< Danieli 11 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa Dario Mmedi, mimi mwenyewe nilikuja kumwezesha na kumlinda Mikaeli.
Tudi jaz sem v prvem letu Medijca Dareja, celó jaz, stal, da ga potrdim in okrepim.
2 Na sasa nitakufunulia ukweli. Wafalme watatu watainuka katika Uajemi, na mfalme wa nne atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Na wakati atakapopata nguvu kupitia utajiri wake, atamwamsha kila mtu kinyume na ufalme wa Ugiriki.
Sedaj ti bom pokazal resnico: »Glej, v Perziji bodo vstali še trije kralji, četrti pa bo mnogo bogatejši kakor oni vsi. S svojo močjo bo po svojih bogastvih vse razvnel zoper področje Grčije.
3 Mfalme wenye nguvu atainuka ambaye atatawala ufalme mkubwa, na ataenenda kufuatana na matakwa yake mwenyewe.
Vstal bo mogočen kralj, ki bo vladal z velikim gospostvom in počel glede na svojo voljo.
4 Na atakapokuwa ameinuka, ufalme wake utavunjika na utagawanyika katika pepo nne za mbinguni, lakini hawatakuwa wazao wake mwenyewe, na si kwa nguvu zake kwa wakati alipokuwa akitawala. Kwa kuwa ufalme wake utang'olewa kwa ajili ya wengine tofauti na wazawa wake.
Ko bo vstal, bo njegovo kraljestvo zlomljeno in razdeljeno bo proti štirim vetrovom neba, in ne k njegovemu potomstvu niti glede na njegovo gospostvo, ki mu je vladal, kajti njegovo kraljestvo bo izpuljeno, celo za druge poleg teh.
5 Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja kati ya maamiri jeshi wake atakuwa mwenye nguvu kuliko yeye na atautawala ufalme wake kwa nguvu kubwa.
Južni kralj bo močan in eden izmed njegovih princev in on bo močan nad njim in imel bo gospostvo; njegovo gospostvo bo veliko gospostvo.
6 Baada ya miaka michache, wakati muda utakapokuwa sawa, watafanya mwungano. Binti wa mfalme wa Kusini atakuja kwa mfalme wa Kaskazini kuyathibitisha makubaliano yao. Lakini hataweza kuzitunza nguvu za mkono wake, wala mfalme hatasimama wala mkono wake. Ataachwa na wale waliomleta, na baba yake, na yeye aliyemwunga mkono katika nyakati hizo.
Ob koncu let se bosta združila skupaj, kajti kraljeva hči iz juga bo prišla k severnemu kralju, da sklene dogovor. Toda ona ne bo obdržala moči lakta niti on ne bo obstal niti njegov laket, temveč bo izdana in tisti, ki so jo privedli in tisti, ki jo je zaplodil in kdor jo je okrepil v teh časih.
7 Lakini tawi kutoka katika mizizi yake litachipuka katika nafasi yake. Atalishambulia jeshi na kuingia ngome ya mfalme wa Kaskazini. Atapigana nao, na atawashinda.
Toda iz mladike njenih korenin bo vstal nekdo v svoji lastnini, ki bo prišel z vojsko in vstopil v trdnjavo severnega kralja in se bo spoprijel zoper njih in bo prevladal.
8 Ataichukua miungu yao mpaka Misri pamoa na sanamu zao za chuma na vyombo vyao vya fedha na vya dhahabu vyenye thamani. Kwa miaka mingi atakaa mbali na mfalme wa Kaskazini.
Prav tako bo ujete odvedel v Egipt njihove bogove z njihovimi princi in z njihovimi dragocenimi posodami iz srebra in zlata, in nadaljeval bo več let kakor kralj iz severa.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atauvamia ufalme wa mfalme wa Kusini, lakini atajitoa na kwenda katika nchi yake mwenyewe.
Tako bo južni kralj prišel v svoje kraljestvo in se bo vrnil v svojo lastno deželo.
10 Wana wake watajiweka tayari na kuunganisha jeshi kubwa. Litaendelea kukua na litagharikisha kila kitu, litapita katikati hadi kwenye ngome yake.
Toda njegova sinova bosta razvneta in bosta zbrala množico velikih sil, in nekdo bo zagotovo prišel, preplavil in šel skozi. Potem se bo vrnil in bo razvnet, celó do svoje trdnjave.
11 Ndipo mfalme wa Kusini atakasirika, na ataenda na kupigana naye, mfalme wa Kaskazini. Mfalme wa Kaskazini atainua jeshi kubwa, bali jeshi litatiwa katika mkono wake.
Južni kralj bo prevzet z gnevom in prišel bo in se boril z njim, celó s severnim kraljem, in postavil bo veliko množico, toda množica bo dana v njegovo roko.
