< Danieli 11 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa Dario Mmedi, mimi mwenyewe nilikuja kumwezesha na kumlinda Mikaeli.
Or en la première année de Darius le Mède j'assistais pour l'affermir et le fortifier.
2 Na sasa nitakufunulia ukweli. Wafalme watatu watainuka katika Uajemi, na mfalme wa nne atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Na wakati atakapopata nguvu kupitia utajiri wake, atamwamsha kila mtu kinyume na ufalme wa Ugiriki.
Et maintenant aussi je te ferai savoir la vérité: Voici, il y aura encore trois Rois en Perse, puis le quatrième possédera de grandes richesses par-dessus tous; et s'étant fortifié par ses richesses il soulèvera tout [le monde] contre le Royaume de Javan.
3 Mfalme wenye nguvu atainuka ambaye atatawala ufalme mkubwa, na ataenenda kufuatana na matakwa yake mwenyewe.
Et un Roi puissant se lèvera, et dominera avec une grande puissance, et fera selon sa volonté.
4 Na atakapokuwa ameinuka, ufalme wake utavunjika na utagawanyika katika pepo nne za mbinguni, lakini hawatakuwa wazao wake mwenyewe, na si kwa nguvu zake kwa wakati alipokuwa akitawala. Kwa kuwa ufalme wake utang'olewa kwa ajili ya wengine tofauti na wazawa wake.
Et sitôt qu'il sera en état, son Royaume sera brisé, et partagé vers les quatre vents des cieux, et ne sera point pour sa race, ni selon la domination avec laquelle il aura dominé: car son Royaume sera extirpé, et sera donné à d'autres, outre ceux-là.
5 Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja kati ya maamiri jeshi wake atakuwa mwenye nguvu kuliko yeye na atautawala ufalme wake kwa nguvu kubwa.
Et le Roi du Midi sera fort puissant, mais un des principaux chefs du [Roi de Javan] sera plus puissant que [le Roi du Midi], et dominera, et sa domination [sera] une grande domination.
6 Baada ya miaka michache, wakati muda utakapokuwa sawa, watafanya mwungano. Binti wa mfalme wa Kusini atakuja kwa mfalme wa Kaskazini kuyathibitisha makubaliano yao. Lakini hataweza kuzitunza nguvu za mkono wake, wala mfalme hatasimama wala mkono wake. Ataachwa na wale waliomleta, na baba yake, na yeye aliyemwunga mkono katika nyakati hizo.
Et au bout de [certaines] années ils s'allieront, et la fille du Roi du Midi viendra vers le Roi de l'Aquilon, pour redresser les affaires; mais elle ne retiendra point la force du bras, et [ni lui] ni son bras ne subsisteront point; mais elle sera livrée, et ceux aussi qui l'auront amenée, et celui qui sera né d'elle, et qui la fortifiait en ces temps-là.
7 Lakini tawi kutoka katika mizizi yake litachipuka katika nafasi yake. Atalishambulia jeshi na kuingia ngome ya mfalme wa Kaskazini. Atapigana nao, na atawashinda.
Mais le soutien [du Royaume] du Midi s'élèvera d'un rejeton des racines d'elle, et viendra à l'armée, et entrera dans les forteresses du Roi de l'Aquilon, et y fera [de grands exploits], et se fortifiera.
8 Ataichukua miungu yao mpaka Misri pamoa na sanamu zao za chuma na vyombo vyao vya fedha na vya dhahabu vyenye thamani. Kwa miaka mingi atakaa mbali na mfalme wa Kaskazini.
Et même il emmènera captifs en Egypte leurs dieux avec les vaisseaux de leurs aspersions, et avec leurs vaisseaux précieux d'argent et d'or, et il subsistera quelques années plus que le Roi de l'Aquilon.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atauvamia ufalme wa mfalme wa Kusini, lakini atajitoa na kwenda katika nchi yake mwenyewe.
Et le Roi du Midi entrera dans [son] Royaume, mais il s'en retournera en son pays.
10 Wana wake watajiweka tayari na kuunganisha jeshi kubwa. Litaendelea kukua na litagharikisha kila kitu, litapita katikati hadi kwenye ngome yake.
Mais les fils de celui-là entreront en guerre, et assembleront une multitude de grandes armées; puis [l'un d'eux] viendra certainement, et se répandra, et passera; il retournera, dis-je, et s'avancera en bataille jusqu'à la forteresse [du Roi du Midi].
11 Ndipo mfalme wa Kusini atakasirika, na ataenda na kupigana naye, mfalme wa Kaskazini. Mfalme wa Kaskazini atainua jeshi kubwa, bali jeshi litatiwa katika mkono wake.
