< Danieli 11 >
1 Katika mwaka wa kwanza wa Dario Mmedi, mimi mwenyewe nilikuja kumwezesha na kumlinda Mikaeli.
Also I, in ye first yere of Darius of ye Medes, euen I stood to incourage and to strengthen him.
2 Na sasa nitakufunulia ukweli. Wafalme watatu watainuka katika Uajemi, na mfalme wa nne atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Na wakati atakapopata nguvu kupitia utajiri wake, atamwamsha kila mtu kinyume na ufalme wa Ugiriki.
And now wil I shew thee ye trueth, Behold, there shall stand vp yet three Kings in Persia, and the fourth shall be farre richer then they all: and by his strength, and by his riches he shall stirre vp all against the realme of Grecia.
3 Mfalme wenye nguvu atainuka ambaye atatawala ufalme mkubwa, na ataenenda kufuatana na matakwa yake mwenyewe.
But a mightie King shall stand vp, that shall rule with great dominion, and doe according to his pleasure.
4 Na atakapokuwa ameinuka, ufalme wake utavunjika na utagawanyika katika pepo nne za mbinguni, lakini hawatakuwa wazao wake mwenyewe, na si kwa nguvu zake kwa wakati alipokuwa akitawala. Kwa kuwa ufalme wake utang'olewa kwa ajili ya wengine tofauti na wazawa wake.
And when he shall stand vp, his kingdome shall be broken, and shall be deuided towarde the foure windes of heauen: and not to his posteritie, nor according to his dominion, which he ruled: for his kingdome shall be pluckt vp, euen to be for others besides those.
5 Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja kati ya maamiri jeshi wake atakuwa mwenye nguvu kuliko yeye na atautawala ufalme wake kwa nguvu kubwa.
And ye King of ye South shalbe mightie, and one of his princes, and shall preuaile against him, and beare rule: his dominio shalbe a great dominion.
6 Baada ya miaka michache, wakati muda utakapokuwa sawa, watafanya mwungano. Binti wa mfalme wa Kusini atakuja kwa mfalme wa Kaskazini kuyathibitisha makubaliano yao. Lakini hataweza kuzitunza nguvu za mkono wake, wala mfalme hatasimama wala mkono wake. Ataachwa na wale waliomleta, na baba yake, na yeye aliyemwunga mkono katika nyakati hizo.
And in the ende of yeeres they shalbe ioyned together: for the Kings daughter of ye South shall come to the King of the North to make an agreement, but she shall not reteine the power of the arme, neither shall he continue, nor his arme: but she shall be deliuered to death, and they that brought her, and he that begate her, and he that comforted her in these times.
7 Lakini tawi kutoka katika mizizi yake litachipuka katika nafasi yake. Atalishambulia jeshi na kuingia ngome ya mfalme wa Kaskazini. Atapigana nao, na atawashinda.
But out of the bud of her rootes shall one stand vp in his stead, which shall come with an armie, and shall enter into the fortresse of the King of the North, and doe with them as he list, and shall preuaile,
8 Ataichukua miungu yao mpaka Misri pamoa na sanamu zao za chuma na vyombo vyao vya fedha na vya dhahabu vyenye thamani. Kwa miaka mingi atakaa mbali na mfalme wa Kaskazini.
And shall also carie captiues into Egypt their gods with their molten images, and with their precious vessels of siluer and of golde, and he shall continue more yeeres then the King of the North.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atauvamia ufalme wa mfalme wa Kusini, lakini atajitoa na kwenda katika nchi yake mwenyewe.
So the King of ye South shall come into his kingdome, and shall returne into his owne land.
10 Wana wake watajiweka tayari na kuunganisha jeshi kubwa. Litaendelea kukua na litagharikisha kila kitu, litapita katikati hadi kwenye ngome yake.
Wherefore his sonnes shall be stirred vp, and shall assemble a mightie great armie: and one shall come, and ouerflowe, and passe through: then shall he returne, and be stirred vp at his fortresse.
11 Ndipo mfalme wa Kusini atakasirika, na ataenda na kupigana naye, mfalme wa Kaskazini. Mfalme wa Kaskazini atainua jeshi kubwa, bali jeshi litatiwa katika mkono wake.
