< Wakolosai 4 >

1 Mabwana, toeni kwa watumwa mambo yaliyo haki na ya adili. Mnajua pia kwamba mnaye Bwana mbinguni.
Masters, give unto [your] servants that which is just and equal; knowing that ye also have a Master in heaven.
2 Endeleeni kuwa thabiti katika maombi. Kaeni macho katika hilo kwa shukrani.
Continue in prayer, and watch in the same with thanksgiving;
3 Ombeni pamoja kwa ajili yetu pia, ili kwamba Mungu afungue mlango kwa ajili ya neno, kunena siri ya ukweli ya Kristo. Kwa sababu ya hili nimefungwa minyororo.
Withal praying also for us, that God would open unto us a door of utterance, to speak the mystery of Christ, for which I am also in bonds:
4 Na ombeni kwamba niweze kuliweka wazi, kama inavyonipasa kusema.
That I may make it manifest, as I ought to speak.
5 Enenda kwa hekima kwa wale walioko nje, na muukomboe wakati.
Walk in wisdom toward them that are without, redeeming the time.
6 Maneno yenu na yawe na neema wakati wote, na yakolee chumvi majira yote, ili kwamba mweze kujua jinsi inavyowapasa kumjibu kila mtu.
Let your speech [be] alway with grace, seasoned with salt, that ye may know how ye ought to answer every man.
7 Kwa mambo yanayonihusu mimi, Tikiko atayafanya yajulikane kwenu. Yeye ni ndugu mpendwa, mtumishi mwaminifu, na mtumwa mwenzetu katika Bwana.
All my state shall Tychicus declare unto you, [who is] a beloved brother, and a faithful minister and fellowservant in the Lord:
8 Namtuma kwenu kwa ajili ya hili, kwamba mweze kujua mambo kuhusu sisi na pia kwamba aweze kuwatia moyo.
Whom I have sent unto you for the same purpose, that he might know your estate, and comfort your hearts;
9 Namtuma pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpendwa mwaminifu, na mmoja wenu. Watawaambia kila kitu kilichotokea hapa.
With Onesimus, a faithful and beloved brother, who is [one] of you. They shall make known unto you all things which [are done] here.
10 Aristarko, mfungwa mwenzangu, anawasalimu, pia na Marko binamu yake na Barnaba mliyepokea utaratibu kutoka kwake, “kama akija kwenu, mpokeeni,”
Aristarchus my fellowprisoner saluteth you, and Marcus, sister’s son to Barnabas, (touching whom ye received commandments: if he come unto you, receive him; )
11 Na pia Yesu aitwaye Yusto. Hawa peke yao wa tohara ni watendakazi wenzangu kwa jili ya ufalme wa Mungu. Wamekuwa ni faraja kwangu.
And Jesus, which is called Justus, who are of the circumcision. These only [are my] fellowworkers unto the kingdom of God, which have been a comfort unto me.
12 Epafra anawasalimu. Yeye ni mmoja wenu na mtumwa wa Kristo Yesu. Yeye hufanya bidii katika maombi kwa ajili, ili kwamba mweze kusimama kwa ukamilifu na kuhakishwa kikamilifu katika mapenzi yote ya Mungu.
Epaphras, who is [one] of you, a servant of Christ, saluteth you, always labouring fervently for you in prayers, that ye may stand perfect and complete in all the will of God.
13 Kwa kuwa ninamshuhudia, kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa hao walioko Laodekia, na kwa hao walioko Hierapoli.
For I bear him record, that he hath a great zeal for you, and them [that are] in Laodicea, and them in Hierapolis.
14 Luka yule tabibu mpendwa, na Dema wanawasalimu.
Luke, the beloved physician, and Demas, greet you.
15 Wasalimu ndugu zangu walioko Laodekia, na Nimfa, na kanisa lile lililoko nyumbani kwake.
Salute the brethren which are in Laodicea, and Nymphas, and the church which is in his house.
16 Barua hii itakapokuwa imesomwa miongoni mwenu, isomwe pia kwa kanisa la walaodekia, nanyi pia hakikisheni mnaisoma ile barua kutoka Laodekia.
And when this epistle is read among you, cause that it be read also in the church of the Laodiceans; and that ye likewise read the [epistle] from Laodicea.
17 Sema kwa Arkipo, ''Angalia ile huduma ambayo umeipokea katika Bwana, kwamba unapaswa kuitimiza.”
And say to Archippus, Take heed to the ministry which thou hast received in the Lord, that thou fulfil it.
18 Salamu hii ni kwa mkono wangu mwenyewe - Paulo. Ikuumbukeni minyororo yangu. Neema na iwe nanyi.
The salutation by the hand of me Paul. Remember my bonds. Grace [be] with you. Amen.

< Wakolosai 4 >