< Amosi 6 >
1 Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na kwa wale ambao wameokoka katika nchi ya mlima wa Samaria, watu mashuhuri bora wa mataifa, ambao nyumba ya Israeli huja kwa ajili ya msaada!
Woe to you that are wealthy in Sion, and to you that have confidence in the mountain of Samaria: ye great men, heads of the people, that go in with state into the house of Israel.
2 Viongozi wenu husema, “Pita kwenda Kalne na mkatazame; kutoka huko nendeni hadi Hamathi, mji mkubwa; kisha nendeni chini hata Gathi ya Wapelestina. Je ni wabora kuliko falme zenu mbili? Je kuna mpaka mkubwa kuliko mpaka wenu?”
Pass ye over to Chalane, and see, and go from thence into Emath the great: and go down into Geth of the Philistines, and to all the best kingdoms of these: if their border be larger than your border.
3 Ole wao wale waiwekao siku ya majanga na kufanya ufalme kuwa kinyume kusogea karibu.
You that are separated unto the evil day: and that approach to the throne of iniquity;
4 Wamelala juu ya vitanda vya pembe na kupumzika juu ya viti vyao. Wakala wana kondoo kutoka kwenye kundi na ndama kutoka kwenye zizi.
You that sleep upon beds of ivory, and are wanton on your couches: that eat the lambs out of the flock, and the calves out of the midst of the herd;
5 Wanaimba nyimbo za kijinga kwenye muziki wa kinubi; wanatunga kwenye vyombo kama vya Daudi.
You that sing to the sound of the psaltery: they have thought themselves to have instruments of music like David;
6 Wanakunywa mvinyo kutoka kwenye bakuli na kujipaka mafuta wenyewe kwa mafuta ya marahamu, lakini hawahuzuniki juu ya mateso ya Yusufu.
That drink wine in bowls, and anoint themselves with the best ointments: and they are not concerned for the affliction of Joseph.
7 Hivyo sasa watakwenda utumwani pamoja na watumwa wakwanza, na kelele za hao waliojinyoosha zitapita.
Wherefore now they shall go captive at the head of them that go into captivity: and the faction of the luxurious ones shall be taken away.
8 “Mimi Bwana Yahwe, nimeapa kwa nafsi yangu -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi, naizira fahari ya Yakobo; nachukia boma zake. Kwa hiyo nitautoa huo mji pamoja vyote vilivyomo humo.”
The Lord God hath sworn by his own soul, saith the Lord the God of hosts: I detest the pride of Jacob, and I hate his houses, and I will deliver up the city with the inhabitants thereof.
9 Itakuja kuhusu kwamba kama kuna wanaume kumi waliobakia kwenye nyumba moja, watakufa.
And if there remain ten men in one house, they also shall die.
10 Wakati ndugu wa mtu huyo atakapokuja kuchukua miili yao-yule ambaye awachomaye baada ya kuleta maiti katika nyumba-kama akisema kwa mtu katika nyumba, “Je kuna mtu yuko pamoja nawe?” Vipi kama yule akisema, “Hapana.” Kisha atasema, “Kaa kimya, kwa kuwa hatulitaja jina la Yahwe.”
And a man’s kinsman shall take him up, and shall burn him, that he may carry the bones out of the house; and he shall say to him that is in the inner rooms of the house: Is there yet any with thee? And he shall answer: There is an end. And he shall any to him: Hold thy peace, and mention not the name of the Lord.
11 Tazama, Yahwe atatoa amri, na nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande, na nyumba ndogo kuwa na nyufa.
For behold the Lord hath commanded, and he will strike the greater house with breaches, and the lesser house with clefts.
12 Je farasi watakimbia juu ya mteremko wa miamba? Je mtu atalima huko na ng'ome? Bado mmegeuza haki kuwa sumu na tunda la haki kuwa uchungu.
Can horses run upon the rocks, or can any one plough with buffles? for you have turned judgment into bitterness, and the fruit of justice into wormwood.
13 Ninyi mnaofurahia juu ya Lo Debari, msemao, “Je hatukuchukua Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
You that rejoice in a thing of nought: you that say: Have we not taken unto us horns by our own strength?
14 Lakini tazama, nitainua juu yenu taifa, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe, Mungu wa majeshi. Watawatesa ninyi kutoka Lebo Hamathi hata kijito cha Araba.”
But behold, I will raise up a nation against you, O house of Israel, saith the Lord the God of hosts; and they shall destroy you from the entrance of Emath, even to the torrent of the desert.