< Danieli 10 >

1 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza. Ujumbe huu ulikuwa ni wa kwelil. Ulihusu vita kuu. Danieli aliufahamu ujumbe alipopata ufumbuzi kutoka katika maono.
During the third year that Cyrus was the king of Persia, I Daniel, [who had been given the] name Belteshazzar, received [another] message [from God]. The message was true, but it was very difficult for me to understand it. But [later] I understood the message because of the vision that I had seen.
2 Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa katika maombolezo kwa wiki tatu.
At that time I had been sad for three weeks [about what had happened to Jerusalem].
3 Sikula chakula kizuri, sikula nyama, sikunywa divai, na sikujipaka mafuta mwenyewe mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzima.
I did not eat any tasty food or any meat or drink any wine. I did not even put any perfumed oil on my [face or hair] for those three weeks.
4 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa niko karibu na mto mkubwa (ambao ni Tigrisi),
[When those three weeks ended, ] on April 23, [my companions and] I were standing on the bank of the great Tigris River.
5 Nilitazama juu na nikamwona mtu aliyevaa kitani, akiwa na mkanda kiunoni mwake uliotengenezwa kwa dhahabu safi kutoka Ufazi.
I looked up and saw someone there who was wearing fine white/linen clothes and a belt [made of] pure gold.
6 Mwili wake ulikuwa kama kito, na sura yake ilikuwa kama radi. Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi, na mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa. Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu.
His body [shone] like a precious beryl stone. His face was as [bright as] a flash of lightning. His eyes [were/shone] like flaming torches. His arms and legs [shone] like polished bronze. And his voice was [very loud], like the roar of a huge crowd.
7 Mimi, Danieli peke yangu niliyaona maono, na watu niliokuwa na pamoja hawakuyaona maono. Lakini, jambo kuu la kuogofya liliwaijia juu yao, na walikimbia na kujificha wao wenyewe.
I, Daniel, was the only one who saw this vision. The men who were with me did not see anything, but [they sensed that someone was there, and they] became terrified. They ran away and hid themselves.
8 Hivyo niliachwa peke yangu na niliyaona maono haya ajabu. Hakuna nguvu iliyobakia ndani yangu; mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu, na hazikubakia nguvu ndani yangu.
So I was left there by myself, looking at this very unusual vision. I had no strength left. My face became very pale, with the result that no one would have recognized me.
9 Kisha nikasikia maneno yake, na nilipoyasikia, nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito.
I saw a man there, and when I heard him speak, I fell to the ground. I (fainted/became unconscious), [and I lay there] with my face on the ground.
10 Mkono ulinigusa, na ilinifanya nitetemeke katika magoti yangu na viganja vya mikono yangu.
Suddenly someone’s hand took hold of me and lifted me, with the result that I was on my hands and knees, [but I was still] trembling.
11 Malaika aliniambia, “Danieli, mtu aliyetunzwa sana, yafahamu maneno ninayokwambia wewe. Simama wima, kwa kuwa nimeshakutuma.” Na alipomaliza kuniambia ujumbe huu, nilisimama nikiwa natetemeka.
The man said to me, “Daniel, [God] loves you very much. Stand up and listen to what I am going to say to you, because [God] sent me to you.” When he said that, I stood up, [but I was still] trembling.
12 Kisha aliniambia, “Usiogope, Danieli. Tangu siku ya kwanza ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele ya Mungu, maneno yako yalisikiwa, na nimekuja kwasababu ya maneno yako.
Then he said to me, “Daniel, do not be afraid. God has heard what you have prayed ever since the first day that you determined to humble yourself in order to understand [the vision]. I have come to you because of what you prayed.
13 Mwana wa mfalme wa ufalme wa Uajemi alinizuia, na niliwekwa huko na mfalme wa Uajemi kwa siku ishirini na moja. Lakini Mikaeli, mmoja kati ya wakuu alikuja kunisaidia.
The [evil spirit who] rules the kingdom of Persia resisted/hindered me for 21 days, but Michael, who is one of God’s chief angels, came to help me. I left him there in Persia [to resist] that evil spirit who rules there.
14 Sasa nimekuja kukusaidia ili ufahamu kile kitakachotokea kwa watu wako katika siku za mwisho. Kwa kuwa maono ni kwa ajili siku ambazo hazijatokea bado.
I have come here to enable you to understand what will happen to the Israeli people in the future. [Do not forget that] the vision [that you saw] is about [things that will happen in] the distant future, [not about things that will happen very soon].”
15 Na alipokuwa akali akiniambia maneno haya, niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini na sikuwa na uwezo wa kuzungumza.
While he was saying that, I stared at the ground and was unable to say anything [because I was very afraid].
16 Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu alinigusa mdomo wangu na nifumbua kinywa changu na nilimwambia huyo aliyekuwa amesimam mbele yangu: “Bwana wangu, niko katika masumbuko makali kwasababu ya maono; sina nguvu ndani yangu iliyosalia.
Suddenly [the angel], who resembled a human, touched my lips. Then [I was able to speak, and] I said to him, “Sir, because [I have seen] this vision, I have become very weak, with the result that I cannot stop trembling.
17 Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu? Kwa kuwa sasa sina nguvu, na hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu.”
I am not able [RHQ] to talk to you, my master. I have no strength left, and it is very difficult for me to breathe.”
18 Tena yule mwenye mwonekano wa mtu alinigusa na kunitia nguvu.
But he took hold of me again, and enabled me to become stronger again.
19 Alisema, “Usiogope, mtu ulithaminiwa sana. Amani na iwe kwako! Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu!” Na alipokuwa anaongea na mimi, nilipata nguvu. Nilimwambia, “Bwana wangu na aseme, kwa kuwa umenitia nguvu.”
He said to me, “You human, God loves you very much. [So] do not be afraid. I desire/want things to go well for you and that you will be encouraged.” When he had said that, I felt even stronger, and I said, “Sir, tell me [what you want to tell me]. You have enabled me to feel stronger.”
20 Aliniambia, “Je unajua ni kwanini nimekuja kwako? Nitarudi hivi karibuni kupigana na mkuu wa Uajemi. Na nitakapoenda, mkuu wa Ugiriki atakuja.
Then he said, “(Do you know why I came to you?/I will tell you why I came to you.) [RHQ] It is to reveal to you what is written in the book which reveals/contains God’s truth. But now I must return to fight against [the evil spirit] who rules the kingdom of Persia. After I have defeated him, [the evil angel] who guards Greece will appear [and I must defeat him]. Michael, who guards you [Israeli people], will help me, but there is no one else to help me.”
21 Lakini nitakwambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli. Hakuna yeyote anayejionesha kuwa na nguvu pamoja nami dhidi yao, isipokuwa Mikaeli mkuu wenu.”

< Danieli 10 >