< Danieli 10 >

1 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza. Ujumbe huu ulikuwa ni wa kwelil. Ulihusu vita kuu. Danieli aliufahamu ujumbe alipopata ufumbuzi kutoka katika maono.
In the thridde yeer of the rewme of Sirus, kyng of Perseis, a word was schewid to Danyel, Balthasar bi name; and a trewe word, and greet strengthe, and he vndurstood the word; for whi vndurstondyng is nedeful in visioun.
2 Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa katika maombolezo kwa wiki tatu.
In tho daies Y, Danyel, mourenyde bi the daies of thre woukis;
3 Sikula chakula kizuri, sikula nyama, sikunywa divai, na sikujipaka mafuta mwenyewe mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzima.
Y eet not desirable breed, and fleisch, and wyn entride not into my mouth, but nethir Y was anoynted with oynement, til the daies of thre woukis weren fillid.
4 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa niko karibu na mto mkubwa (ambao ni Tigrisi),
Forsothe in the foure and twentithe dai of the firste monethe, Y was bisidis the greet flood, which is Tigris.
5 Nilitazama juu na nikamwona mtu aliyevaa kitani, akiwa na mkanda kiunoni mwake uliotengenezwa kwa dhahabu safi kutoka Ufazi.
And Y reiside myn iyen, and Y siy, and lo! o man was clothid with lynun clothis, and hise reynes weren gird with schynynge gold;
6 Mwili wake ulikuwa kama kito, na sura yake ilikuwa kama radi. Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi, na mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa. Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu.
and his bodi was as crisolitus, and his face was as the licnesse of leit, and hise iyen weren as a brennynge laumpe, and hise armes and tho thingis that weren bynethe til to the feet weren as the licnesse of bras beynge whijt, and the vois of hise wordis was as the vois of multitude.
7 Mimi, Danieli peke yangu niliyaona maono, na watu niliokuwa na pamoja hawakuyaona maono. Lakini, jambo kuu la kuogofya liliwaijia juu yao, na walikimbia na kujificha wao wenyewe.
Forsothe Y, Danyel, aloone siy the visioun; certis the men that weren with me, sien not, but ful greet ferdfulnesse felle yn on hem, and thei fledden in to an hid place.
8 Hivyo niliachwa peke yangu na niliyaona maono haya ajabu. Hakuna nguvu iliyobakia ndani yangu; mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu, na hazikubakia nguvu ndani yangu.
But Y was left aloone, and Y siy this greet visioun, and strengthe dwellide not in me; but also my licnesse was chaungid in me, and Y was stark, and Y hadde not in me ony thing of strengthis.
9 Kisha nikasikia maneno yake, na nilipoyasikia, nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito.
And Y herde the vois of hise wordis, and Y herde, and lay astonyed on my face, and my face cleuyde to the erthe.
10 Mkono ulinigusa, na ilinifanya nitetemeke katika magoti yangu na viganja vya mikono yangu.
And lo! an hond touchide me, and reiside me on my knees, and on the toes of my feet.
11 Malaika aliniambia, “Danieli, mtu aliyetunzwa sana, yafahamu maneno ninayokwambia wewe. Simama wima, kwa kuwa nimeshakutuma.” Na alipomaliza kuniambia ujumbe huu, nilisimama nikiwa natetemeka.
And he seide to me, Thou, Danyel, a man of desiris, vndurstonde the wordis whiche Y speke to thee, and stonde in thi degree; for now Y am sent to thee. And whanne he hadde seid this word to me, Y stood quakynge.
12 Kisha aliniambia, “Usiogope, Danieli. Tangu siku ya kwanza ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele ya Mungu, maneno yako yalisikiwa, na nimekuja kwasababu ya maneno yako.
And he seide to me, Danyel, nyle thou drede, for fro the firste dai in which thou settidist thin herte to vndurstonde, that thou schuldist turmente thee in the siyt of thi God, thi wordis weren herd, and Y cam for thi wordis.
13 Mwana wa mfalme wa ufalme wa Uajemi alinizuia, na niliwekwa huko na mfalme wa Uajemi kwa siku ishirini na moja. Lakini Mikaeli, mmoja kati ya wakuu alikuja kunisaidia.
Forsothe the prince of the rewme of Perseis ayenstood me oon and twenti daies, and lo! Myyhel, oon of the firste princes, cam in to myn help, and Y dwellide stille there bisidis the kyng of Perseis.
14 Sasa nimekuja kukusaidia ili ufahamu kile kitakachotokea kwa watu wako katika siku za mwisho. Kwa kuwa maono ni kwa ajili siku ambazo hazijatokea bado.
Forsothe Y am comun to teche thee, what thingis schulen come to thi puple in the laste daies; for yit the visioun is delaied in to daies.
15 Na alipokuwa akali akiniambia maneno haya, niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini na sikuwa na uwezo wa kuzungumza.
And whanne he spak to me bi siche wordis, Y castide doun my cheer to erthe, and was stille.
16 Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu alinigusa mdomo wangu na nifumbua kinywa changu na nilimwambia huyo aliyekuwa amesimam mbele yangu: “Bwana wangu, niko katika masumbuko makali kwasababu ya maono; sina nguvu ndani yangu iliyosalia.
And lo! as the licnesse of sone of man touchide my lippis; and Y openyde my mouth, and spak, and seide to hym that stood bifore me, My Lord, in thi siyt my ioynctis ben vnknit, and no thing of strengthis dwellide in me.
17 Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu? Kwa kuwa sasa sina nguvu, na hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu.”
And hou schal the seruaunt of my Lord mow speke with my Lord? no thing of strengthis dwellide in me, but also my breeth is closyde bitwixe.
18 Tena yule mwenye mwonekano wa mtu alinigusa na kunitia nguvu.
Therfor eft as the siyt of a man touchide me, and coumfortide me,
19 Alisema, “Usiogope, mtu ulithaminiwa sana. Amani na iwe kwako! Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu!” Na alipokuwa anaongea na mimi, nilipata nguvu. Nilimwambia, “Bwana wangu na aseme, kwa kuwa umenitia nguvu.”
and seide, Man of desiris, nyle thou drede; pees be to thee, be thou coumfortid, and be thou strong. And whanne he spak with me, Y wexide strong and seide, My Lord, speke thou, for thou hast coumfortid me.
20 Aliniambia, “Je unajua ni kwanini nimekuja kwako? Nitarudi hivi karibuni kupigana na mkuu wa Uajemi. Na nitakapoenda, mkuu wa Ugiriki atakuja.
And he seide, Whether thou woost not, whi Y cam to thee? And now Y schal turne ayen, to fiyte ayens the prince of Perseis. For whanne Y yede out, the prince of Grekis apperide comynge.
21 Lakini nitakwambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli. Hakuna yeyote anayejionesha kuwa na nguvu pamoja nami dhidi yao, isipokuwa Mikaeli mkuu wenu.”
Netheles Y schal telle to thee that, that is expressid in the scripture of treuthe; and noon is myn helpere in alle these thingis, no but Myyhel, youre prynce.

< Danieli 10 >