< Wakolosai 3 >
1 Ikiwa tena Mungu amewafufua pamoja na Kristo, yatafuteni mambo ya juu ambako Kristo anakaa mkono wa kuume wa Mungu.
Therefore, since you have been raised with Christ, strive for the things above, where Christ is seated at the right hand of God.
2 Fikirini kuhusu mambo ya juu, sio kuhusu mambo ya duniani.
Set your minds on things above, not on earthly things.
3 Kwa kuwa mmekufa, na maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
For you died, and your life is now hidden with Christ in God.
4 Wakati Kristo atakapoonekana, ambaye ni maisha yenu, ndipo nanyi pia mtaonekana naye katika utukufu.
When Christ, who is your life, appears, then you also will appear with Him in glory.
5 Kwa hiyo yafisheni mambo yaliyo katika nchi yaani, zinaa, uchafu, shauku mbaya, nia mbaya, na tamaa, ambayo ni ibada ya sanamu.
Put to death, therefore, the components of your earthly nature: sexual immorality, impurity, lust, evil desires, and greed, which is idolatry.
6 Ni kwa ajili ya mambo haya ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wasio tii.
Because of these, the wrath of God is coming on the sons of disobedience.
7 Ni kwa ajili ya mambo haya ninyi pia mlitembea kwayo mlipoishi kati yao.
When you lived among them, you also used to walk in these ways.
8 Lakini sasa ni lazima myaondoe mambo haya yote. Yaani, ghadhabu, hasira, nia mbaya, matusi, na maneno machafu yatokayo vinywani mwenu.
But now you must put aside all such things as these: anger, rage, malice, slander, and filthy language from your lips.
9 Msidanganyane ninyi kwa ninyi, kwa kuwa mmeuvua utu wenu wa kale na matendo yake.
Do not lie to one another, since you have taken off the old self with its practices,
10 Mmevaa utu mpya, ambao unafanywa upya katika maarifa kutokana mfano wa yule aliye muumba.
and have put on the new self, which is being renewed in knowledge in the image of its Creator.
11 Katika maarifa haya, hakuna Myunani na Myahudi, kutahiriwa na kutokutahiriwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, asiye mtumwa, lakini badala yake Kristo ni mambo yote katika yote.
Here there is no Greek or Jew, circumcised or uncircumcised, barbarian, Scythian, slave, or free, but Christ is all and is in all.
12 Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Therefore, as the elect of God, holy and beloved, clothe yourselves with hearts of compassion, kindness, humility, gentleness, and patience.
13 Chukulianeni ninyi kwa ninyi. Hurumianeni kila mtu na mwenzake. Kama mtu analalamiko dhidi ya mwingine, amsamehe kwa jinsi ilele ambayo Bwana alivyo wasamehe ninyi.
Bear with one another and forgive any complaint you may have against someone else. Forgive as the Lord forgave you.
14 Zaidi ya mambo haya yote, muwe na upendo, ambao ndio kigezo cha ukamilifu.
And over all these virtues put on love, which is the bond of perfect unity.
15 Amani ya Kristo na iwaongoze mioyoni mwenu. Ilikuwa ni kwa ajili ya amani hii kwamba mliitiwa katika mwili mmoja. Iweni na shukrani.
Let the peace of Christ rule in your hearts, for to this you were called as members of one body. And be thankful.
16 Na Neno la Kristo likae ndani yenu kwa utajiri. Kwa hekima yote, fundishaneni na kushauriana ninyi kwa ninyi kwa Zaburi, nyimbo, na nyimbo za rohoni. Imbeni kwa shukrani mioyo yenu kwa Mungu.
Let the word of Christ richly dwell within you as you teach and admonish one another with all wisdom, and as you sing psalms, hymns, and spiritual songs with gratitude in your hearts to God.
17 Na chochote mfanyacho, katika maneno au katika matendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu. Mpeni shukrani Mungu baba kupitia Yeye.
And whatever you do, in word or deed, do it all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God the Father through Him.
18 Wake, wanyenyekeeni waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
Wives, submit to your husbands, as is fitting in the Lord.
19 Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali dhidi yao.
Husbands, love your wives and do not be harsh with them.
20 Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, maana ndivyo impendezavyo Bwana.
Children, obey your parents in everything, for this is pleasing to the Lord.
21 Akina baba msiwachokoze watoto wenu, ili kwamba wasije wakakata tamaa.
Fathers, do not provoke your children, so they will not become discouraged.
22 Watumwa, watiini mabwana zenu katika mwili kwa mambo yote, sio kwa huduma ya macho kama watu wa kufurahisha tu, bali kwa moyo wa kweli. Mwogopeni Mungu.
Slaves, obey your earthly masters in everything, not only to please them while they are watching, but with sincerity of heart and fear of the Lord.
23 Chochote mfanyacho, fanyeni kutoka nafsini mwenu kama kwa Bwana na si kama kwa wanadamu.
Whatever you do, work at it with your whole being, for the Lord and not for men,
24 Mnajua ya kwamba mtapokea tuzo ya umilkaji kutoka kwa Bwana. Ni Kristo Bwana mnayemtumikia.
because you know that you will receive an inheritance from the Lord as your reward. It is the Lord Christ you are serving.
25 Kwa sababu yeyote atendaye yasiyo haki atapokea hukumu kwa matendo yasiyo haki aliyoyafanya, na hakuna upendeleo.
Whoever does wrong will be repaid for his wrong, and there is no favoritism.