< Danieli 1 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja Yerusalemu na kuuzunguka mji ili kuzuia mahitaji yake yote.
In the thridde yeer of the rewme of Joachym, king of Juda, Nabugodonosor, the kyng of Babiloyne, cam to Jerusalem, and bisegide it.
2 Bwana alimpa Nebukadneza ushindi dhidi ya Yehoyakimu mfalme wa Yuda, na alimpatia vitu vitakatifu kutoka nyumba ya Mungu. Alivipeleka vitu hivyo mpaka katika nchi ya Babeli, kwa nyumba ya mungu wake, na aliviweka vitu vitakatifu katika hazina ya mungu wake.
And the Lord bitook in his hond Joachym, the kyng of Juda, and he took a part of the vessels of the hous of God; and he bar out tho in to the lond of Sennaar, in to the hous of his god, and he took the vessels in to the hous of tresour of his god.
3 Mfalme akamwambia Ashipenazi, afisa wake mkuu, awalete baadhi ya watu wa Israeli, wa familia ya kifalme na za kiungwana -
And the kyng seide to Asphaneth, souereyn of his onest seruauntis and chast, that he schulde brynge yn of the sones of Israel, and of the kyngis seed, and the children of tirauntis, in whiche weren no wem,
4 vijana wasio na hila, wenye mwonekano wa kuvutia, wenye ujuzi katika hekima yote, wenye kujawa na ufahamu na weledi, na wenye sifa za kutumika katika ikulu ya mfalme. Alitakiwa kuwafundisha maandiko na lugha ya Babeli.
faire in schap, and lerned in al wisdom, war in kunnyng, and tauyt in chastisyng, and that myyten stonde in the paleis of the kyng, that he schulde teche hem the lettris and langage of Caldeis.
5 Mfalme aliwatengea kwa ajili yao fungu kutoka katika chakula chake kizuri kwa kila siku na katika divai aliyokunywa. Vijana hawa walitakiwa kufunzwa kwa miaka mitatu, na baada ya hapo, wangeweza kumtumikia mfalme.
And the king ordeynede to hem lijflode bi ech dai of hise meetis, and of the wyn wherof he drank; that thei nurschid bi thre yeer, schulden stonde aftirward bifor the siyt of the kyng.
6 Miongoni mwao walikuwa ni Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria, baadhi ya watu wa Yuda.
Therfor Danyel, Ananye, Myzael, and Azarie, of the sones of Juda, weren among hem.
7 Afisa mkuu aliwapa majina: Danieli alimwita Belteshaza, Hanania alimwita Shadraka, Mishaeli alimwita Meshaki, na Azaria alimwita Abedinego.
And the souereyn of onest seruauntis and chast puttide to hem names; to Danyel he puttide Balthasar; to Ananye, Sidrach; to Mysael, Misach; and to Azarie, Abdenago.
8 Lakini Danieli alinuia katika akili yake kuwa asingejitia ujanisi mwenyewe kwa chakula kizuri cha mfalme wala kwa divai ambayo alikunywa.
Forsothe Danyel purposide in his herte, that he schulde not be defoulid of the boord of the kyng, nether of the wyn of his drink; and he preiede the souereyn of onest seruauntis and chast, that he schulde not be defoulid.
9 Basi, aliomba ruhusa kutoka kwa afisa mkuu ili kwamba asije akajitia uchafu yeye mwenyewe. Hivyo, Mungu alimpa Danieli kibali na huruma kupitia katika heshima ambayo afisa mkuu alikuwa nayo kwake.
Forsothe God yaf grace and merci to Daniel, in the siyt of the prince of onest seruauntis and chast.
10 Afisa mkuu alimwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme. Ameagiza aina ya chakula na vinywaji mnavyotakiwa kutumia. Kwa nini awaone ninyi mkiwa mnaonekana vibaya kuliko vijana wengine wa umri wenu? Mfalme aweza kukitwaa kichwa changu kwa sababu yenu.
And the prince of onest seruauntis and chast seide to Daniel, Y drede my lord the king, that ordeinede to you mete and drynk; and if he seeth youre faces lennere than othere yonge wexynge men, youre eueneeldis, ye schulen condempne myn heed to the kyng.
11 Kisha Daniel akamwambia msimamizi ambaye afisa mkuu alikuwa amemweka juu ya Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria.
And Danyel seide to Malazar, whom the prince of onest seruauntis and chast hadde ordeynede on Danyel, Ananye, Mysael, and Asarie,
12 Alisema, “Tafadhari tujaribuni, sisi watumishi wako kwa siku kumi. Tupatieni tu mboga mboga za kula na maji ya kunywa.
Y biseche, asaie thou vs thi seruauntis bi ten daies, and potagis be youun to vs to ete, and water to drynke; and biholde thou oure cheris,
13 Kisha ulinganishe mwonekano wetu na mwonekano wa vijana wanaokula vyakula vya mfalme, na mtutendee, sisi watu wako kulingana na kile unachokiona.”'
and the cheris of children that eten the kyngis mete; and as thou seest, so do thou with thi seruauntis.
14 Hivyo msimamizi alikubaliana naye kufanya hivi, na aliwajaribu kwa siku kumi.
And whanne he herde siche a word, he asaiede hem bi ten daies.
15 Katika mwisho wa siku kumi mwonekano wao ulikuwa ni wenye afya nzuri kuliko wa wale vijana waliokula vyakula vya kifalme.
Forsothe after ten daies the cheris of hem apperiden betere and fattere, than alle the children that eeten the kyngis mete.
16 Basi, msimamizi aliliondoa fungu lao la chakula na vivywaji vyao na walipewa mboga mboga tu.
Certis Malazar took the metis, and the wyn of the drynk of hem, and yaf to hem potagis.
17 Na kuhusu vijana hawa nne Mungu aliwapa uelewa na ufahamu katika maandiko yote na hekima, na Danieli aliweza kupambanua aina zote za maono na ndoto.
Forsothe to these children God yaf kunnyng and lernyng in ech book, and in al wisdom; but to Daniel God yaf vndurstondyng of alle visiouns and dremys.
18 Katika mwisho wa muda uliokuwa umepangwa na mfalme kuwaleta ndani, afisa mkuu aliwaleta mbele ya Nebukadneza.
Therfor whanne the daies weren fillid, aftir whiche the kyng seide, that thei schulden be brouyt yn, the souereyn of onest seruauntis and chast brouyte in hem, in the siyt of Nabugodonosor.
19 Mfalme aliongea nao, na miongoni mwa kundi lote hapo hapakuwa na wa kuwalinganisha na akina Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria. Walisimama mbele ya mfalme, wakiwa tayari kumtumikia.
And whanne the kyng hadde spoke to hem, siche weren not foundun of alle, as Daniel, Ananye, Misael, and Azarie; and thei stoden in the siyt of the king.
20 Katika kila swali la hekima na ufahamu ambalo mfalme aliwauliza, aliwakuta wakiwa na uwezo mara kumi kuliko waganga wote na wale waliojidai kusema na wafu, waliokuwa katika ufalme wake wote.
And ech word of wisdom and of vndurstondyng, which the king axide of hem, he foond in hem ten fold ouer alle false dyuynouris and astronomyens, that weren in al his rewme.
21 Danieli alikuwa hapo mpaka mwaka wa kwanza wa Mfalme Koreshi.
Forsothe Danyel was til to the firste yeer of king Cyrus.

< Danieli 1 >