< Amosi 7 >
1 Hivi ndivyo ambavyo Bwana Yahwe alivyonionyesha. Tazama, aliumba kundi kubwa la nzige wakati wa kuchipuka kwa mmea, na, tazama, ulikuwa ni mmea wa mwisho baada ya mavuno ya mfalme.
The Lord God schewide these thingis to me; and lo! a makere of locust in bigynnyng of buriownynge thingis of euentid reyn, and lo! euentid reyn after the clippere of the kyng.
2 Wakati walipomaliza kula mbogamboga za nchi, kisha nikasema, “Bwana Yahwe, tafadhali nisamehe; Je Yakobo ataishije? kwa kuwa yeye ni mdogo sana.”
And it was don, whanne he hadde endid for to ete the erbe of erthe, Y seide, Lord God, Y biseche, be thou merciful; who schal reise Jacob, for he is litil?
3 Yahwe akapunguza hasira kuhusu hili. “Haitatokea,” akasema.
The Lord hadde merci on this thing; It schal not be, seide the Lord God.
4 Hivi ndivyo ambavyo Bwana Yahwe alivyonionyesha: Tazama, Bwana Yahwe aliita juu ya moto kuhukumu. Nao ukakausha sana, kilindi chini ya dunia na kutaka kuitekeza nchi, pia.
The Lord God schewide to me these thingis; and lo! the Lord God schal clepe doom to fier, and it schal deuoure myche depthe of watir, and it eet togidere a part.
5 Lakini nikasema, “Bwana Yahwe, acha tafadhali; Yakobo ataishije? Kwa kuwa yeye ni mdigo sana.”
And Y seide, Lord God, Y biseche, reste thou; who schal reise Jacob, for he is litil?
6 Yahwe akagairi kuhusiana na hili, “Hili halitajitokeza pia,” asema Bwana Yahwe.
The Lord hadde merci on this thing; But and this thing schal not be, seide the Lord God.
7 Hivi ndivyo ambavyo Yahwe alivyo nionyesha: Tazama, Bwana amesimama karibu na ukuta, pamoja na uzi wa timiza kwenye mkono wake.
The Lord God schewide to me these thingis; and lo! the Lord stondinge on a wal plastrid, and in the hond of hym was a trulle of a masoun.
8 Yahwe akanambia, “Amosi, unaona nini?” nikasema, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, nitaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli. Sintowaharibu tena.
And the Lord seide to me, What seest thou, Amos? And Y seide, A trulle of a masoun. And the Lord seide, Lo! I schal putte a trulle in the myddil of my puple Israel; Y schal no more putte to, for to ouerlede it;
9 Mahala pa juu pa Isaka pataharibiwa, patakatifu pa Israeli pataangamia, na nitainuka juu ya nyumba ya Yeroboamu kwa upanga.”
and the hiy thingis of idol schulen be distried, and the halewyngis of Israel schulen be desolat; and Y schal rise on the hous of Jeroboam bi swerd.
10 Kisha Amazia, yule kuhani wa Betheli, akatuma ujumbe kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli: “amosi amefanya njama dhidi yako katikati ya nyumba ya Israeli. Nchi haiwezi kubeba maneno yote haya.
And Amasie, prest of Bethel, sente to Jeroboam, kyng of Israel, and seide, Amos rebellide ayens thee, in the myddil of the hous of Israel; the lond mai not susteyne alle hise wordis.
11 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Amosi, 'Yeroboamu atakufa kwa upanga, na hakika Israeli itakwenda utumwani kutoka nchi yake.”'
For Amos seith these thingis, Jeroboam schal die bi swerd, and Israel caitif schal passe fro his lond.
12 Amazia akamwambia Amosi, “Mwonaji, nenda, kimbia irudie nchi ya Yuda, na hapo ule mkate na kutabiri.
And Amasie seide to Amos, Thou that seest, go; fle thou in to the lond of Juda, and ete thou there thi breed; and there thou schalt profesie.
13 Lakini usitabiri tena hapa katika Betheli, kwa kuwa ni patakatifu pa mfalme na nyumba ya kifalme.”
And thou schalt no more put to, that thou profesie in Bethel, for it is the halewyng of the king, and is the hous of the rewme.
14 Kisha Amosi akamwambia Amazia, “Mimi sio nabii wala mwana wa nabii. Mimi ni mchungaji wa mifugo, na mtunza mikuyu.
And Amos answeride, and seide to Amasie, Y am not a profete, and Y am not sone of profete; but an herde of neet Y am, drawyng vp sicomoris.
15 Lakini Yahwe akanichukua kutoka kuchunga mifugo na kunambia, 'Nenda, katabiri kwa watu wangu Israeli.'
And the Lord took me, whanne Y suede the floc; and the Lord seide to me, Go, and profesie thou to my puple Israel.
16 Sasa sikia neno la Yahwe. Wewe usemaye, 'Usitabiri juu ya Israeli, na usiongee juu ya nyumba ya Isaka.
And now here thou the word of the Lord. Thou seist, Thou schalt not profesie on Israel, and thou schal not droppe on the hous of idol.
17 Kwa hiyo hivi ndivyo Yahwe asemavyo, 'Mke wako atakuwa kahaba katika mji; wana wako waume na binti zako wataanguka kwa upanga; nchi yako itapimwa na kugawanywa; utakufa katika nchi najisi, na Israeli hakika itakwenda utumwani kutoka nchi yake.”'
For this thing the Lord seith these thingis, Thi wijf schal do fornicacioun in the citee, and thi sones and thi douytris schal falle bi swerd, and thi lond schal be motun with a litil coord; and thou schalt die in a pollutid lond, and Israel caitif schal passe fro his lond.