliyekuwa juu ya mkondo wa mto, “Je itachukua muda gani mpaka mwisho wa matukio haya ya kushangaza?”
And I said to the man, who was clothed in linen, who stood over the waters of the river, “How long will it be until the end of these wonders?”
7 Nilimsikia mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu katika mkondo wa mto, aliinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni na kuapa kwa yeye aishiye milele kwamba itakuwa kwa wakati, nyakati, na nusu wakati. Na wakati nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimeshaharibiwa, mambo haya yote yatakuwa yamemalizika.
And I heard the man, who was clothed in linen, who stood over the waters of the river, when he had lifted his right hand and his left hand up to heaven, and had sworn by He who lives forever, that it would be for a time, and times, and half a time. And when the dispersion of the hand of the holy people is completed, all these things will be completed.
8 Nilisikia, lakini sikufahamu. Basi nikamwuliza, “Bwana wangu, mambo haya yote yatakuwa na matokeo gani?”
And I heard and did not understand. And I said, “My lord, what will be after these things?”
9 Alisema, “Nenda zako Danieli, kwa kuwa maneno yamefungwa na kutiwa chapa mpaka wakati wa mwisho.
And he said, “Go, Daniel, for the words are closed and sealed until the predetermined time.
10 Watu wengi watakuwa wametakaswa, wameoshwa, na kusafishwa, lakini waovu wataenenda katika uovu.
Many will be chosen and purified, and, as if by fire, they will be tested, and the impious will act impiously, and none of the impious will understand, yet the teachers will understand.
11 Katika muda ule ambapo sadaka ya kawaida ya kuteketezwa itakapokuwa imeondolewa na chukizo la uharibifu liliosababisha ukiwa limesimamishwa, kutakuwa na siku zipatazo 1, 290.
And from the time when the continual sacrifice will be taken away and the abomination of desolation will be set up, there will be one thousand two hundred ninety days.
12 Ana heri mtu yule anayengojea mpaka mwisho wa siku 1, 335.
Blessed is he who waits and reaches until one thousand three hundred thirty-five days.
13 Unapaswa uondoke uende njia yako hata mwisho, na kisha utapumzika. Utainuka katika sehemu uliyopewa, mwishoni mwa siku.”
But you, go, until the predetermined time, and you will rest and will stand in your allotted place at the end of days.

< Danieli 12 >