< Amosi 4 >

1 Lisikilizeni neno hili, ninyi ng'ombe wa Bashani, ninyi mliomo katika mlima wa Samaria, ninyi mnaowakandamiza maskini, ninyi mnaowaponda wahitaji, ninyi muwaambiao waume zenu, “Tuleteeni vinywaji.”
Listen to this message, you well-fed cows of Bashan who live on Mount Samaria, who oppress the poor and crush the needy, and who order your husbands, “Bring us drinks!”
2 Bwana Yahwe ameapa kwa utukufu wake, “Tazama, siku zitakuja kwenu wakati watakapowaondoa kwa ndoana, wa mwisho wenu na ndoana za kuvulia samaki.
The Lord God has sworn by his holiness: Watch out! For the time is coming when they will drag you away with hooks, each one of you will be like a fish on a hook.
3 Mtatoka kupitia mahali palipo bomolewa kwenye kuta za mji, kila mmoja wenu kwenda moja kwa moja kupitia hapo, na mtajitupa mbele ya Harmoni -hivi ndivyo asemavyo Yahwe.”
You will leave through breaches in the city walls, thrown out in the direction of Mount Hermon.
4 “Nendeni Betheli na uovu, hata Gilgali mkaongeza dhambi, leteni dhabihu zenu kila asubuhi, zaka zenu kila baada ya siku tatu.
Why don't you go to Bethel and sin? Go to Gilgal and add to your sins even more? Offer your sacrifices in the morning, bring your tithes after three days.
5 Toeni dhabihu za shukurani pamoja na mkate; tangazeni sadaka za hiari; watangazieni, kwa kuwa hii ndiyo iwapendezayo, ninyi watu wa Israeli -hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
Burn a thank offering of bread made with yeast, and announce what you're giving as freewill offerings so everyone will know. This is what you love to do! declares the Lord God.
6 Nawapatia usafi wa meno katika miji yenu na na kupungukiwa na mkate katika sehemu zenu zote. Bado hamkurudi kwangu -hivi ndivyo Yahwe asemavyo.
It was I who made sure you had nothing to eat in all your cities, and a lack of food wherever you lived, but still you wouldn't return to me, says the Lord.
7 Pia nimeizuia mvua kutoka kwenu wakati bado kulikuwa na miezi mitatu kwa mavuno. Nikaifanya inyeshe juu ya mji, na kuifanya isinyeshe katika mji mwingine. Kipande kimoja cha nchi ilinyesha, lakini kipande kingine cha nchi ambapo haikunyesha palikuwa pakavu.
It was I who kept the rain from falling when there was still three months before harvest. One city would have rain, while another would not. One field would have rain, another would dry up from lack of rain.
8 Walizunguka miji miwili au mitatu kwenda mji mwingine kunywa maji, lakini hawakutosheka. Bado hawakunirudia mimi -asema Yahwe.
People wandered from town to town looking for water, yet were still thirsty. But still you did not return to me, declares the Lord.
9 Nimewapiga kwa maradhi yanayosababisha kuvu. Wingi wa bustani, mashamba yenu ya zabibu, mitini yenu, na mizaituni-kuteketeza yote. Bado hamkunirudia hivi ndivyo Yahwe asemavyo.
I struck your many farms and vineyards with blight and mildew; locusts devoured your fig trees and olive trees. But still you did not return to me, declares the Lord.
10 Nimetuma tauni kwenu kama ya Misri. Nimewaua watoto wenu kwa upanga, kubeba farasi zenu, na kuufanya uvundo wa kambi zenu na kuingiza kwenye pua zenu. Bado hamkunirudia mimi -hivi ndivyo asemavyo Yahwe.
I sent a plague on you like I did in Egypt. I killed your young men in battle; I took away your horses; I made you smell the stench of dead bodies in your camps. But still you did not return to me, declares the Lord.
11 Nimeiangamiza miji miongoni mwenu, kama wakati Mungu alipoiangamiza Sodoma na Gomora. Mlikuwa kama kijinga kilichonyakuliwa kutoka kwenye moto. Bado hamkunirudia - asema Yahwe.
Some of you I destroyed as I destroyed Sodom and Gomorrah. You were like a burning stick pulled out of a fire. But still you did not return to me, declares the Lord.
12 Kwa hiyo nitafanya jambo baya kwako, Israeli; na kwa sababu nitafanya jambo baya kwako, jiandae kukutana na Mungu, Israeli!
Therefore, this is what I am going to do to you, Israel. Because I am going to do this, Israel, prepare to meet your God!
13 Kwa kuwa, tazama, yeye atangenezaye milima pia ndiye aumbaye upepo, humfunulia mawazo yake mwanadamu, hufanya asubuhi kuwa giza, na kupakanyaga mahala pa juu ya dunia. Yahwe, Mungu wa majeshi, ndilo jina lake.”
Watch! The One who made the mountains, who created the winds, who reveals his thoughts to humankind, who turns the sunlight into darkness, who walks on the high places of the earth—the Lord God of power is his name!

< Amosi 4 >