< Danieli 10 >

1 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza. Ujumbe huu ulikuwa ni wa kwelil. Ulihusu vita kuu. Danieli aliufahamu ujumbe alipopata ufumbuzi kutoka katika maono.
La troisième année de Cyrus, roi de Perse, un message fut révélé à Daniel, dont le nom était Beltschatsar, et le message était vrai, même une grande guerre. Il comprit le message, et il eut l'intelligence de la vision.
2 Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa katika maombolezo kwa wiki tatu.
En ces jours-là, moi, Daniel, je fus en deuil pendant trois semaines entières.
3 Sikula chakula kizuri, sikula nyama, sikunywa divai, na sikujipaka mafuta mwenyewe mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzima.
Je ne mangeais aucun mets agréable. Il n'est entré dans ma bouche ni viande ni vin. Je ne me suis pas oint du tout, jusqu'à ce que trois semaines entières soient accomplies.
4 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa niko karibu na mto mkubwa (ambao ni Tigrisi),
Le vingt-quatrième jour du premier mois, comme j'étais au bord du grand fleuve, qui est Hiddékel,
5 Nilitazama juu na nikamwona mtu aliyevaa kitani, akiwa na mkanda kiunoni mwake uliotengenezwa kwa dhahabu safi kutoka Ufazi.
je levai les yeux et je regardai. Et voici, c'était un homme vêtu de lin, et dont la taille était ornée d'or pur d'Uphaz.
6 Mwili wake ulikuwa kama kito, na sura yake ilikuwa kama radi. Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi, na mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa. Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu.
Son corps était semblable à du béryl, son visage avait l'aspect de l'éclair, et ses yeux étaient comme des torches enflammées. Ses bras et ses pieds étaient comme de l'airain poli. La voix de ses paroles était comme la voix d'une multitude.
7 Mimi, Danieli peke yangu niliyaona maono, na watu niliokuwa na pamoja hawakuyaona maono. Lakini, jambo kuu la kuogofya liliwaijia juu yao, na walikimbia na kujificha wao wenyewe.
Moi, Daniel, j'ai vu seul la vision, car les hommes qui étaient avec moi n'ont pas vu la vision, mais un grand tremblement est tombé sur eux, et ils ont fui pour se cacher.
8 Hivyo niliachwa peke yangu na niliyaona maono haya ajabu. Hakuna nguvu iliyobakia ndani yangu; mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu, na hazikubakia nguvu ndani yangu.
Je restai donc seul et je vis cette grande vision. Je n'avais plus de force, car mon visage était d'une pâleur mortelle, et je n'avais plus de force.
9 Kisha nikasikia maneno yake, na nilipoyasikia, nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito.
Mais j'ai entendu la voix de ses paroles. Quand j'entendis la voix de ses paroles, je tombai dans un profond sommeil, sur ma face, le visage tourné vers le sol.
10 Mkono ulinigusa, na ilinifanya nitetemeke katika magoti yangu na viganja vya mikono yangu.
Voici, une main me toucha, qui me mit à genoux et sur les paumes des mains.
11 Malaika aliniambia, “Danieli, mtu aliyetunzwa sana, yafahamu maneno ninayokwambia wewe. Simama wima, kwa kuwa nimeshakutuma.” Na alipomaliza kuniambia ujumbe huu, nilisimama nikiwa natetemeka.
Il me dit: « Daniel, homme bien-aimé, comprends les paroles que je te dis, et tiens-toi droit, car c'est maintenant que je suis envoyé vers toi. » Quand il m'eut dit cette parole, je me tins debout en tremblant.
12 Kisha aliniambia, “Usiogope, Danieli. Tangu siku ya kwanza ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele ya Mungu, maneno yako yalisikiwa, na nimekuja kwasababu ya maneno yako.
Alors il me dit: « Ne crains pas, Daniel, car dès le premier jour où tu as mis ton cœur à comprendre et à t'humilier devant ton Dieu, tes paroles ont été entendues. Je suis venu à cause de tes paroles.
13 Mwana wa mfalme wa ufalme wa Uajemi alinizuia, na niliwekwa huko na mfalme wa Uajemi kwa siku ishirini na moja. Lakini Mikaeli, mmoja kati ya wakuu alikuja kunisaidia.
Mais le prince du royaume de Perse m'a résisté vingt et un jours; et voici que Michel, l'un des principaux princes, est venu me secourir, parce que je suis resté là avec les rois de Perse.
14 Sasa nimekuja kukusaidia ili ufahamu kile kitakachotokea kwa watu wako katika siku za mwisho. Kwa kuwa maono ni kwa ajili siku ambazo hazijatokea bado.
Maintenant, je suis venu pour vous faire comprendre ce qui arrivera à votre peuple dans la suite des temps, car la vision est encore pour de nombreux jours. »
15 Na alipokuwa akali akiniambia maneno haya, niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini na sikuwa na uwezo wa kuzungumza.
Lorsqu'il m'eut dit ces paroles, je fixai mon visage à terre et je restai muet.
16 Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu alinigusa mdomo wangu na nifumbua kinywa changu na nilimwambia huyo aliyekuwa amesimam mbele yangu: “Bwana wangu, niko katika masumbuko makali kwasababu ya maono; sina nguvu ndani yangu iliyosalia.
Et voici que quelqu'un de semblable aux fils des hommes toucha mes lèvres. J'ouvris alors la bouche, je parlai et je dis à celui qui se tenait devant moi: « Mon seigneur, à cause de la vision, mes douleurs m'ont envahi, et je n'ai plus de force.
17 Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu? Kwa kuwa sasa sina nguvu, na hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu.”
Car comment le serviteur de ce monseigneur pourrait-il parler avec ce monseigneur? Quant à moi, à l'instant même, je n'avais plus de force. Il n'y avait plus de souffle en moi. »
18 Tena yule mwenye mwonekano wa mtu alinigusa na kunitia nguvu.
Alors quelqu'un ayant l'apparence d'un homme me toucha de nouveau, et il me fortifia.
19 Alisema, “Usiogope, mtu ulithaminiwa sana. Amani na iwe kwako! Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu!” Na alipokuwa anaongea na mimi, nilipata nguvu. Nilimwambia, “Bwana wangu na aseme, kwa kuwa umenitia nguvu.”
Il dit: « Homme bien-aimé, n'aie pas peur. Que la paix soit avec toi. Sois fort. Oui, sois fort. » Quand il m'a parlé, j'ai été fortifié, et j'ai dit: « Laisse parler mon seigneur, car tu m'as fortifié. »
20 Aliniambia, “Je unajua ni kwanini nimekuja kwako? Nitarudi hivi karibuni kupigana na mkuu wa Uajemi. Na nitakapoenda, mkuu wa Ugiriki atakuja.
Puis il dit: « Savez-vous pourquoi je suis venu chez vous? Je vais maintenant retourner pour combattre le prince de Perse. Quand je sortirai, voici que viendra le prince de la Grèce.
21 Lakini nitakwambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli. Hakuna yeyote anayejionesha kuwa na nguvu pamoja nami dhidi yao, isipokuwa Mikaeli mkuu wenu.”
Mais je vais te dire ce qui est inscrit dans l'écriture de la vérité. Il n'y a personne qui tienne avec moi contre ceux-ci, sinon Michel, ton prince.

< Danieli 10 >