< Amosi 3 >

1 Sikieni neno la Yahwe aliloongea juu yenu, watu wa Israeli, juu ya familia nzima ambayo niliwatoa kutoka nchi ya Misri,
Listen to this message, Israelites, which the Lord has spoken against you, against the whole nation that I brought out of Egypt:
2 “Nimewachagua ninyi tu kutoka familia zote za dunia. Kwa hiyo nitawaadhibu kwa dhambi zenu zote.”
You alone have I cared for of all the nations of the world, this is why I will punish you for your crimes.
3 Je wawili wanaweza kutembea pamoja isipokuwa wamekubaliana?
Do two walk together unless they agreed to meet?
4 Je simba huunguruma msituni wakati hakuna mawindo? Je mwana simba ataunguruma kutoka pangoni mwake kama hajakamata kitu?
Does a lion roar in the forest when there is no prey for him? Does a young lion cry out in his den unless he has caught something?
5 Je ndege ataanguka kwenye mtego aridhini wakati hakuna chambo kimewekwa kwa ajili yake? Je mtego utafyatuka juu aridhini wakati hakuna kitu cha kukamata?
Does a bird swoop down into a trap if no bait is set for it? Does a trap spring up from the ground if nothing sets it off?
6 Je tarumbeta itapigwa mjini na watu wasitetemeke? Je janga laweza kuja mjini lisiyoletwa na Yahwe?
Can a trumpet be blown in a city and the people not tremble? Can disaster strike a city and the Lord not have caused it?
7 Hakika Bwna Yahwe hatafanya kitu vinginevyo amewafunulia mpango watumishi wake manabii.
Surely the Lord God does nothing without revealing his purpose to his servants the prophets.
8 Simba ameshaunguruma; nani hatoogopa? Bwana Yahwe amekwisha ongea; nani hatotabiri?
The lion has roared; who does not fear? The Lord God has spoken; who will not prophesy?
9 Tangaza hii katika ngome huko Ashdodi, na katika ngome za nchi ya Misri; sema, “Kusanyikeni kwenye milima ya Samaria na oneni vile mchafuko ulivyomkubwa kwake, na ukandamizaji uliopo katika yeye.
Proclaim over the palaces in Ashdod, and over the palaces in the land of Egypt: Gather upon the mountain of Samaria, and see the violent turmoil, the acts of oppression in her midst.
10 Kwa kuwa hawajui jinsi ya kufanya haki -hivi ndivyo Yahwe asemavyo- hao watunzao nguvu na uharibifu katika ngome zao.”
For they do not know how to do right. They are heaping up violence and oppression in their palaces, says the Lord.
11 Kwa hiyo, hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Adui ataizunguka nchi. Atazivuta chini nguvu zako na ngome zenu zitatekwa nyara.”
Therefore the Lord God says: An enemy will surround the land, he will strip your strength from you. and your palaces will be looted.
12 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo,” Kama mchungaji aokoavyo miguu miwili tu kwenye mdomo wa simba, au kipande cha sikio, ndivyo wana wa Israeli watakavyookolewa wale waishio katika Samaria, pamoja na pembe ya kulalia, au pembe ya kitanda.”
The Lord says: Just as a shepherd rescues from the jaws of a lion two shinbones or a piece of an ear, so the Israelites living in Sameria will be rescued – with the corner of a couch, and the damask of a divan!
13 Sikieni na kushudia juu ya nyumba ya Yakobo -hivi ndivyo Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi,
Listen and testify against the house of Jacob, says the Lord God, the God of hosts.
14 “Kwa kuwa katika siku ambayo nimeadhibu dhambi za Israeli, pia nitaziadhibu madhabahu za Betheli. Pembe za madhabahu zitakatwa na kuanguka chini.
On the day when I punish Israel for their crimes, I will also visit in judgment the altars of Bethel, the horns of the altar will be hacked off, and they will fall to the ground.
15 Nitaiharibu nyumba ya baridi pamoja na nyumba ya hari. Nyumba za pembe zitaangamia, na nyumba kubwa zitatoweka, -hivi ndivyo Yahwe asemavyo.”
I will destroy the winter houses together with the summer houses and the houses of ivory will perish. Many great houses will be swept away, says the Lord.

< Amosi 3 >