12 Jeshi litachukuliwa, na moyo wa mfalme wa Kusini utainuliwa juu, na atawafanya makumi maelfu kuanguka, lakini hataweza kuwa mshindi.
In ko bo odvedel množico, bo njegovo srce povzdignjeno in podrl bo mnogo deset tisočev, toda s tem ne bo okrepljen.
13 Kisha mfalme wa Kaskazini atainua jeshi jingine, kubwa kuliko la kwanza. Baada ya miaka kadhaa, mfalme wa Kaskazini atakuja na jeshi kubwa likiwa na vifaa vingi.
Kajti severni kralj se bo vrnil in vzpostavil množico, večjo kakor prejšnja in zagotovo bo prišel čez določena leta z veliko vojsko in z mnogimi bogastvi.
14 Katika siku hizo wengi watainuka kinyume na mfalmea wa Kusini. Wana wa vurugu miongoni mwa watu wake watasimama wao wenyewe ili kuyatimiliza maono, lakini watajikwaa.
V tistih časih bodo mnogi vstali zoper južnega kralja. Tudi roparji tvojega ljudstva se bodo povišali, da vzpostavijo videnje; vendar bodo padli.
15 Mfalme wa Kaskazini atakuja, kuizingira nchi kwa kuweka vilima, na kuuteka mji wenye ngome. Majeshi ya Kusini hayataweza kusimama, hata wanajeshi wake bora. Hawatakuwa na nguvu za kusimama.
Tako bo prišel severni kralj in nasul nasip in zavzel najbolj utrjena mesta, in orožje iz juga se ne bo zoperstavilo niti njegovo izvoljeno ljudstvo niti ne bo nobene moči, da se zoperstavi.
16 Badala yake, yeye ajaye ataenenda kwa kufuata tamaa zake kinyume chake; hakuna yeyote atakayesimama katika njia yake. Atasimama katika nchi ya uzuri, na uharibifu utakuwa mkononi wake.
Toda tisti, ki prihaja zoper njega, bo storil glede na svojo lastno voljo in nihče ne bo obstal pred njim. Ta pa bo stal v veličastni deželi, ki bo z njegovo roko použita.
17 Mfalme wa Kaskazini atauelekeza uso wake ili kuja kwa nguvu za ufalme wake wote, na kutakuwa na makubaliano atakayoyafanya na mfalme wa Kusini. Atampatia katika ndoa binti wa wanawake ili kuuharibu ufalme wa Kusini. Lakini mpango huo hautafanikiwa wala kumsaidia.
Svoj obraz bo tudi naravnal, da vstopi z močjo svojega celotnega kraljestva in pokončni z njim. Tako bo storil. Dal mu bo hčer izmed žensk, kvareč jo, toda ona ne bo obstala na njegovi strani niti ne bo zanj.
18 Baada ya hayo, mfalme atafuatilia nchi za pwani na ataziteka nchi nyingi. Lakini amiri jeshi atakikomesha kiburi chake na atakisababisha kiburi chake kiishe.
Potem bo svoj obraz obrnil k otokom in bo mnoge zavzel, toda princ bo zaradi svoje koristi povzročil, da bo zasramovanje, ki ga je ta dajal, prenehalo. Brez njegovega lastnega zasramovanja mu bo povzročil, da se to obrne nadenj.
19 Kisha atafuatilia miji yenye ngome katika nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka; na hatapatikana tena.
Potem bo svoj obraz obrnil proti utrdbi svoje lastne dežele, toda spotaknil se bo, padel in ne bo najden.
20 Kisha mtu mwingine atainuka katika nafasi ambaye atamfanya mtoza ushuru apite kwa ajili ya ufahari wa ufalme. Lakini katika siku zijazo atakatiliwa mbali, lakini si kwa hasira wala si katika vita.
Potem bo v svoji lastnini vstal prenašalec davkov v slavi kraljestva, toda v nekaj dneh bo uničen, niti z jezo, niti v bitki.
21 Katika nafasi atainuka mtu wa kudharauliwa ambaye watu hawatampa heshima ya nguvu ya kifalme; atakuja bila kukusudiwa na atautwaa ufalme kwa ulaghai.
V njegovi lastnini bo vstala podla oseba, ki ji ne bodo dali časti kraljestva, toda vstopil bo miroljubno in kraljestvo dosegel z laskanji.
22 Mbele yake, kila jeshi litafutiliwa mbali kama gharika. Jeshi na kiongozi wa agano wataangamizwa wote kwa pamoja.
S silami poplave bodo odplavljeni izpred njega in bodo zlomljeni; da, tudi princ zaveze.
23 Tangu katika kipindi kile ambacho makubaliano yalifanywa pamoja naye, ataenenda kwa kwa hila; atakuwa mwenye nguvu akiwa na watu wachache tu.