Et le Roi du Midi sera irrité, et sortira, et combattra contre lui, [savoir] contre le Roi de l'Aquilon; et il assemblera une grande multitude, et cette multitude sera livrée entre les mains du Roi du Midi.
12 Jeshi litachukuliwa, na moyo wa mfalme wa Kusini utainuliwa juu, na atawafanya makumi maelfu kuanguka, lakini hataweza kuwa mshindi.
Et après avoir défait cette multitude il élèvera son cœur, et abattra des [gens] à milliers, mais il ne sera pas fortifié.
13 Kisha mfalme wa Kaskazini atainua jeshi jingine, kubwa kuliko la kwanza. Baada ya miaka kadhaa, mfalme wa Kaskazini atakuja na jeshi kubwa likiwa na vifaa vingi.
Car le Roi de l'Aquilon reviendra, et assemblera une plus grande multitude que la première, et au bout de quelque temps, [savoir], de quelques années, il viendra certainement avec une grande armée, et un grand appareil.
14 Katika siku hizo wengi watainuka kinyume na mfalmea wa Kusini. Wana wa vurugu miongoni mwa watu wake watasimama wao wenyewe ili kuyatimiliza maono, lakini watajikwaa.
Et en ce temps-là plusieurs s'élèveront contre le Roi du Midi; et les hommes violents de ton peuple s'élèveront, afin de confirmer la vision, mais ils tomberont.
15 Mfalme wa Kaskazini atakuja, kuizingira nchi kwa kuweka vilima, na kuuteka mji wenye ngome. Majeshi ya Kusini hayataweza kusimama, hata wanajeshi wake bora. Hawatakuwa na nguvu za kusimama.
Et le Roi de l'Aquilon viendra, et fera des terrasses, et prendra les villes fortes; et les bras du Midi, ni son peuple d'élite ne pourront point résister, car [il n'y aura] point de force pour résister.
16 Badala yake, yeye ajaye ataenenda kwa kufuata tamaa zake kinyume chake; hakuna yeyote atakayesimama katika njia yake. Atasimama katika nchi ya uzuri, na uharibifu utakuwa mkononi wake.
Et il fera de celui qui sera venu contre lui, selon sa volonté, et il n'y aura personne qui tienne ferme devant lui; et il s'arrêtera au pays de noblesse, et il y aura consomption par sa force.
17 Mfalme wa Kaskazini atauelekeza uso wake ili kuja kwa nguvu za ufalme wake wote, na kutakuwa na makubaliano atakayoyafanya na mfalme wa Kusini. Atampatia katika ndoa binti wa wanawake ili kuuharibu ufalme wa Kusini. Lakini mpango huo hautafanikiwa wala kumsaidia.
Puis il tournera sa face pour entrer par force dans tout le Royaume de celui-là, et ses affaires iront bien, et il fera de [grands exploits], et il lui donnera une fille de femmes, pour ruiner le Royaume; mais [cela] ne tiendra point, et elle ne sera point pour lui.
18 Baada ya hayo, mfalme atafuatilia nchi za pwani na ataziteka nchi nyingi. Lakini amiri jeshi atakikomesha kiburi chake na atakisababisha kiburi chake kiishe.
Puis il tournera sa face vers les Iles, et en prendra plusieurs, mais un capitaine l'obligera de cesser l'opprobre qu'il faisait, et outre cela il fera retomber sur lui son opprobre.
19 Kisha atafuatilia miji yenye ngome katika nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka; na hatapatikana tena.
Puis il tournera visage vers les forteresses de son pays, il heurtera, il sera renversé, et il ne sera plus trouvé.
20 Kisha mtu mwingine atainuka katika nafasi ambaye atamfanya mtoza ushuru apite kwa ajili ya ufahari wa ufalme. Lakini katika siku zijazo atakatiliwa mbali, lakini si kwa hasira wala si katika vita.
Et un autre sera établi en sa place, qui enverra l'exacteur pour la Majesté Royale, et il sera détruit dans peu de jours, mais non dans une rencontre, ni dans une bataille.
21 Katika nafasi atainuka mtu wa kudharauliwa ambaye watu hawatampa heshima ya nguvu ya kifalme; atakuja bila kukusudiwa na atautwaa ufalme kwa ulaghai.
Et en sa place il en sera établi un autre qui sera méprisé, auquel on ne donnera point l'honneur royal; mais il viendra en paix, et il occupera le Royaume par des flatteries.
22 Mbele yake, kila jeshi litafutiliwa mbali kama gharika. Jeshi na kiongozi wa agano wataangamizwa wote kwa pamoja.
Et les bras des grandes eaux seront engloutis par un déluge devant lui, et seront rompus, et il sera le Chef d'un accord.
23 Tangu katika kipindi kile ambacho makubaliano yalifanywa pamoja naye, ataenenda kwa kwa hila; atakuwa mwenye nguvu akiwa na watu wachache tu.