And the King of the South shall be angrie, and shall come foorth, and fight with him, euen with the King of the North: for he shall set foorth a great multitude, and the multitude shall be giuen into his hand.
12 Jeshi litachukuliwa, na moyo wa mfalme wa Kusini utainuliwa juu, na atawafanya makumi maelfu kuanguka, lakini hataweza kuwa mshindi.
Then the multitude shall be proude, and their heart shall be lifted vp: for hee shall cast downe thousands: but he shall not still preuaile.
13 Kisha mfalme wa Kaskazini atainua jeshi jingine, kubwa kuliko la kwanza. Baada ya miaka kadhaa, mfalme wa Kaskazini atakuja na jeshi kubwa likiwa na vifaa vingi.
For the King of the North shall returne, and shall set foorth a greater multitude then afore, and shall come foorth (after certeine yeeres) with a mightie armie, and great riches.
14 Katika siku hizo wengi watainuka kinyume na mfalmea wa Kusini. Wana wa vurugu miongoni mwa watu wake watasimama wao wenyewe ili kuyatimiliza maono, lakini watajikwaa.
And at the same time there shall many stand vp against the King of the South: also the rebellious children of thy people shall exalt them selues to establish the vision, but they shall fall.
15 Mfalme wa Kaskazini atakuja, kuizingira nchi kwa kuweka vilima, na kuuteka mji wenye ngome. Majeshi ya Kusini hayataweza kusimama, hata wanajeshi wake bora. Hawatakuwa na nguvu za kusimama.
So the King of the North shall come, and cast vp a mount, and take the strong citie: and the armes of the South shall not resist, neither his chosen people, neither shall there be any strength to withstand.
16 Badala yake, yeye ajaye ataenenda kwa kufuata tamaa zake kinyume chake; hakuna yeyote atakayesimama katika njia yake. Atasimama katika nchi ya uzuri, na uharibifu utakuwa mkononi wake.
But he that shall come, shall doe vnto him as he list, and none shall stand against him: and he shall stand in the pleasant land, which by his hand shalbe consumed.
17 Mfalme wa Kaskazini atauelekeza uso wake ili kuja kwa nguvu za ufalme wake wote, na kutakuwa na makubaliano atakayoyafanya na mfalme wa Kusini. Atampatia katika ndoa binti wa wanawake ili kuuharibu ufalme wa Kusini. Lakini mpango huo hautafanikiwa wala kumsaidia.
Againe he shall set his face to enter with the power of his whole kingdome, and his confederates with him: thus shall he doe, and he shall giue him the daughter of women, to destroy her: but she shall not stande on his side, neither bee for him.
18 Baada ya hayo, mfalme atafuatilia nchi za pwani na ataziteka nchi nyingi. Lakini amiri jeshi atakikomesha kiburi chake na atakisababisha kiburi chake kiishe.
After this shall he turne his face vnto the yles, and shall take many, but a prince shall cause his shame to light vpon him, beside that he shall cause his owne shame to turne vpon himselfe.
19 Kisha atafuatilia miji yenye ngome katika nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka; na hatapatikana tena.
For he shall turne his face toward the fortes of his owne land: but he shall be ouerthrowen and fall, and be no more founde.
20 Kisha mtu mwingine atainuka katika nafasi ambaye atamfanya mtoza ushuru apite kwa ajili ya ufahari wa ufalme. Lakini katika siku zijazo atakatiliwa mbali, lakini si kwa hasira wala si katika vita.
Then shall stand vp in his place in the glorie of the kingdome, one that shall raise taxes: but after fewe dayes he shall be destroyed, neither in wrath, nor in battell.
21 Katika nafasi atainuka mtu wa kudharauliwa ambaye watu hawatampa heshima ya nguvu ya kifalme; atakuja bila kukusudiwa na atautwaa ufalme kwa ulaghai.
And in his place shall stand vp a vile person, to whom they shall not giue the honour of the kingdome: but he shall come in peaceably, and obteine the kingdome by flatteries.
22 Mbele yake, kila jeshi litafutiliwa mbali kama gharika. Jeshi na kiongozi wa agano wataangamizwa wote kwa pamoja.
And the armes shall be ouerthrowen with a flood before him, and shall be broken: and also the prince of the couenant.
