< Wakolosai 2 >
1 Kwa kuwa nataka mfahamu jinsi ambavyo nimekuwa na taabu nyingi kwa ajili yenu, kwa wote walioko Laodikia na kwa wote ambao hawajaona uso wangu katika mwili.
PORQUE quiero que sepais cuan gran solicitud tengo por vosotros, y [por] los [que están] en Laodicéa, y [por] todos los que nunca vieron mi rostro en carne,
2 Nafanya kazi ili kwamba mioyo yao iweze kufarijiwa kwa kuletwa pamoja katika upendo na katika utajiri wote wa wingi wa uhakika kamili wa maarifa, katika kuijua siri ya kweli ya Mungu, ambaye ni Kristo.
Para que sean confortados sus corazones, unidos en amor, y en todas riquezas de cumplido entendimiento, para conocer el misterio de Dios, y del Padre, y de Cristo;
3 Katika Yeye hazina zote za hekima na maarifa zimefichwa.
En el cual están escondidos todos los tesoros de sabiduría y conocimiento.
4 Nasema hivi ili kwamba mtu yeyote asije akawafanyia hila kwa hotuba yenye ushawishi.
Y esto digo, para que nadie os engañe con palabras persuasivas.
5 Na ingawa sipo pamoja nanyi katika mwili, lakini nipo nanyi katika roho. Ninafurahi kuona utaratibu wenu mzuri na nguvu ya imani yenu katika Kristo.
Porque aunque estoy ausente con el cuerpo, no obstante con el espíritu estoy con vosotros, gozándome y mirando vuestro concierto, y la firmeza de vuestra fé en Cristo.
6 Kama mlivyompokea Kristo Bwana, tembeeni katika yeye.
Por tanto de la manera que habeis recibido al Señor Jesu-Cristo, andad en él:
7 Mwimarishwe katika yeye, mjengwe katika yeye, mwimarishwe katika imani kama tu mlivyofundishwa, na kufungwa katika shukrani nyingi.
Arraigados y sobreedificados en él, y confirmados en la fé, así como [lo] habeis aprendido, creciendo en ella con hacimiento de gracias.
8 Angalieni ya kwamba mtu yeyote asiwanase kwa falsafa na maneno matupu ya udanganyifu kulingana na mapokeo ya wanadamu, kulingana na kanuni za kidunia, na sio kulingana na Kristo.
Mirad que ninguno os engañe por filosofías, y vanas sutilezas, segun las tradiciones de los hombres, conforme á los elementos del mundo, y no segun Cristo.
9 Kwa kuwa katika yeye ukamilifu wote wa Mungu unaishi katika mwili.
Porque en él habita toda la plenitud de la Divinidad corporalmente:
10 Nanyi mmejazwa katika yeye. Yeye ni kichwa cha kila uweza na mamlaka.
Y en él estais cumplidos, el cual es la cabeza de todo principado y potestad:
11 Katika yeye pia mlitahiriwa kwa tohara isiyofanywa na wanadamu katika kuondolewa mwili wa nyama, lakini ni katika tohara ya Kristo.
En el cual tambien sois circuncidados de circuncision, no hecha con manos, con el despojamiento del cuerpo de los pecados de la carne en la circuncision de Cristo:
12 Mlizikwa pamoja naye katika ubatizo. Na kwa njia ya imani katika yeye mlifufuliwa kwa uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
Sepultados juntamente con él en el bautismo, en el cual tambien resucitasteis con [él, ] por la fe de la operacion de Dios que le levantó de los muertos.
13 Na mlipokuwa mmekufa katika makosa yenu na kutokutahiriwa kwa miili yenu, aliwafanya hai pamoja naye na kutusamehe makosa yetu yote.
Y á vosotros, estando muertos en pecados y [en] la incircuncision de vuestra carne, os vivifico juntamente con él, perdonándoos todos los pecados,
14 Alifuta kumbukumbu ya madeni iliyoandikwa, na taratibu zilizokuwa kinyume nasi. Aliiondoa yote na kuigongomea msalabani.
Rayendo la cédula de los ritos que nos era contraria, que era contra nosotros, quitándola de en medio y enclavándola en la cruz;
15 Aliziondoa nguvu na mamlaka. Aliyaweka wazi na kuyafanya kuwa sherehe ya ushidi kwa njia ya msalaba wake.
Y despojando los principados y las potestades, sacólos á la vergüenza en público, triunfando de ellos en sí mismo.
16 Kwa hiyo, mtu yeyote asiwahukumu ninyi katika kula au katika kunywa, au kuhusu siku ya sikukuu au mwezi mpya, au siku za Sabato.
Por tanto nadie os juzgue en comida, ó en bebida, ó en parte de dia de fiesta, ó de nueva luna, ó de Sábados:
17 Hivi ni vivuli vya mambo yajayo, lakini kiini ni Kristo.
Lo cual es la sombra de lo [que estaba] por venir; mas el cuerpo [es] de Cristo.
18 Mtu awaye yote asinyang'anywe tuzo yake kwa kutamani unyenyekevu na kwa kuabudu malaika. Mtu wa jinsi hiyo huingia katika mambo aliyoyaona na kushawishiwa na mawazo yake ya kimwili.
Nadie os prive de vuestro premio, afectando humildad y culto á los ángeles, metiéndose en lo que no ha visto, vanamente hinchado en el sentido de su propia carne,
19 Yeye hakishikilii kichwa. Ni kutoka katika kichwa kwamba mwili wote kupitia viungo vyake na mifupa huungwa na kushikamanishwa kwa pamoja; na hukua kwa ukuaji utolewao na Mungu.
Y no teniendo la Cabeza, de la cual todo el cuerpo, alimentado y conjunto por [sus] ligaduras y conjunturas, crece en aumento de Dios.
20 Ikiwa mlikufa pamoja na Kristo kwa tabia za dunia, mbona mnaishi kama mnawajibika kwa dunia:
Pues si sois muertos con Cristo cuanto á los rudimentos del mundo, ¿por qué, como si vivieseis al mundo, os someteis á ordenanzas,
21 “Msishike, wala kuonja, wala kugusa”?
[Tales como] no manejes, ni gustes, ni aun toques,
22 Haya yote yameamuriwa kwa ajili ya uharibifu ujao na matumizi, kutokana na maelekezo na mafundisho ya wanadamu.
(Las cuales cosas son todas para destruccion en el uso [mismo, ]) en conformidad á mandamientos y doctrinas de hombres?
23 Sheria hizi zina hekima ya dini zilizotengenezwa kwa ubinafsi na unyenyekevu na mateso ya mwili. Lakini hazina thamani dhidi ya tamaa za mwili.
Tales cosas tienen á la verdad cierta reputacion de sabiduría en culto voluntario, y humildad, y en duro trato del cuerpo; no en alguna honra para el saciar de la carne.