Mais après les accords faits avec lui, il usera de tromperie, et il montera, et se renforcera avec peu de gens.
24 Kwa ghafla ataingia katika sehemu tajiri sana za jimbo, na atafanya kile ambacho si baba yake wala baba wa baba yake alishakifanya. Atagawanya mateka, nyara, na mali zake miongoni mwa wafuasi wake. Atapanga mpango wa kuiangusha ngome, lakini ni kwa muda tu.
Il entrera dans les lieux gras d'une Province [alors] paisible, et il fera des choses que ses pères, ni les pères de ses pères, n'ont point faites; il leur répandra le pillage, le butin, et les richesses; et il formera des desseins contre les forteresses: et cela jusqu'à un certain temps.
25 Ataamsha nguvu zake na moyo wake kinyume na mfalme wa Kusini kwa jeshi kubwa. Mfalme wa Kusini atapigana vita akiwa na jeshi kubwa lenye nguvu, lakini hataweza kusimama kwa kuwa wengine watafanya njama dhidi yake.
Puis il réveillera sa force et son cœur contre le Roi du Midi, avec une grande armée, et le Roi du Midi s'avancera en bataille avec une très grande et très forte armée, mais il ne subsistera point, parce qu'on formera des entreprises contre lui.
26 Hata wale wanaokula chakula chake kizuri watajaribu kumwangamiza. Jeshi lake litakatiliwa mbali kama gharika, na wengi wao watauawa.
Et ceux qui mangent les mets de sa table le mettront en pièces, et son armée sera accablée, comme d'un déluge, et beaucoup de gens tomberont blessés à mort.
27 Wafalme wote hawa wawili, wakiwa na mioyo yao imejawa na uovu kinyume na mwenzake, watakaa katika meza moja na kudanganyana, lakini haitakuwa na maana yoyote. Kwa kuwa mwisho utatokea katika kipindi ambacho kimeshapangwa.
Et le cœur de ces deux Rois sera [adonné] à s'entre-nuire, et ils parleront en une même table avec tromperie, ce qui ne tournera point à bien; car il y aura encore une fin au temps ordonné.
28 Kisha mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake akiwa na utajiri mkubwa, na moyo wake ukipinga vikali agano takatifu. Atatenda na kisha atarudi katika nchi yake mwenyewe.
Après quoi il s'en retournera en son pays avec de grandes richesses, et son cœur sera contre la sainte alliance, et il fera [de grands exploits], puis il retournera en son pays.
29 Katika muda uloamriwa atarudi na kuushambulia ufalme wa Kusini. Lakini katika kipindi hiki hakitakuwa kama awali.
[Ensuite] il retournera au temps préfix, et il viendra contre le Midi, mais cette dernière [expédition] ne sera pas comme la précédente.
30 Kwa kuwa meli kutoka Kitimu zitamshambulia, naye ataogopa na kurudi nyuma. Atakuwa mwenye hasira dhidi ya agano takatifu, na atawaonyesha mema wale watakaoliacha agano takatifu.
Car les navires de Kittim viendront contre lui, dont il sera contristé, et il s'en retournera, et il sera irrité contre la sainte alliance, et fera [de grands exploits], et retournera, et s'entendra avec les apostats de la sainte alliance.
31 Majeshi yake yatainuka na kukufuru sehemu takatifu katika ngome. Wataziondoa sadaka za kawaida za kuteketezwa, na watasimamisha chukizo la uharibifu litakalosababisha ukiwa.
Et les forces seront de son côté, et on souillera le Sanctuaire, qui est la forteresse, et on ôtera le sacrifice continuel, et on y mettra l'abomination qui causera la désolation.
32 Na kwa wale walioenenda kwa ouvu kinyume na agano, atawadanganya na kuwatia uovu. Bali watu wale wanaomjua Mungu wao watakuwa jasiri na watachukua hatua.
Et il fera pécher par flatteries ceux qui se porteront méchamment dans l'alliance; mais le peuple de ceux qui connaîtront leur Dieu se fortifiera, et fera [de grands exploits.]
33 Watu wenye hekima miongobi mwa watu watawafanya watu waelewe. Lakini watajikwaa kwa upanga na kwa miali ya moto; watatiwa mateka na kunyang'anywa kwa siku.
Et les plus intelligents d'entre le peuple donneront instruction à plusieurs, et il y en aura qui tomberont par l'épée et par la flamme, ou qui seront en captivité et en proie durant plusieurs jours.
34 Katika siku za kujikwaa kwao, watasaidiwa kwa msaada kidogo. Watu wengi watajiunga nao wenyewe katika unafiki.
Et lorsqu'ils tomberont ainsi, ils seront un peu secourus; mais plusieurs se joindront à eux sous un beau semblant.
