< Wakolosai 1 >

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu,
Paweł, apostoł Jezusa Chrystusa z woli Boga, i Tymoteusz, brat;
2 kwa waumini na ndugu waaminifu katika Kristo walioko Kolosai. Neema iwe kwenu, na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
Do świętych i wiernych braci w Chrystusie Jezusie, którzy są w Kolosach. Łaska wam i pokój od Boga, naszego Ojca, i od Pana Jezusa Chrystusa.
3 Tunatoa shukrani kwa Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, na tunawaombea mara kwa mara.
Dziękujemy Bogu i Ojcu naszego Pana Jezusa Chrystusa, nieustannie modląc się za was;
4 Tumesikia imani yenu katika Yesu Kristo na upendo mlionao kwa wale wote waliotengwa kwa ajili ya Mungu.
Odkąd usłyszeliśmy o waszej wierze w Chrystusa Jezusa i o miłości względem wszystkich świętych;
5 Mna upendo huu kwa sababu ya taraja la uhakika lililohifadhiwa mbinguni kwa ajili yenu. Mlisikia kuhusu taraja hiyo ya uhakika kabla katika neno la kweli, injili,
Z powodu nadziei odłożonej dla was w niebie. O niej to przedtem słyszeliście w słowie prawdy ewangelii;
6 ambayo imekuja kwenu. Injili hii inazaa tunda na inaenea ulimwenguni kote. Imekuwa ikifanya hivi ndani yenu pia tangu siku mlipoisikia na kujifunza kuhusu neema ya Mungu katika kweli.
Która dotarła do was, jak i na cały świat, i wydaje owoc, tak jak u was od dnia, w którym usłyszeliście i poznaliście łaskę Boga w prawdzie;
7 Hii ndiyo injili mliyojifunza kutoka kwa Epafra, mpendwa wetu mtumishi mwenzetu, ambaye ni mtumishi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
Jak też nauczyliście się od naszego umiłowanego współsługi Epafrasa, który jest wiernym sługą Chrystusa dla was;
8 Epafra ameufanya ujulikane kwetu upendo wenu katika Roho.
Który też oznajmił nam waszą miłość w Duchu.
9 Kwa sababu ya upendo huu, tangu siku tuliposikia hivi, hatujaacha kuwaombea. Tumekuwa tukiomba kwamba mtajazwa na maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa kiroho.
Dlatego i my od tego dnia, w którym [to] usłyszeliśmy, nie przestajemy za was się modlić i prosić, abyście byli napełnieni poznaniem jego woli we wszelkiej mądrości i duchowym zrozumieniu;
10 Tumekuwa tukiomba kwamba mtatembea kwa ustahimilivu wa Bwana katika njia zipendezazo. Tumekuwa tukiomba kwamba mtazaa tunda katika kila tendo jema na kwamba mtakua katika maarifa ya Mungu.
Abyście postępowali w sposób godny Pana, by podobać [mu] się we wszystkim, w każdym dobrym uczynku wydając owoc i wzrastając w poznawaniu Boga;
11 Tunaomba mweze kutiwa nguvu katika kila uwezo kulingana na nguvu za utukufu wake katika uvumilivu na ustahimilivu wote.
Umocnieni wszelką mocą według jego chwalebnej potęgi, ku wszelkiej cierpliwości i wytrwałości z radością;
12 Tunaomba kwamba, kwa furaha, mtatoa shukrani kwa Baba, aliyewafanya ninyi mweze kuwa na sehemu katika urithi wa waumini katika nuru.
Dziękując Ojcu, który nas uzdolnił do uczestnictwa w dziedzictwie świętych w światłości;
13 Ametuokoa kutoka katika utawala wa giza na kutuhamishia katika ufalme wa Mwana wake mpendwa.
Który nas wyrwał z mocy ciemności i przeniósł do królestwa swego umiłowanego Syna;
14 Katika Mwanae tuna ukombozi, msamaha wa dhambi.
W którym mamy odkupienie przez jego krew, przebaczenie grzechów.
15 Mwana ni mfano wa Mungu asiyeonekana. Ni mzaliwa wa kwanza wa uumbaji wote.
On jest obrazem Boga niewidzialnego [i] pierworodnym wszelkiego stworzenia.
16 Kwakuwa kwa yeye vitu vyote viliumbwa, vile vilivyoko mbinguni na vilivyoko duniani, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana. ikiwa ni vya enzi au mamlaka au utawala au wenye nguvu, vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
Przez niego bowiem wszystko zostało stworzone, to, co w niebie i [to, co] na ziemi, [to, co] widzialne i [co] niewidzialne, czy trony, czy panowania, czy zwierzchności, czy władze. Wszystko przez niego i dla niego zostało stworzone.