23 Tangu katika kipindi kile ambacho makubaliano yalifanywa pamoja naye, ataenenda kwa kwa hila; atakuwa mwenye nguvu akiwa na watu wachache tu.
And after the league made with him, he shall worke deceitfully: for he shall come vp, and ouercome with a small people.
24 Kwa ghafla ataingia katika sehemu tajiri sana za jimbo, na atafanya kile ambacho si baba yake wala baba wa baba yake alishakifanya. Atagawanya mateka, nyara, na mali zake miongoni mwa wafuasi wake. Atapanga mpango wa kuiangusha ngome, lakini ni kwa muda tu.
He shall enter into the quiet and plentifull prouince, and he shall doe that which his fathers haue not done, nor his fathers fathers: he shall deuide among them the pray and the spoyle, and the substance, yea, and he shall forecast his deuises against the strong holdes, euen for a time.
25 Ataamsha nguvu zake na moyo wake kinyume na mfalme wa Kusini kwa jeshi kubwa. Mfalme wa Kusini atapigana vita akiwa na jeshi kubwa lenye nguvu, lakini hataweza kusimama kwa kuwa wengine watafanya njama dhidi yake.
Also he shall stirre vp his power and his courage against the King of the South with a great armie, and the King of the South shall be stirred vp to battell with a very great and mightie armie: but he shall not stand: for they shall forecast and practise against him.
26 Hata wale wanaokula chakula chake kizuri watajaribu kumwangamiza. Jeshi lake litakatiliwa mbali kama gharika, na wengi wao watauawa.
Yea, they that feede of the portion of his meate, shall destroy him: and his armie shall ouerflowe: and many shall fall, and be slaine.
27 Wafalme wote hawa wawili, wakiwa na mioyo yao imejawa na uovu kinyume na mwenzake, watakaa katika meza moja na kudanganyana, lakini haitakuwa na maana yoyote. Kwa kuwa mwisho utatokea katika kipindi ambacho kimeshapangwa.
And both these Kings hearts shall be to do mischiefe, and they shall talke of deceite at one table: but it shall not auaile: for yet the ende shall be at the time appointed.
28 Kisha mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake akiwa na utajiri mkubwa, na moyo wake ukipinga vikali agano takatifu. Atatenda na kisha atarudi katika nchi yake mwenyewe.
Then shall he returne into his land with great substance: for his heart shall be against the holy couenant: so shall he doe and returne to his owne land.
29 Katika muda uloamriwa atarudi na kuushambulia ufalme wa Kusini. Lakini katika kipindi hiki hakitakuwa kama awali.
At the time appointed he shall returne, and come toward the South: but the last shall not be as the first.
30 Kwa kuwa meli kutoka Kitimu zitamshambulia, naye ataogopa na kurudi nyuma. Atakuwa mwenye hasira dhidi ya agano takatifu, na atawaonyesha mema wale watakaoliacha agano takatifu.
For the shippes of Chittim shall come against him: therefore he shalbe sorie and returne, and freat against the holy couenant: so shall he doe, he shall euen returne and haue intelligence with them that forsake the holy couenant.
31 Majeshi yake yatainuka na kukufuru sehemu takatifu katika ngome. Wataziondoa sadaka za kawaida za kuteketezwa, na watasimamisha chukizo la uharibifu litakalosababisha ukiwa.
And armes shall stand on his part, and they shall pollute the Sanctuarie of strength, and shall take away the dayly sacrifice, and they shall set vp the abominable desolation.
32 Na kwa wale walioenenda kwa ouvu kinyume na agano, atawadanganya na kuwatia uovu. Bali watu wale wanaomjua Mungu wao watakuwa jasiri na watachukua hatua.
And such as wickedly breake ye couenant, shall he cause to sinne by flatterie: but the people that do know their God, shall preuaile and prosper.
33 Watu wenye hekima miongobi mwa watu watawafanya watu waelewe. Lakini watajikwaa kwa upanga na kwa miali ya moto; watatiwa mateka na kunyang'anywa kwa siku.
And they that vnderstand among the people, shall instruct many: yet they shall fall by sword, and by flame, by captiuitie and by spoile many dayes.
34 Katika siku za kujikwaa kwao, watasaidiwa kwa msaada kidogo. Watu wengi watajiunga nao wenyewe katika unafiki.
Nowe when they shall fall, they shall be holpen with a litle helpe: but many shall cleaue vnto them fainedly.
