< Amosi 8 >
1 Hiki ndicho ambacho bwana Yahwe amenionyesha. Tazama, kikapu cha matunda ya hari!
Here, My Lord, Yahweh, gave me to see, —and lo! there was a basket of summer fruit.
2 Akasema, “Unaona nini, Amosi?” Nikasema, “Kikapu cha matunda ya hari.” Kisha Yahwe akanambia, “Mwisho umefika kwa watu wangu Israeli; sintowaumiza tena.
So then he said, What canst thou see, Amos? And I said, A basket of summer fruit. Then said Yahweh unto me, The end hath come unto my people Israel, I will not again any more forgive them;
3 Nyimbo za kwenye hekalu zitakuwa vilio. Katika siku hiyo-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe. Mizoga itakuwa mingi, katika kila sehemu wataitupa katika ukimya!”
but palace-songs, shall become howlings, in that day, Declareth My Lord, Yahweh, —Many shall be the dead bodies in every place—cast forth—[with a] hush!
4 Lisikilizeni hili, ninyi mkanyagao maskini na kumuondoa fukara wa nchi.
Hear this, ye who pant after the needy, and to make an end of the oppressed of the land:
5 wakisema, “Wakati mwezi mpya utakapoisha, hivyo tunaweza kuuza mazao tena? Wakati siku ya Sabato itakapoisha, ili kwamba tuuze ngano? Tutafanya kipimo kidogo na kuongeza bei, tukidanganya kwa mizani za udanganyifu.
Who say, When will the new moon, pass away, that we may sell corn? and the sabbath that we may open grain? who diminish the ephah, and increase the shekel, and who falsify by deceitful weights:
6 Hivi ndivyo ambavyo tunaweza kuuza ngano mbaya, kununua fukara kwa fedha, na masikini kwa jozi moja ya kubadhi.”
Who buy—for silver—the poor, and the needy for a pair of shoes, —and that the refuse of the grain we may sell.
7 Yahwe ameapa kwa fahari ya Yakobo, “Hakika sintoweza kusahau kazi zao hata moja.”
Sworn hath Yahweh, by the Excellency of Jacob, —Surely I will never forget any of their doings!
8 Je nchi haitatetemeka kwa hili, na kila mmoja aishiye kuombolezea? Yote hayo yatainuka kama Mto Naili, nayo itataabika juu na kupwa tena, kama mto wa Misri.
Is it not, for this, that the land, shall tremble? and shall mourn every inhabitant therein? Shall it not come up—like the Nile, all of it, and be tossed and subside like the river of Egypt?
9 “Itakuja siku ambayo -huu ndio usemi wa Bwana Yahwe- kwamba nitafanya jua litue wakati wa mchana, na nitaiweka giza dunia wakati wa mchana.
Yea it shall come to pass, in that day, Declareth My Lord, Yahweh, that I will cause the sun to go in at high noon, —and will darken the earth on a day of brightness!
10 Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo na nyimbo zenu zote kuwa masikitiko. Nitawafanya wote kuvaa nguo za magunia na kipara juu ya kila kichwa. Nitayafanya haya kama maombolezo kwa mwana pekee, na siku ya uchungu mwisho wake.
So will I turn your festivals into mourning, and all your songs into a dirge, and I will bring up—on all loins—sackcloth, and upon every head—baldness, —and I will make it like the mourning for an only one, even the afterpart thereof, as a day of bitterness.
11 Tazama, siku zinakuja -asema Bwana Yahwe- wakati nitakapoleta njaa katika nchi, sio njaa ya mkate, wala kiu ya maji, ila kusikia maneno ya Yahwe.
Lo! days are coming, Declareth My Lord, Yahweh, that I will send a hunger throughout the land, —not a hunger for food, nor a thirst for water, but for hearing the words of Yahweh;
12 watatangatanga kutoka bahari hata bahari; watakimbia kutoka kaskazini kwenda magharibi kutafuta neno la Yahwe, lakini hawatalipata.
Therefore shall men rove about—from sea to sea, and from the north even unto sunrise, —they shall run to and fro—seeking the word of Yahweh, but shall not find [it].
13 Katika siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kutokana na njaa.
In that day, shall the fair virgins and the choice young men faint for thirst.
14 Wale waapao kwa dhambi ya Samaria wataanguka na hawatainuka tena.”
They who swear by the Guilt of Samaria, and say, As thy God, liveth, O Dan! and, As the Way of Beer-sheba, liveth, shall fall, and shall not rise any more.