< Amosi 1 >

1 Haya ni mambo yanayoihusu Israeli ambayo Amosi, mmoja wa wachungaji katika Tekoa, aliyapokea katika ufunuo. Alipokea haya mambo katika siku za Uzia mfalme wa Yuda, na pia katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la aridhi.
Here is the message that was given to Amos, a shepherd from Tekoa in Judah. This is what he saw concerning Israel when Uzziah was king of Judah and Jeroboam, son of Jehoash, was king of Israel, two years before the earthquake.
2 Alisema, “Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu. Malisho ya wachungaji yatanyamaza kimya; kilele cha Karmeli kitanyauka.”
And he said, The Lord roars from Zion, he shouts from Jerusalem. The shepherds' pastures wither, the top of Mount Carmel dries up.
3 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Damaskasi, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya chuma.
This is what the Lord says: The people of Damascus have repeatedly sinned and so I will not hesitate to punish them, for they beat the people of Gilead with sharp iron threshing tools.
4 Nitapeleka moto kwenye nyumba ya Hazaeli, na utaiteketeza ngome za Ben Hadadi.
So I will send fire down on the house of Hazael and burn up Ben-Hadad's fortresses.
5 Nitazivunja komeo za Damaskasi na kumkatilia mbali mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni, na pia yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni. Na watu wa shamu watakwenda utumwani hata Kiri,” asema Yahwe.
I will smash the gates of Damascus, I will cut down those who live in the Valley of Aven, and the ruler from Beth Eden. The people of Aram will be deported as prisoners to the land of Kir, says the Lord.
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu waliwachukua mateka watu wote, kuwaweka juu ya mkono wa Edomu.
This is what the Lord says: The people of Gaza have repeatedly sinned and so I will not hesitate to punish them, for they sent into exile whole communities, handing them over to Edom.
7 Nitatuma moto kwenye kuta za Gaza, na kuziteketeza ngome zake.
So I will send down fire on the walls of Gaza and burn up its fortresses.
8 Nitamkatilia mbali yule mtu aishiye katika Ashdodi na mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, na mabaki ya Wafilisti wataangamia,” asema Bwana Yahwe.
I will cut down those who live in Ashdod and the ruler of Ashkelon. I will turn to punish Ekron and the Philistines who remain will die, says the Lord God.
9 Hivi ndivyo Yhawe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa nne, sintobadili adhabu, kwa sababu waliwapelekea watu wote wa Edomu, na wamevunja agano lao la undugu.
This is what the Lord says: The people of Tyre have repeatedly sinned and so I will not hesitate to punish them, for they exiled whole communities, handing them over to Edom, and did not keep their agreement to help each other as members of the same family.
10 Nitapeleka moto kwenye kuta za Tiro, nao utaziteketeza ngome zake.”
So I will send down fire on the walls of Tyre and burn up its fortresses.
11 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake kwa upanga na kutupilia mbali huruma zote. Hasira yake ikaendelea kuwa kali, na ghadhabu yake ikabaki milele.
This is what the Lord says: The people of Edom have repeatedly sinned and so I will not hesitate to punish them, for they hunted down the Israelites to whom they were related, killing them with swords. They attacked without mercy, tearing the Israelites to pieces in an angry rage that never stopped.
12 Nitapeleka moto juu ya Temani, na utaziteketeza nyumb a za kifalme za Bozra.”
So I will send down fire on Teman, and I will burn up the fortresses of Bozrah.
13 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za watu wa Amoni, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili waweze kupanua mipaka yao.
This is what the Lord says: The people of Ammon have repeatedly sinned and so I will not hesitate to punish them, because they ripped open pregnant women in Gilead as part of their war to enlarge their territory.
14 Nitawasha moto katika kuta za Raba, nao utaziteketeza nyumba za kifalme, pamoja na kupiga kelele katika siku ya vita, pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga.
I will set fire to the walls of Rabbah and burn up its fortresses. There will be shouts on the day of battle which will whirl with rage like a windstorm.
15 Mfalme wao ataenda utumwani, yeye na maafisa wake pamoja,” asema Yahwe.
Their king will be sent into exile together with his princes, says the Lord.

< Amosi 1 >