Potem ko z njim sklene sodelovanje, bo postopal varljivo, kajti prišel bo gor in postal močan z majhnim ljudstvom.
24 Kwa ghafla ataingia katika sehemu tajiri sana za jimbo, na atafanya kile ambacho si baba yake wala baba wa baba yake alishakifanya. Atagawanya mateka, nyara, na mali zake miongoni mwa wafuasi wake. Atapanga mpango wa kuiangusha ngome, lakini ni kwa muda tu.
Vstopil bo miroljubno, celo na najrodovitnejše kraje province. Počel bo to, kar njegovi očetje niso storili niti očetje njihovih očetov. Mednje bo razkropil plen, oplenjeno in bogastva. Da, napovedal bo svoje naklepe zoper oporišča, celo za nekaj časa.
25 Ataamsha nguvu zake na moyo wake kinyume na mfalme wa Kusini kwa jeshi kubwa. Mfalme wa Kusini atapigana vita akiwa na jeshi kubwa lenye nguvu, lakini hataweza kusimama kwa kuwa wengine watafanya njama dhidi yake.
Z veliko vojsko bo razvnel svojo moč in svoj pogum zoper južnega kralja, in južni kralj bo razvnet v bitko z veliko in mogočno vojsko, toda ne bo obstal, kajti zoper njega bodo napovedali naklepe.
26 Hata wale wanaokula chakula chake kizuri watajaribu kumwangamiza. Jeshi lake litakatiliwa mbali kama gharika, na wengi wao watauawa.
Da, tisti, ki se hranijo od deleža njegove hrane, ga bodo uničili in njegova vojska se bo razkropila. Mnogi bodo popadali umorjeni.
27 Wafalme wote hawa wawili, wakiwa na mioyo yao imejawa na uovu kinyume na mwenzake, watakaa katika meza moja na kudanganyana, lakini haitakuwa na maana yoyote. Kwa kuwa mwisho utatokea katika kipindi ambacho kimeshapangwa.
Srci obeh teh kraljev bosta počeli vragolijo in pri eni mizi bosta govorila laži. Toda to ne bo uspelo, kajti vendar bo konec ob določenem času.
28 Kisha mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake akiwa na utajiri mkubwa, na moyo wake ukipinga vikali agano takatifu. Atatenda na kisha atarudi katika nchi yake mwenyewe.
Potem se bo vrnil v svojo deželo z velikimi bogastvi, in njegovo srce bo zoper sveto zavezo. Počel bo junaška dejanja in se vrnil v svojo lastno deželo.
29 Katika muda uloamriwa atarudi na kuushambulia ufalme wa Kusini. Lakini katika kipindi hiki hakitakuwa kama awali.
Ob določenem času se bo vrnil in prišel proti jugu, toda ta ne bo kakor prejšnji ali kakor zadnji.
30 Kwa kuwa meli kutoka Kitimu zitamshambulia, naye ataogopa na kurudi nyuma. Atakuwa mwenye hasira dhidi ya agano takatifu, na atawaonyesha mema wale watakaoliacha agano takatifu.
Kajti ladje Kitéjcev bodo prišle zoper njega. Zato bo užaloščen, se vrnil in bo ogorčen zoper sveto zavezo. Tako bo storil; torej vrnil se bo in imel posvet s tistimi, ki so zapustili sveto zavezo.
31 Majeshi yake yatainuka na kukufuru sehemu takatifu katika ngome. Wataziondoa sadaka za kawaida za kuteketezwa, na watasimamisha chukizo la uharibifu litakalosababisha ukiwa.
Sile bodo stopile na njegovo stran in oskrunili bodo svetišče moči in odpravili bodo dnevno daritev in postavili ogabnost, ki dela opustošenje.
32 Na kwa wale walioenenda kwa ouvu kinyume na agano, atawadanganya na kuwatia uovu. Bali watu wale wanaomjua Mungu wao watakuwa jasiri na watachukua hatua.
Tiste, ki zlobno ravnajo zoper zavezo, bo pokvaril z laskanji, toda ljudstvo, ki pozna svojega Boga, bo močno in delalo bo junaška dela.
33 Watu wenye hekima miongobi mwa watu watawafanya watu waelewe. Lakini watajikwaa kwa upanga na kwa miali ya moto; watatiwa mateka na kunyang'anywa kwa siku.
Tisti med ljudstvom, ki razumejo, bodo poučevali mnoge, vendar bodo padali pod mečem in v plamenu, v ujetništvu in po plenjenju, mnogo dni.
34 Katika siku za kujikwaa kwao, watasaidiwa kwa msaada kidogo. Watu wengi watajiunga nao wenyewe katika unafiki.
Torej ko bodo padali, jim bo pomagano z majhno pomočjo, toda mnogi se jih bodo oklenili z laskanji.
