< Amosi 6 >

1 Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na kwa wale ambao wameokoka katika nchi ya mlima wa Samaria, watu mashuhuri bora wa mataifa, ambao nyumba ya Israeli huja kwa ajili ya msaada!
Woe to those who are at ease in Zion, and to those who are secure on the mountain of Samaria, the notable men of the foremost of nations, to whom the house of Israel come.
2 Viongozi wenu husema, “Pita kwenda Kalne na mkatazame; kutoka huko nendeni hadi Hamathi, mji mkubwa; kisha nendeni chini hata Gathi ya Wapelestina. Je ni wabora kuliko falme zenu mbili? Je kuna mpaka mkubwa kuliko mpaka wenu?”
Go to Calneh, and see; and from there go to Hamath the great; then go down to Gath of the Philistines. Are they better than these kingdoms? or is their border greater than your border?
3 Ole wao wale waiwekao siku ya majanga na kufanya ufalme kuwa kinyume kusogea karibu.
Those who put far away the evil day, and cause the seat of violence to come near;
4 Wamelala juu ya vitanda vya pembe na kupumzika juu ya viti vyao. Wakala wana kondoo kutoka kwenye kundi na ndama kutoka kwenye zizi.
Who lie on beds of ivory, and stretch themselves on their couches, and eat the lambs out of the flock, and the calves out of the midst of the stall;
5 Wanaimba nyimbo za kijinga kwenye muziki wa kinubi; wanatunga kwenye vyombo kama vya Daudi.
who strum on the strings of a harp; who invent for themselves instruments of music, like David;
6 Wanakunywa mvinyo kutoka kwenye bakuli na kujipaka mafuta wenyewe kwa mafuta ya marahamu, lakini hawahuzuniki juu ya mateso ya Yusufu.
who drink wine in bowls, and anoint themselves with the best oils; but they are not grieved for the affliction of Joseph.
7 Hivyo sasa watakwenda utumwani pamoja na watumwa wakwanza, na kelele za hao waliojinyoosha zitapita.
Therefore they will now go captive with the first who go captive; and the feasting and lounging will end.
8 “Mimi Bwana Yahwe, nimeapa kwa nafsi yangu -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi, naizira fahari ya Yakobo; nachukia boma zake. Kwa hiyo nitautoa huo mji pamoja vyote vilivyomo humo.”
"The LORD has sworn by himself," says the LORD, the God of hosts: "I abhor the pride of Jacob, and detest his fortresses. Therefore I will deliver up the city with all that is in it.
9 Itakuja kuhusu kwamba kama kuna wanaume kumi waliobakia kwenye nyumba moja, watakufa.
And it will be, if there remain ten men in one house, they will die, and the remaining ones will be left.
10 Wakati ndugu wa mtu huyo atakapokuja kuchukua miili yao-yule ambaye awachomaye baada ya kuleta maiti katika nyumba-kama akisema kwa mtu katika nyumba, “Je kuna mtu yuko pamoja nawe?” Vipi kama yule akisema, “Hapana.” Kisha atasema, “Kaa kimya, kwa kuwa hatulitaja jina la Yahwe.”
"When a man's relative carries him, even he who burns him, to bring bodies out of the house, and asks him who is in the innermost parts of the house, 'Is there yet any with you?' And he says, 'No;' then he will say, 'Hush. Indeed we must not mention the name of the LORD.'
11 Tazama, Yahwe atatoa amri, na nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande, na nyumba ndogo kuwa na nyufa.
"For, look, the LORD commands, and the great house will be smashed to pieces, and the little house into bits.
12 Je farasi watakimbia juu ya mteremko wa miamba? Je mtu atalima huko na ng'ome? Bado mmegeuza haki kuwa sumu na tunda la haki kuwa uchungu.
Do horses run on the rocky crags? Does one plow there with oxen? But you have turned justice into poison, and the fruit of righteousness into bitterness;
13 Ninyi mnaofurahia juu ya Lo Debari, msemao, “Je hatukuchukua Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
you who rejoice in Lo Debar, who say, 'Haven't we taken for ourselves Karnaim by our own strength?'
14 Lakini tazama, nitainua juu yenu taifa, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe, Mungu wa majeshi. Watawatesa ninyi kutoka Lebo Hamathi hata kijito cha Araba.”
For, look, I will raise up against you a nation, house of Israel," says the LORD, the God of hosts; "and they will afflict you from Lebo Hamath to the Wadi Arabah."

< Amosi 6 >