< Wakolosai 3 >
1 Ikiwa tena Mungu amewafufua pamoja na Kristo, yatafuteni mambo ya juu ambako Kristo anakaa mkono wa kuume wa Mungu.
If then you were raised together with Meshikha, seek the things that are above, where Meshikha is, seated on the right hand of God.
2 Fikirini kuhusu mambo ya juu, sio kuhusu mambo ya duniani.
Set your mind on the things that are above, not on the things that are on the earth.
3 Kwa kuwa mmekufa, na maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
For you died, and your life is hidden with Meshikha in God.
4 Wakati Kristo atakapoonekana, ambaye ni maisha yenu, ndipo nanyi pia mtaonekana naye katika utukufu.
When Meshikha, your life, is revealed, then you will also be revealed with him in glory.
5 Kwa hiyo yafisheni mambo yaliyo katika nchi yaani, zinaa, uchafu, shauku mbaya, nia mbaya, na tamaa, ambayo ni ibada ya sanamu.
Put to death, therefore, whatever is worldly in you: sexual immorality, impurity, lust, evil desire, and covetousness, which is idolatry.
6 Ni kwa ajili ya mambo haya ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wasio tii.
Because of these, the wrath of God is coming on the children of disobedience.
7 Ni kwa ajili ya mambo haya ninyi pia mlitembea kwayo mlipoishi kati yao.
You also once walked in those, when you lived in them;
8 Lakini sasa ni lazima myaondoe mambo haya yote. Yaani, ghadhabu, hasira, nia mbaya, matusi, na maneno machafu yatokayo vinywani mwenu.
but now you also put them all away: anger, wrath, malice, slander, and shameful speaking out of your mouth.
9 Msidanganyane ninyi kwa ninyi, kwa kuwa mmeuvua utu wenu wa kale na matendo yake.
Do not lie to one another, seeing that you have put off the old self with its practices,
10 Mmevaa utu mpya, ambao unafanywa upya katika maarifa kutokana mfano wa yule aliye muumba.
and have put on the new self, who is being renewed in knowledge after the image of his Creator,
11 Katika maarifa haya, hakuna Myunani na Myahudi, kutahiriwa na kutokutahiriwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, asiye mtumwa, lakini badala yake Kristo ni mambo yote katika yote.
where there cannot be Greek and Jew, circumcision and uncircumcision, barbarian, Scythian, slave, freeman; but Meshikha is all, and in all.
12 Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Put on therefore, as God's chosen ones, holy and beloved, a heart of compassion, kindness, gentleness, humility, and patience;
13 Chukulianeni ninyi kwa ninyi. Hurumianeni kila mtu na mwenzake. Kama mtu analalamiko dhidi ya mwingine, amsamehe kwa jinsi ilele ambayo Bwana alivyo wasamehe ninyi.
bearing with one another, and forgiving each other, if anyone has a complaint against another; even as the Lord forgave you, so you also do.
14 Zaidi ya mambo haya yote, muwe na upendo, ambao ndio kigezo cha ukamilifu.
Above all these things, walk in love, which is the bond of perfection.
15 Amani ya Kristo na iwaongoze mioyoni mwenu. Ilikuwa ni kwa ajili ya amani hii kwamba mliitiwa katika mwili mmoja. Iweni na shukrani.
And let the peace of Meshikha rule in your hearts, to which also you were called in one body; and be thankful.
16 Na Neno la Kristo likae ndani yenu kwa utajiri. Kwa hekima yote, fundishaneni na kushauriana ninyi kwa ninyi kwa Zaburi, nyimbo, na nyimbo za rohoni. Imbeni kwa shukrani mioyo yenu kwa Mungu.
Let the word of Meshikha dwell in you richly; in all wisdom teaching and admonishing one another with psalms, hymns, and spiritual songs, singing with grace in your heart to God.
17 Na chochote mfanyacho, katika maneno au katika matendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu. Mpeni shukrani Mungu baba kupitia Yeye.
Whatever you do, in word or in deed, do all in the name of the Lord Yeshua, giving thanks to God the Father, through him.
18 Wake, wanyenyekeeni waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
Wives, be in subjection to your husbands, as is fitting in the Lord.
19 Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali dhidi yao.
Husbands, love your wives, and do not be bitter against them.
20 Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, maana ndivyo impendezavyo Bwana.
Children, obey your parents in all things, for this pleases the Lord.
21 Akina baba msiwachokoze watoto wenu, ili kwamba wasije wakakata tamaa.
Fathers, do not provoke your children, so that they won't be discouraged.
22 Watumwa, watiini mabwana zenu katika mwili kwa mambo yote, sio kwa huduma ya macho kama watu wa kufurahisha tu, bali kwa moyo wa kweli. Mwogopeni Mungu.
Servants, obey in all things those who are your masters according to the flesh, not just when they are looking, as people-pleasers, but in singleness of heart, fearing the Lord.
23 Chochote mfanyacho, fanyeni kutoka nafsini mwenu kama kwa Bwana na si kama kwa wanadamu.
And whatever you do, work heartily, as for the Lord, and not for people,
24 Mnajua ya kwamba mtapokea tuzo ya umilkaji kutoka kwa Bwana. Ni Kristo Bwana mnayemtumikia.
knowing that from the Lord you will receive the reward of the inheritance; for you serve the Lord Meshikha.
25 Kwa sababu yeyote atendaye yasiyo haki atapokea hukumu kwa matendo yasiyo haki aliyoyafanya, na hakuna upendeleo.
But he who does wrong will receive again for the wrong that he has done, and there is no partiality.