35 Baadhi ya watu wenye hekima watajikwaa ili kujisafisha kutokee kwao, na kujiosha, na kujitakasa, mpaka wakati wa mwisho. Kwa kuwa wakati ulioamriwa haujaja bado.
Nekateri izmed tistih z razumevanjem bodo padli, da se jih preizkusi in prečisti in se jih naredi bele, celó do časa konca, ker je to še za določeni čas.
36 Mfalme atafanya kutokana na matakwa yake. Atajiinua mwenyewe na kujifanya mkubwa kuliko kila mungu. Kinyume cha Mungu wa miungu, atasema vitu vibaya, kwa kuwa atafanikiwa mpaka pale ghadhabu itakapokuwa imekamilika. Kwa ajili kile kilichoamriwa kitakapokuwa kimefanyika.
Kralj pa bo počel glede na svojo voljo in poviševal se bo in se poveličeval nad vsakega boga in govoril bo osupljive stvari zoper Boga bogov in uspeval bo, dokler ne bo dovršeno ogorčenje, kajti to, kar je določeno, bo storjeno.
37 Hatazijali miungu ya baba zake wala mungu anayependwa na wanawake. Wala hatamjali mungu mwingine yeyote. Kwa kuwa zaidi ya mtu yeyote atajifanya mwenyewe kuwa mkuu.
Niti se ne bo oziral na Boga svojih očetov, niti na željo žensk, niti na kateregakoli boga, kajti poveličeval se bo nad vse.
38 Atamheshimu mungu wa ngome badala ya haya. Ni mungu ambaye baba zake hawakumkubali ambaye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa mawe ya thamani na zawadi zenye kuthaminiwa.
Toda v svoji lastnini bo spoštoval boga sil, in boga, ki ga njegovi očetje niso poznali, bo častil z zlatom, srebrom, dragocenimi kamni in prijetnimi stvarmi.
39 Atazishambulia ngome imara sana kwa msaada wa mungu mgeni. Atampa heshima kubwa yeyote anayemkubali. Atawafanya kuwa watawala juu ya watu wengi, na ataigawanya nchi kama thawabu.
Tako bo storil v najmočnejših oporiščih s tujim bogom, ki ga bo priznal in narastel s slavo. Povzročil jim bo, da vladajo nad mnogimi in deželo bo razdelil zaradi dobička.
40 Kwa wakati wa mwisho mfalme wa Kusini atamshambulia. Mfalme wa Kaskazini atamvamia kwa ukali wa magari na wapanda farasi, na meli nyingi. Naye ataenda kinyume cha nchi, kuwagharikisha, na kupita katikati.
Ob času konca bo južni kralj pritisnil nanj in severni kralj bo prišel proti njemu kot vrtinčast veter, z bojnimi vozovi in s konjeniki in z mnogimi ladjami in vstopil bo v dežele, jih preplavil in prešel.
41 Naye ataingia katika nchi ya uzuri, makumi elfu ya Waisraeli wataanguka. Lakini watu hawa watatoroka kutoka katika mkono wake: Waedomu, Wamoabu, na mabaki ya watu wa Amoni.
Vstopil bo tudi v veličastno deželo in mnoge dežele bodo premagane, toda te bodo pobegnile iz njegove roke, celó Edóm, Moáb in vodja Amónovih sinov.
42 Naye ataunyosha mkono katika nchi; nchi ya Misri haitaokolewa.
Svojo roko bo iztegnil tudi nad dežele in egiptovska dežela ne bo ubežala.
43 Atakuwa na mamlaka juu ya hazina za dhahabu na za fedha, na juu ya utajiri wote wa Misri; watu wa Libya na Ethiopia watakuwa chini katika nyayo za miguu yake.
Toda imel bo oblast nad zakladi iz zlata, srebra in nad vsemi dragocenimi egiptovskimi stvarmi in Libijci in Etiopijci bodo pri njegovih korakih.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamwogopesha, naye atatoka akiwa mwenye hasira nyingi kuwa ili kuwaharibu kabisa na kuwahifadhi kwa ajli ya uharibifu.
Toda novice iz vzhoda in iz severa ga bodo vznemirile, zato bo šel naprej z veliko razjarjenostjo, da uniči in popolnoma odpravi mnoge.
45 Naye ataisimamisha hema ya makao yake ya kifalme kati ya bahari na milima ya uzuri wa utakatifu. Ataufikia mwisho wake, na hapatakuwa na msaidizi wa kumsadia.
Zasadil bo šotorska svetišča svoje palače med morjem in veličastno sveto goro, vendar bo prišel do svojega konca in nihče mu ne bo pomagal.

< Danieli 11 >