< Wakolosai 3 >

1 Ikiwa tena Mungu amewafufua pamoja na Kristo, yatafuteni mambo ya juu ambako Kristo anakaa mkono wa kuume wa Mungu.
Si donc vous avez été ressuscités avec le Christ, cherchez les choses d'en haut, où est le Christ, assis à la droite de Dieu.
2 Fikirini kuhusu mambo ya juu, sio kuhusu mambo ya duniani.
Fixez vos pensées sur les choses d'en haut, et non sur celles qui sont sur la terre.
3 Kwa kuwa mmekufa, na maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
Car vous êtes morts, et votre vie est cachée avec le Christ en Dieu.
4 Wakati Kristo atakapoonekana, ambaye ni maisha yenu, ndipo nanyi pia mtaonekana naye katika utukufu.
Quand le Christ, notre vie, paraîtra, vous paraîtrez aussi avec lui dans la gloire.
5 Kwa hiyo yafisheni mambo yaliyo katika nchi yaani, zinaa, uchafu, shauku mbaya, nia mbaya, na tamaa, ambayo ni ibada ya sanamu.
Faites donc mourir vos membres qui sont sur la terre: l'immoralité sexuelle, l'impureté, la passion dépravée, le mauvais désir, la cupidité, qui est une idolâtrie.
6 Ni kwa ajili ya mambo haya ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wasio tii.
C'est à cause de ces choses que la colère de Dieu vient sur les enfants de la désobéissance.
7 Ni kwa ajili ya mambo haya ninyi pia mlitembea kwayo mlipoishi kati yao.
Vous aussi, vous avez marché autrefois dans ces choses, quand vous viviez dans ces choses-là,
8 Lakini sasa ni lazima myaondoe mambo haya yote. Yaani, ghadhabu, hasira, nia mbaya, matusi, na maneno machafu yatokayo vinywani mwenu.
mais maintenant il faut les rejeter toutes: la colère, l'emportement, la malice, la calomnie, et les paroles honteuses qui sortent de votre bouche.
9 Msidanganyane ninyi kwa ninyi, kwa kuwa mmeuvua utu wenu wa kale na matendo yake.
Ne vous mentez pas les uns aux autres, puisque vous avez dépouillé le vieil homme et ses actions,
10 Mmevaa utu mpya, ambao unafanywa upya katika maarifa kutokana mfano wa yule aliye muumba.
et que vous avez revêtu l'homme nouveau, qui se renouvelle dans la connaissance, à l'image de son Créateur,
11 Katika maarifa haya, hakuna Myunani na Myahudi, kutahiriwa na kutokutahiriwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, asiye mtumwa, lakini badala yake Kristo ni mambo yote katika yote.
où il n'y a ni Grec ni Juif, ni circoncis ni incirconcis, ni barbare ni Scythe, ni esclave ni homme libre, mais où Christ est tout et en tous.
12 Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Revêtez-vous donc, comme des élus de Dieu, saints et bien-aimés, d'un cœur de compassion, de bonté, de modestie, d'humilité et de persévérance;
13 Chukulianeni ninyi kwa ninyi. Hurumianeni kila mtu na mwenzake. Kama mtu analalamiko dhidi ya mwingine, amsamehe kwa jinsi ilele ambayo Bwana alivyo wasamehe ninyi.
supportez-vous les uns les autres, et pardonnez-vous mutuellement, si quelqu'un a quelque chose à se reprocher; comme Christ vous a pardonné, faites-le vous aussi.
14 Zaidi ya mambo haya yote, muwe na upendo, ambao ndio kigezo cha ukamilifu.
Par-dessus toutes ces choses, marchez dans l'amour, qui est le lien de la perfection.
15 Amani ya Kristo na iwaongoze mioyoni mwenu. Ilikuwa ni kwa ajili ya amani hii kwamba mliitiwa katika mwili mmoja. Iweni na shukrani.
Et que la paix de Dieu règne dans vos cœurs, à laquelle vous avez aussi été appelés en un seul corps, et soyez reconnaissants.
16 Na Neno la Kristo likae ndani yenu kwa utajiri. Kwa hekima yote, fundishaneni na kushauriana ninyi kwa ninyi kwa Zaburi, nyimbo, na nyimbo za rohoni. Imbeni kwa shukrani mioyo yenu kwa Mungu.
Que la parole de Christ habite richement en vous; en toute sagesse, enseignez-vous et exhortez-vous les uns les autres par des psaumes, des hymnes et des chants spirituels, en chantant au Seigneur avec grâce dans votre cœur.
17 Na chochote mfanyacho, katika maneno au katika matendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu. Mpeni shukrani Mungu baba kupitia Yeye.
Quoi que vous fassiez, en paroles ou en actes, faites tout au nom du Seigneur Jésus, en rendant par lui des actions de grâces à Dieu le Père.
18 Wake, wanyenyekeeni waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
Femmes, soyez soumises à vos maris, comme il convient dans le Seigneur.
19 Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali dhidi yao.
Maris, aimez vos femmes, et ne vous aigrissez pas contre elles.
20 Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, maana ndivyo impendezavyo Bwana.
Enfants, obéissez en toutes choses à vos parents, car cela plaît au Seigneur.
21 Akina baba msiwachokoze watoto wenu, ili kwamba wasije wakakata tamaa.
Pères, ne provoquez pas vos enfants, afin qu'ils ne se découragent pas.
22 Watumwa, watiini mabwana zenu katika mwili kwa mambo yote, sio kwa huduma ya macho kama watu wa kufurahisha tu, bali kwa moyo wa kweli. Mwogopeni Mungu.
Serviteurs, obéissez en toutes choses à ceux qui sont vos maîtres selon la chair, non pas seulement quand ils regardent, comme pour plaire aux hommes, mais dans la simplicité du cœur, en craignant Dieu.
23 Chochote mfanyacho, fanyeni kutoka nafsini mwenu kama kwa Bwana na si kama kwa wanadamu.
Et quoi que vous fassiez, travaillez de bon cœur, comme pour le Seigneur et non pour des hommes,
24 Mnajua ya kwamba mtapokea tuzo ya umilkaji kutoka kwa Bwana. Ni Kristo Bwana mnayemtumikia.
sachant que vous recevrez du Seigneur la récompense de l'héritage; car vous servez le Seigneur Christ.
25 Kwa sababu yeyote atendaye yasiyo haki atapokea hukumu kwa matendo yasiyo haki aliyoyafanya, na hakuna upendeleo.
Mais celui qui fait le mal recevra de nouveau pour le mal qu'il a fait, et il n'y a pas de partialité.

< Wakolosai 3 >