< Wakolosai 3 >
1 Ikiwa tena Mungu amewafufua pamoja na Kristo, yatafuteni mambo ya juu ambako Kristo anakaa mkono wa kuume wa Mungu.
Si vous êtes ressuscités avec Christ, cherchez les choses qui sont en haut, où Christ est assis à la droite de Dieu;
2 Fikirini kuhusu mambo ya juu, sio kuhusu mambo ya duniani.
attachez-vous aux choses d'en haut, et non à celles qui sont sur la terre;
3 Kwa kuwa mmekufa, na maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
car vous êtes morts, et votre vie est cachée avec Christ en Dieu.
4 Wakati Kristo atakapoonekana, ambaye ni maisha yenu, ndipo nanyi pia mtaonekana naye katika utukufu.
Lorsque Christ, qui est notre vie, paraîtra, vous aussi, vous paraîtrez avec lui dans la gloire.
5 Kwa hiyo yafisheni mambo yaliyo katika nchi yaani, zinaa, uchafu, shauku mbaya, nia mbaya, na tamaa, ambayo ni ibada ya sanamu.
Faites donc mourir vos membres, ces membres qui sont de la terre, le libertinage, l'impureté, la passion, les mauvais désirs et l’avarice, car elle est une idolâtrie.
6 Ni kwa ajili ya mambo haya ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wasio tii.
C'est là ce qui attire la colère de Dieu sur les hommes rebelles,
7 Ni kwa ajili ya mambo haya ninyi pia mlitembea kwayo mlipoishi kati yao.
parmi lesquels vous marchiez autrefois, quand vous viviez dans ces désordres:
8 Lakini sasa ni lazima myaondoe mambo haya yote. Yaani, ghadhabu, hasira, nia mbaya, matusi, na maneno machafu yatokayo vinywani mwenu.
mais aujourd'hui, rejetez toutes ces souillures, la colère, l'emportement, la méchanceté; que les injures et les paroles déshonnêtes soient bannies de votre bouche.
9 Msidanganyane ninyi kwa ninyi, kwa kuwa mmeuvua utu wenu wa kale na matendo yake.
N'usez point de mensonge les uns envers les autres,
10 Mmevaa utu mpya, ambao unafanywa upya katika maarifa kutokana mfano wa yule aliye muumba.
puisque vous avez dépouillé le vieil homme avec ses oeuvres, et revêtu l'homme nouveau, qui se renouvelle par la connaissance conformément à l'image de Celui qui l'a créé,
11 Katika maarifa haya, hakuna Myunani na Myahudi, kutahiriwa na kutokutahiriwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, asiye mtumwa, lakini badala yake Kristo ni mambo yote katika yote.
et cela, dans une sphère où il n'y a ni Grec ni Juif, ni circoncis ni incirconcis, ni barbare ni Scythe, ni esclave ni homme libre, mais où Christ est tout en tous.
12 Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Revêtez-vous donc, comme des élus de Dieu saints et bien-aimés, d'une tendresse compatissante, de bonté, d'humilité, de douceur, de longanimité,
13 Chukulianeni ninyi kwa ninyi. Hurumianeni kila mtu na mwenzake. Kama mtu analalamiko dhidi ya mwingine, amsamehe kwa jinsi ilele ambayo Bwana alivyo wasamehe ninyi.
vous supportant les uns les autres, et, si l'un a sujet de se plaindre de l'autre, vous pardonnant réciproquement: comme le Seigneur vous a pardonné, pardonnez- vous aussi.
14 Zaidi ya mambo haya yote, muwe na upendo, ambao ndio kigezo cha ukamilifu.
Surtout, revêtez-vous de charité, c'est le lien de la perfection.
15 Amani ya Kristo na iwaongoze mioyoni mwenu. Ilikuwa ni kwa ajili ya amani hii kwamba mliitiwa katika mwili mmoja. Iweni na shukrani.
Que la paix de Christ, à laquelle vous avez été appelés pour ne former qu'un seul et même corps, règne dans vos coeurs. Soyez reconnaissants.
16 Na Neno la Kristo likae ndani yenu kwa utajiri. Kwa hekima yote, fundishaneni na kushauriana ninyi kwa ninyi kwa Zaburi, nyimbo, na nyimbo za rohoni. Imbeni kwa shukrani mioyo yenu kwa Mungu.
Que la parole de Christ habite richement en vous, de sorte que vous vous instruisiez et que vous vous avertissiez les uns les autres en toute sagesse, et que vous chantiez à Dieu des psaumes, des hymnes, des cantiques spirituels, du fond de vos coeurs, avec reconnaissance.
17 Na chochote mfanyacho, katika maneno au katika matendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu. Mpeni shukrani Mungu baba kupitia Yeye.
Que tout ce que vous faites, paroles ou actes, que tout se fasse au nom du Seigneur Jésus en rendant grâces par lui à Dieu, notre Père.
18 Wake, wanyenyekeeni waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
Femmes, soyez soumises à vos maris comme cela se doit, selon le Seigneur.
19 Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali dhidi yao.
Maris, aimez vos femmes, et ne vous aigrissez point contre elles.
20 Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, maana ndivyo impendezavyo Bwana.
Enfants, obéissez en tout à vos pères et à vos mères, car c'est une chose agréable au Seigneur.
21 Akina baba msiwachokoze watoto wenu, ili kwamba wasije wakakata tamaa.
Pères, n'irritez pas vos enfants, afin qu'ils ne se découragent pas.
22 Watumwa, watiini mabwana zenu katika mwili kwa mambo yote, sio kwa huduma ya macho kama watu wa kufurahisha tu, bali kwa moyo wa kweli. Mwogopeni Mungu.
Esclaves, obéissez en tout à ceux qui sont vos maîtres selon la chair, non pas seulement lorsqu'ils ont l'oeil sur vous, comme gens cherchant à plaire aux hommes, mais avec droiture de coeur, comme gens craignant le Seigneur.
23 Chochote mfanyacho, fanyeni kutoka nafsini mwenu kama kwa Bwana na si kama kwa wanadamu.
Quoi que vous fassiez, acquittez-vous-en de bon coeur, comme pour le Seigneur, non pour les hommes,
24 Mnajua ya kwamba mtapokea tuzo ya umilkaji kutoka kwa Bwana. Ni Kristo Bwana mnayemtumikia.
sachant que vous recevrez du Seigneur l'héritage pour récompense. Vous êtes au service de Christ, le Seigneur:
25 Kwa sababu yeyote atendaye yasiyo haki atapokea hukumu kwa matendo yasiyo haki aliyoyafanya, na hakuna upendeleo.
celui qui commet l'injustice, recevra la rétribution du tort qu'il aura fait, et il n'y aura pas acception de personnes.