< Amosi 3 >
1 Sikieni neno la Yahwe aliloongea juu yenu, watu wa Israeli, juu ya familia nzima ambayo niliwatoa kutoka nchi ya Misri,
Give ear to this word which the Lord has said against you, O children of Israel, against all the family which I took up out of the land of Egypt, saying,
2 “Nimewachagua ninyi tu kutoka familia zote za dunia. Kwa hiyo nitawaadhibu kwa dhambi zenu zote.”
You only of all the families of the earth have I taken care of: for this reason I will send punishment on you for all your sins.
3 Je wawili wanaweza kutembea pamoja isipokuwa wamekubaliana?
Is it possible for two to go walking together, if not by agreement?
4 Je simba huunguruma msituni wakati hakuna mawindo? Je mwana simba ataunguruma kutoka pangoni mwake kama hajakamata kitu?
Will a lion give his loud cry in the woodland when no food is there? will the voice of the young lion be sounding from his hole if he has taken nothing?
5 Je ndege ataanguka kwenye mtego aridhini wakati hakuna chambo kimewekwa kwa ajili yake? Je mtego utafyatuka juu aridhini wakati hakuna kitu cha kukamata?
Is it possible for a bird to be taken in a net on the earth where no net has been put for him? will the net come up from the earth if it has taken nothing at all?
6 Je tarumbeta itapigwa mjini na watu wasitetemeke? Je janga laweza kuja mjini lisiyoletwa na Yahwe?
If the horn is sounded in the town will the people not be full of fear? will evil come on a town if the Lord has not done it?
7 Hakika Bwna Yahwe hatafanya kitu vinginevyo amewafunulia mpango watumishi wake manabii.
Certainly the Lord will do nothing without making clear his secret to his servants, the prophets.
8 Simba ameshaunguruma; nani hatoogopa? Bwana Yahwe amekwisha ongea; nani hatotabiri?
The cry of the lion is sounding; who will not have fear? The Lord God has said the word; is it possible for the prophet to keep quiet?
9 Tangaza hii katika ngome huko Ashdodi, na katika ngome za nchi ya Misri; sema, “Kusanyikeni kwenye milima ya Samaria na oneni vile mchafuko ulivyomkubwa kwake, na ukandamizaji uliopo katika yeye.
Give out the news in the great houses of Assyria and in the land of Egypt, and say, Come together on the mountains of Samaria, and see what great outcries are there, and what cruel acts are done in it.
10 Kwa kuwa hawajui jinsi ya kufanya haki -hivi ndivyo Yahwe asemavyo- hao watunzao nguvu na uharibifu katika ngome zao.”
For they have no knowledge of how to do what is right, says the Lord, who are storing up violent acts and destruction in their great houses.
11 Kwa hiyo, hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Adui ataizunguka nchi. Atazivuta chini nguvu zako na ngome zenu zitatekwa nyara.”
For this reason, says the Lord, an attacker will come, shutting in the land on every side; and your strength will come down and your great houses will be made waste.
12 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo,” Kama mchungaji aokoavyo miguu miwili tu kwenye mdomo wa simba, au kipande cha sikio, ndivyo wana wa Israeli watakavyookolewa wale waishio katika Samaria, pamoja na pembe ya kulalia, au pembe ya kitanda.”
These are the words of the Lord: As the keeper of sheep takes out of the mouth of the lion two legs or part of an ear; so will the children of Israel be made safe, who are resting in Samaria on seats of honour or on the silk cushions of a bed.
13 Sikieni na kushudia juu ya nyumba ya Yakobo -hivi ndivyo Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi,
Give ear now, and give witness against the family of Jacob, says the Lord God, the God of armies;
14 “Kwa kuwa katika siku ambayo nimeadhibu dhambi za Israeli, pia nitaziadhibu madhabahu za Betheli. Pembe za madhabahu zitakatwa na kuanguka chini.
For in the day when I give Israel punishment for his sins, I will send punishment on the altars of Beth-el, and the horns of the altar will be cut off and come down to the earth.
15 Nitaiharibu nyumba ya baridi pamoja na nyumba ya hari. Nyumba za pembe zitaangamia, na nyumba kubwa zitatoweka, -hivi ndivyo Yahwe asemavyo.”
And I will send destruction on the winter house with the summer house; the ivory houses will be falling down and the great houses will come to an end, says the Lord.