< Amosi 2 >

1 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Moabu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu amechoma moto mifupa ya mfalme wa Edomu hadi kuwa chokaa.
The Lord says: For Moab’s three crimes – no, four! – I will not rescind my judgment. They have burned to lime the bones of the king of Edom,
2 Nitatuma moto juu ya Moabu, na utaangamiza ngome za Keriothi. Moabu atakufa katika gasia, pamoja na kelele na sauti ya tarumbeta.
to desecrate the dead. So I will send a fire into Moab. It will devour the palaces of Kirioth, with a war-cry, with the sound of trumpets.
3 Nitamuharibu mwamuzi kati yake, na nitawaua wana wa mfalme pamoja na yeye,” asema Yahwe.
I will kill the ruler, all his nobles I will slay with him, says the Lord.
4 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Yuda, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameikataa sheria ya Yahwe na hawakuzishika amri zake. Uongo wao umesababisha kupotea, ambao baba zao pia waliufuata.
The Lord says: For Judah’s three crimes – no, four! – I will not rescind my judgment. They have rejected the law of the Lord and have not kept his statutes. Instead their false gods their ancestors followed, have led them astray.
5 Nitatuma moto juu ya Yuda, na utaimeza ngome ya Yerusalemu.”
So I will send a fire on Judah. It will devour the palaces of Jerusalem.
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Israeli, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewauza wasio na hatia kwa fedha na maskini kwa jozi moja ya makubadhi.
The Lord says: For Israel’s three crimes – no, four! – I will not rescind my judgment. They sell the righteous for money, the needy for a pair of shoes.
7 Nao hukanyaga juu ya vichwa vya maskini kama kukanyaga kwenye mavumbi juu ya aridhi; wanasukuma kukandamiza. Mtu mmoja na baba yake walilala na msichana mmoja na hivyo kukufuru jina langu takatifu.
They trample on the head of the poor, push the humble out of the way. Father and son go to the same temple girl, and so profane my holy name.
8 Nao hulala chini karibu na kila madhabahu kwenye nguo zilizowekwa dhamana, na katika nyumba ya Mungu wao hunywa divai ya wale ambao walitozwa faini.
They stretch themselves on garments taken in pledges beside every altar, and they drink the wine of those who have been fined in the house of their God.
9 Bado nimemwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi; alikuwa na nguvu kama mialoni. Kisha nikaharibu matunda yake juu na mizizi yake chini.
It was I who destroyed the Amorites for your sake, whose height was like that of the cedars, as strong as oaks. I destroyed their fruit from above and their roots from below.
10 Pia, niliwapandisha kutoka nchi ya Misri na kuwaongoza miaka arobaini nyikani ili mmiliki nchi ya Wamori.
It was I who brought you up from the land of Egypt, led you forty years in the wilderness, brought you here to possess the land of the Amorites.
11 Nimewainua manabii kutoka miongoni mwa watoto wanu wawe Wanadhiri kutoka vijana wenu. Je sio hivyo, watu wa Israeli? -hivi ndivyo Yahwe asemavyo.
I raised up some of your sons to be prophets some of your youths to be Nazirites. Is not this indeed so, Israelites? says the Lord.
12 Lakini mmewashawishi Wanadhiri kunywa mvinyo na kuwaamuru manabii wasifanye unabii.
But you made the Nazirites drink wine and banned the prophets from prophesying.
13 Tazama, nitawakanyaga kama mkokoteni uliojaa miganda inayoweza kumkanyaga mtu.
Listen! It is I who will make you groan in your places, as a wagon groans under its load of grain.
14 Mtu akimbiaye hatapata kimbilio; mwenye nguvu hatoongeza nguvu zake mwenyewe; wala shujaa kujiokoa mwenyewe.
Then flight will fail the swift, and the strength of the strongest will be useless. The warrior will not save his life,
15 Apindaye upinde hatasimama; mkimbiaji sana hatakimbia; mwendesha farasi hatajiokoa mwenyewe.
the archer will not stand firm, the swift of foot will not escape, the horseman will not save his life.
16 Hata wapiganaji shujaa watakimbia uchi katika siku hiyo -hivi ndivyo Yahwe asemavy.”
The bravest of warriors will flee away naked in that day, says the Lord.

< Amosi 2 >