35 Baadhi ya watu wenye hekima watajikwaa ili kujisafisha kutokee kwao, na kujiosha, na kujitakasa, mpaka wakati wa mwisho. Kwa kuwa wakati ulioamriwa haujaja bado.
Et quelques-uns de ces plus intelligents tomberont, afin qu'il y en ait d'entre eux qui soient rendus éprouvés, qui soient épurés, et qui soient blanchis, jusqu'au temps déterminé; car cela est encore pour un certain temps.
36 Mfalme atafanya kutokana na matakwa yake. Atajiinua mwenyewe na kujifanya mkubwa kuliko kila mungu. Kinyume cha Mungu wa miungu, atasema vitu vibaya, kwa kuwa atafanikiwa mpaka pale ghadhabu itakapokuwa imekamilika. Kwa ajili kile kilichoamriwa kitakapokuwa kimefanyika.
Ce Roi donc fera selon sa volonté, et s'enorgueillira, et s'élèvera par-dessus tout Dieu; il proférera des choses étranges contre le Dieu des dieux, et prospérera jusqu'à ce que l'indignation ait pris fin; car la détermination en a été faite.
37 Hatazijali miungu ya baba zake wala mungu anayependwa na wanawake. Wala hatamjali mungu mwingine yeyote. Kwa kuwa zaidi ya mtu yeyote atajifanya mwenyewe kuwa mkuu.
Et il ne se souciera point des dieux de ses pères, ni de l'amour des femmes, même il ne se souciera d'aucun Dieu; car il s'élèvera au-dessus de tout.
38 Atamheshimu mungu wa ngome badala ya haya. Ni mungu ambaye baba zake hawakumkubali ambaye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa mawe ya thamani na zawadi zenye kuthaminiwa.
Mais il honorera dans son lieu le dieu Mahuzzim, il honorera, dis-je, avec de l'or et de l'argent, et des pierres précieuses, et des choses désirables, le dieu que ses pères n'ont point connu.
39 Atazishambulia ngome imara sana kwa msaada wa mungu mgeni. Atampa heshima kubwa yeyote anayemkubali. Atawafanya kuwa watawala juu ya watu wengi, na ataigawanya nchi kama thawabu.
Et il fera [de grands exploits] dans les forteresses les plus fortes, tenant le parti du dieu inconnu qu'il aura connu, il [leur] multipliera la gloire, et les fera dominer sur plusieurs, et leur partagera le pays à prix d'argent.
40 Kwa wakati wa mwisho mfalme wa Kusini atamshambulia. Mfalme wa Kaskazini atamvamia kwa ukali wa magari na wapanda farasi, na meli nyingi. Naye ataenda kinyume cha nchi, kuwagharikisha, na kupita katikati.
Et au temps déterminé le Roi du Midi choquera avec lui de ses cornes mais le Roi de l'Aquilon se lèvera contre lui comme une tempête, avec des chariots et des gens de cheval, et avec plusieurs navires, et il entrera dans ses terres, et les inondera, et passera outre.
41 Naye ataingia katika nchi ya uzuri, makumi elfu ya Waisraeli wataanguka. Lakini watu hawa watatoroka kutoka katika mkono wake: Waedomu, Wamoabu, na mabaki ya watu wa Amoni.
Et il entrera au pays de noblesse, et plusieurs pays seront ruinés, mais ceux-ci réchapperont de sa main, [savoir], Edom, et Moab, et le principal lieu des enfants de Hammon.
42 Naye ataunyosha mkono katika nchi; nchi ya Misri haitaokolewa.
Il mettra donc la main sur ces pays-là; et le pays d'Egypte n'échappera point.
43 Atakuwa na mamlaka juu ya hazina za dhahabu na za fedha, na juu ya utajiri wote wa Misri; watu wa Libya na Ethiopia watakuwa chini katika nyayo za miguu yake.
Il se rendra maître des trésors d'or et d'argent, et de toutes les choses désirables de l'Egypte; les Libyens et ceux de Cus seront à sa suite.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamwogopesha, naye atatoka akiwa mwenye hasira nyingi kuwa ili kuwaharibu kabisa na kuwahifadhi kwa ajli ya uharibifu.
Mais les nouvelles de l'Orient et de l'Aquilon le troubleront, et il sortira avec une grande fureur, pour détruire et exterminer beaucoup de gens.
45 Naye ataisimamisha hema ya makao yake ya kifalme kati ya bahari na milima ya uzuri wa utakatifu. Ataufikia mwisho wake, na hapatakuwa na msaidizi wa kumsadia.
Et il dressera les tentes de sa maison royale entre les mers, à l'[opposite] de la noble montagne de la sainteté; mais il viendra à sa fin, et personne ne lui donnera du secours.

< Danieli 11 >