17 Yeye amekuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.
On jest przed wszystkim i wszystko istnieje dzięki niemu.
18 Na yeye ndiye kichwa cha mwili yaani kanisa, yeye ni mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka miongoni mwa wafu, hivyo, ana nafasi ya kwanza miongoni mwa vitu vyote.
On też jest głową ciała – kościoła; on jest początkiem [i] pierworodnym z umarłych, aby we wszystkim był pierwszy;
19 Kwa kuwa Mungu alipendezwa kwamba utimilifu wake wote uishi ndani yake,
Ponieważ upodobał sobie [Ojciec], aby w nim zamieszkała cała pełnia;
20 na kupatanisha vitu vyote kwake kwa njia ya Mwanawe. Mungu alifanya amani kupitia damu ya msalaba wake. Mungu alipatanisha vitu vyote kwake mwenyewe, ikiwa ni vitu vya duniani au vitu vya mbinguni.
I żeby przez niego pojednał wszystko ze sobą, czyniąc pokój przez krew jego krzyża; przez niego, [mówię], to, co jest na ziemi, jak i to, co jest w niebie.
21 Nanyi pia, kwa wakati mmoja mlikuwa wageni kwa Mungu na mlikuwa maadui wake katika akili na matendo maovu.
I was, którzy kiedyś byliście obcymi i wrogami umysłem w niegodziwych uczynkach, teraz pojednał;
22 Lakini sasa amewapatanisha ninyi kwa mwili wake kupitia kifo. Alifanya hivi ili kuwaleta ninyi watakatifu, wasio na lawama na bila dosari mbele yake,
W jego doczesnym ciele przez śmierć, aby was przedstawić [jako] świętych, nieskalanych i nienagannych przed swoim obliczem;
23 kama mkiendelea katika imani, mliyoimarishwa na kuwa thabiti, pasipo kuondoshwa mbali kutoka kwenye taraja la ujasiri la injili mliyoisikia. Hi ndiyo injili iliyotangazwa kwa kila mtu aliyeumbwa chini ya mbingu. Hii ndiyo injili ambayo kwayo mimi, Paulo, nimekuwa mtumishi.
Jeśli tylko trwacie w wierze, ugruntowani i utwierdzeni, niedający się odwieść od nadziei ewangelii, którą usłyszeliście, a która jest głoszona wszelkiemu stworzeniu pod niebem, której ja, Paweł, stałem się sługą;
24 Sasa nafurahia mateso yangu kwa ajili yenu. Nami natimiliza katika mwili wangu kinachopungua kwa mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
Teraz raduję się w swoich cierpieniach dla was i tego, czego z udręk Chrystusa brakuje w moim ciele, dopełniam dla jego ciała, którym jest kościół.
25 Mimi ni mtumishi wa kanisa hili, sawasawa na wajibu niliopewa kutoka kwa Mungu kwa ajili yenu, kulijaza neno la Mungu.
Jego sługą stałem się zgodnie z zarządzeniem Boga, danym mi dla was, abym wypełnił słowo Boże;
26 Huu ni ukweli wa siri iliyokuwa imefichwa kwa miaka mingi na kwa vizazi. Lakini sasa imefunuliwa kwa wote waaminio katika Yeye. (aiōn g165)
Tajemnicę, która była ukryta od wieków i pokoleń, ale teraz została objawiona jego świętym; (aiōn g165)
27 Ni kwa wale ambao Mungu alitaka kufunua kulivyo utajiri wa utukufu wa siri ya ukweli huu miongoni mwa Mataifa. Ni kwamba Kristo yumo ndani yenu, ujasiri wa utukufu ujao.
Którym Bóg zechciał oznajmić, jakie jest wśród pogan bogactwo chwały tej tajemnicy, którą jest Chrystus w was, nadzieja chwały.
28 Huyu ndiye tunayemtangaza. Tunamwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote, ili kwamba tumlete kila mtu mkamilifu katika Kristo.
Jego to głosimy, napominając każdego człowieka i nauczając każdego człowieka we wszelkiej mądrości, aby każdego człowieka przedstawić doskonałym w Chrystusie Jezusie.
29 Kwa jili hii, mimi najibidisha na kujitahidi kulingana na nguvu yake ifanyayo kazi ndani yangu katika uweza.
Nad tym też się trudzę, walcząc według jego mocy, która potężnie działa we mnie.

< Wakolosai 1 >