< Amosi 6 >

1 Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na kwa wale ambao wameokoka katika nchi ya mlima wa Samaria, watu mashuhuri bora wa mataifa, ambao nyumba ya Israeli huja kwa ajili ya msaada!
Sorrow to those who are resting in comfort in Zion, and to those who have no fear of danger in the mountain of Samaria, the noted men of the chief of the nations, to whom the people of Israel come!
2 Viongozi wenu husema, “Pita kwenda Kalne na mkatazame; kutoka huko nendeni hadi Hamathi, mji mkubwa; kisha nendeni chini hata Gathi ya Wapelestina. Je ni wabora kuliko falme zenu mbili? Je kuna mpaka mkubwa kuliko mpaka wenu?”
Go on to Calneh and see; and from there go to Hamath the great; then go down to Gath of the Philistines: are you better than these kingdoms? or is your land wider than theirs?
3 Ole wao wale waiwekao siku ya majanga na kufanya ufalme kuwa kinyume kusogea karibu.
You who put far away the evil day, causing the rule of the violent to come near;
4 Wamelala juu ya vitanda vya pembe na kupumzika juu ya viti vyao. Wakala wana kondoo kutoka kwenye kundi na ndama kutoka kwenye zizi.
Who are resting on beds of ivory, stretched out on soft seats, feasting on lambs from the flock and young oxen from the cattle-house;
5 Wanaimba nyimbo za kijinga kwenye muziki wa kinubi; wanatunga kwenye vyombo kama vya Daudi.
Making foolish songs to the sound of corded instruments, and designing for themselves instruments of music, like David;
6 Wanakunywa mvinyo kutoka kwenye bakuli na kujipaka mafuta wenyewe kwa mafuta ya marahamu, lakini hawahuzuniki juu ya mateso ya Yusufu.
Drinking wine in basins, rubbing themselves with the best oils; but they have no grief for the destruction of Joseph.
7 Hivyo sasa watakwenda utumwani pamoja na watumwa wakwanza, na kelele za hao waliojinyoosha zitapita.
So now they will go away prisoners with the first of those who are made prisoners, and the loud cry of those who were stretched out will come to an end.
8 “Mimi Bwana Yahwe, nimeapa kwa nafsi yangu -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi, naizira fahari ya Yakobo; nachukia boma zake. Kwa hiyo nitautoa huo mji pamoja vyote vilivyomo humo.”
The Lord God has taken an oath by himself, says the Lord, the God of armies: the pride of Jacob is disgusting to me, and I have hate for his great houses: so I will give up the town with everything in it.
9 Itakuja kuhusu kwamba kama kuna wanaume kumi waliobakia kwenye nyumba moja, watakufa.
Then it will come about that if there are still ten men in a house, death will overtake them.
10 Wakati ndugu wa mtu huyo atakapokuja kuchukua miili yao-yule ambaye awachomaye baada ya kuleta maiti katika nyumba-kama akisema kwa mtu katika nyumba, “Je kuna mtu yuko pamoja nawe?” Vipi kama yule akisema, “Hapana.” Kisha atasema, “Kaa kimya, kwa kuwa hatulitaja jina la Yahwe.”
And when a man's relation, even the one who is responsible for burning his body, lifting him up to take his bones out of the house, says to him who is in the inmost part of the house, Is there still anyone with you? and he says, No; then he will say, Keep quiet, for the name of the Lord may not be named.
11 Tazama, Yahwe atatoa amri, na nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande, na nyumba ndogo kuwa na nyufa.
For see, at the order of the Lord the great house will be full of cracks and the little house will be broken.
12 Je farasi watakimbia juu ya mteremko wa miamba? Je mtu atalima huko na ng'ome? Bado mmegeuza haki kuwa sumu na tunda la haki kuwa uchungu.
Is it possible for horses to go running on the rock? may the sea be ploughed with oxen? for the right to be turned by you into poison, and the fruit of righteousness into a bitter plant?
13 Ninyi mnaofurahia juu ya Lo Debari, msemao, “Je hatukuchukua Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
You whose joy is in a thing of no value, who say, Have we not taken for ourselves horns by the strength which is ours?
14 Lakini tazama, nitainua juu yenu taifa, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe, Mungu wa majeshi. Watawatesa ninyi kutoka Lebo Hamathi hata kijito cha Araba.”
For see, I will send against you a nation, O Israel, says the Lord, the God of armies, ruling you cruelly from the way into Hamath as far as the stream of the Arabah.

< Amosi 6 >