< Amosi 6 >

1 Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na kwa wale ambao wameokoka katika nchi ya mlima wa Samaria, watu mashuhuri bora wa mataifa, ambao nyumba ya Israeli huja kwa ajili ya msaada!
»Gorje tistim, ki so v udobju na Sionu in zaupajo v samarijsko goro, ki se imenujejo vodje narodov, h katerim je prihajala Izraelova hiša!
2 Viongozi wenu husema, “Pita kwenda Kalne na mkatazame; kutoka huko nendeni hadi Hamathi, mji mkubwa; kisha nendeni chini hata Gathi ya Wapelestina. Je ni wabora kuliko falme zenu mbili? Je kuna mpaka mkubwa kuliko mpaka wenu?”
Prečkajte v Kalne in poglejte in od tam pojdite v veliki Hamát. Potem pojdite dol v Gat Filistejcev. Mar so boljši kakor ta kraljestva? Je njihova meja večja kakor vaša meja?
3 Ole wao wale waiwekao siku ya majanga na kufanya ufalme kuwa kinyume kusogea karibu.
Vi, ki zli dan polagate daleč stran in sedežu nasilja naredite, da pride blizu,
4 Wamelala juu ya vitanda vya pembe na kupumzika juu ya viti vyao. Wakala wana kondoo kutoka kwenye kundi na ndama kutoka kwenye zizi.
ki ležite na posteljah iz slonovine in se iztegujete na svojih ležiščih in jeste jagnjeta iz tropa in teleta iz srede hleva,
5 Wanaimba nyimbo za kijinga kwenye muziki wa kinubi; wanatunga kwenye vyombo kama vya Daudi.
ki monotono pojete na zvok lire in si izmišljate glasbene instrumente, podobno kakor David;
6 Wanakunywa mvinyo kutoka kwenye bakuli na kujipaka mafuta wenyewe kwa mafuta ya marahamu, lakini hawahuzuniki juu ya mateso ya Yusufu.
ki pijete vino v skledicah in se mazilite z vodilnimi mazili. Toda niso užaloščeni zaradi Jožefove stiske.
7 Hivyo sasa watakwenda utumwani pamoja na watumwa wakwanza, na kelele za hao waliojinyoosha zitapita.
Zato bodo sedaj šli ujeti s prvimi, ki gredo ujeti in gostija tistih, ki so se iztegovali, bo odstranjena.
8 “Mimi Bwana Yahwe, nimeapa kwa nafsi yangu -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi, naizira fahari ya Yakobo; nachukia boma zake. Kwa hiyo nitautoa huo mji pamoja vyote vilivyomo humo.”
Gospod Bog je prisegel pri samem sebi, « govori Gospod, Bog nad bojevniki, »preziram odličnost Jakoba in sovražim njegove palače, zato bom izročil mesto, z vsem, kar je v njem.
9 Itakuja kuhusu kwamba kama kuna wanaume kumi waliobakia kwenye nyumba moja, watakufa.
In zgodilo se bo, če tam ostane deset ljudi v eni hiši, da bodo umrli.
10 Wakati ndugu wa mtu huyo atakapokuja kuchukua miili yao-yule ambaye awachomaye baada ya kuleta maiti katika nyumba-kama akisema kwa mtu katika nyumba, “Je kuna mtu yuko pamoja nawe?” Vipi kama yule akisema, “Hapana.” Kisha atasema, “Kaa kimya, kwa kuwa hatulitaja jina la Yahwe.”
In njegov stric ga bo vzdignil in tisti, ki ga sežiga, da odnese kosti iz hiše in rekel bo tistemu, ki je pri straneh hiše: › Je tam še kdo s teboj?‹ Ta pa bo rekel: ›Ne.‹ Potem bo rekel: ›Molči, kajti ne smemo omenjati Gospodovega imena.‹
11 Tazama, Yahwe atatoa amri, na nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande, na nyumba ndogo kuwa na nyufa.
Kajti glej, Gospod zapoveduje in veliko hišo bo udaril z vrzelmi in majhno hišo z razpokami.
12 Je farasi watakimbia juu ya mteremko wa miamba? Je mtu atalima huko na ng'ome? Bado mmegeuza haki kuwa sumu na tunda la haki kuwa uchungu.
Mar bodo konji tekli po skali? Ali bo tam kdo oral z voli? Kajti sodbo ste obrnili v žolč in sad pravičnosti v pikasti mišjak.
13 Ninyi mnaofurahia juu ya Lo Debari, msemao, “Je hatukuchukua Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
Vi, ki se veselite v ničevi stvari, ki pravite: ›Mar nismo s svojo lastno močjo k sebi vzeli rogov?‹
14 Lakini tazama, nitainua juu yenu taifa, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe, Mungu wa majeshi. Watawatesa ninyi kutoka Lebo Hamathi hata kijito cha Araba.”
Toda glejte, zoper vas bom dvignil narod, oh Izraelova hiša, « govori Gospod, Bog nad bojevniki, »in stiskali vas bodo od vstopanja v Hamát, do reke iz divjine.«

< Amosi 6 >