35 Baadhi ya watu wenye hekima watajikwaa ili kujisafisha kutokee kwao, na kujiosha, na kujitakasa, mpaka wakati wa mwisho. Kwa kuwa wakati ulioamriwa haujaja bado.
And some of the of vnderstanding shall fall to trie them, and to purge, and to make them white, till the time be out: for there is a time appointed.
36 Mfalme atafanya kutokana na matakwa yake. Atajiinua mwenyewe na kujifanya mkubwa kuliko kila mungu. Kinyume cha Mungu wa miungu, atasema vitu vibaya, kwa kuwa atafanikiwa mpaka pale ghadhabu itakapokuwa imekamilika. Kwa ajili kile kilichoamriwa kitakapokuwa kimefanyika.
And the King shall doe what him list: he shall exalt himselfe, and magnifie himselfe against all, that is God, and shall speake marueilous things against ye God of gods, and shall prosper, till ye wrath be accomplished: for ye determination is made.
37 Hatazijali miungu ya baba zake wala mungu anayependwa na wanawake. Wala hatamjali mungu mwingine yeyote. Kwa kuwa zaidi ya mtu yeyote atajifanya mwenyewe kuwa mkuu.
Neither shall he regard the God of his fathers, nor the desires of women, nor care for any God: for he shall magnifie himselfe aboue all.
38 Atamheshimu mungu wa ngome badala ya haya. Ni mungu ambaye baba zake hawakumkubali ambaye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa mawe ya thamani na zawadi zenye kuthaminiwa.
But in his place shall he honour the god Mauzzim, and the god whom his fathers knewe not, shall he honour with golde and with siluer, and with precious stones, and pleasant things.
39 Atazishambulia ngome imara sana kwa msaada wa mungu mgeni. Atampa heshima kubwa yeyote anayemkubali. Atawafanya kuwa watawala juu ya watu wengi, na ataigawanya nchi kama thawabu.
Thus shall he do in the holdes of Mauzzim with a strange god whom he shall acknowledge: he shall increase his glory, and shall cause them to rule ouer many and shall deuide ye land for gaine.
40 Kwa wakati wa mwisho mfalme wa Kusini atamshambulia. Mfalme wa Kaskazini atamvamia kwa ukali wa magari na wapanda farasi, na meli nyingi. Naye ataenda kinyume cha nchi, kuwagharikisha, na kupita katikati.
And at ye end of time shall the King of the South push at him, and the king of the North shall come against him like a whirlewind with charets, and with horsemen, and with many ships, and he shall enter into ye countreis, and shall ouerflow and passe through.
41 Naye ataingia katika nchi ya uzuri, makumi elfu ya Waisraeli wataanguka. Lakini watu hawa watatoroka kutoka katika mkono wake: Waedomu, Wamoabu, na mabaki ya watu wa Amoni.
He shall enter also into the pleasant land, and many countreis shalbe ouerthrowen: but these shall escape out of his hand, euen Edom and Moab, and the chiefe of the children of Ammon.
42 Naye ataunyosha mkono katika nchi; nchi ya Misri haitaokolewa.
He shall stretch foorth his hands also vpon the countreis, and ye land of Egypt shall not escape.
43 Atakuwa na mamlaka juu ya hazina za dhahabu na za fedha, na juu ya utajiri wote wa Misri; watu wa Libya na Ethiopia watakuwa chini katika nyayo za miguu yake.
But he shall haue power ouer the treasures of golde and of siluer, and ouer all the precious things of Egypt, and of the Lybians, and of the blacke Mores where he shall passe.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamwogopesha, naye atatoka akiwa mwenye hasira nyingi kuwa ili kuwaharibu kabisa na kuwahifadhi kwa ajli ya uharibifu.
But the tidings out of the East and the North shall trouble him: therefore he shall goe foorth with great wrath to destroy and roote out many.
45 Naye ataisimamisha hema ya makao yake ya kifalme kati ya bahari na milima ya uzuri wa utakatifu. Ataufikia mwisho wake, na hapatakuwa na msaidizi wa kumsadia.
And he shall plant the tabernacles of his palace betweene the seas in the glorious and holy mountaine, yet he shall come to his end, and none shall helpe him.