< Amosi 2 >
1 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Moabu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu amechoma moto mifupa ya mfalme wa Edomu hadi kuwa chokaa.
Thus said YHWH: “For three transgressions of Moab, And for four, I do not reverse it, Because of his burning the bones of the king of Edom to lime,
2 Nitatuma moto juu ya Moabu, na utaangamiza ngome za Keriothi. Moabu atakufa katika gasia, pamoja na kelele na sauti ya tarumbeta.
And I have sent a fire against Moab, And it has consumed the palaces of Kerioth, And Moab is dying with noise, With shouting, with voice of a horn.
3 Nitamuharibu mwamuzi kati yake, na nitawaua wana wa mfalme pamoja na yeye,” asema Yahwe.
And I have cut off judge from her midst, And I slay all its heads with him,” said YHWH.
4 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Yuda, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameikataa sheria ya Yahwe na hawakuzishika amri zake. Uongo wao umesababisha kupotea, ambao baba zao pia waliufuata.
Thus said YHWH: “For three transgressions of Judah, And for four, I do not reverse it, Because of their loathing the Law of YHWH, And His statutes they have not kept, And their lies cause them to err, After which their fathers walked,
5 Nitatuma moto juu ya Yuda, na utaimeza ngome ya Yerusalemu.”
And I have sent a fire against Judah, And it has consumed palaces of Jerusalem.”
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Israeli, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewauza wasio na hatia kwa fedha na maskini kwa jozi moja ya makubadhi.
Thus said YHWH: “For three transgressions of Israel, And for four, I do not reverse it, Because of their selling the righteous for silver, And the needy for a pair of sandals.
7 Nao hukanyaga juu ya vichwa vya maskini kama kukanyaga kwenye mavumbi juu ya aridhi; wanasukuma kukandamiza. Mtu mmoja na baba yake walilala na msichana mmoja na hivyo kukufuru jina langu takatifu.
Who are panting for the dust of the earth on the head of the poor, And the way of the humble they turn aside, And a man and his father go to the girl, So as to defile My holy Name.
8 Nao hulala chini karibu na kila madhabahu kwenye nguo zilizowekwa dhamana, na katika nyumba ya Mungu wao hunywa divai ya wale ambao walitozwa faini.
And they stretch themselves on pledged garments near every altar, And the wine of fined ones they drink [in] the house of their gods.
9 Bado nimemwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi; alikuwa na nguvu kama mialoni. Kisha nikaharibu matunda yake juu na mizizi yake chini.
And I have destroyed the Amorite from before them, Whose height [is] as the height of cedars, And he [is] strong as the oaks, And I destroy his fruit from above, And his roots from beneath.
10 Pia, niliwapandisha kutoka nchi ya Misri na kuwaongoza miaka arobaini nyikani ili mmiliki nchi ya Wamori.
And I have brought you up from the land of Egypt, And cause you to go in a wilderness forty years, To possess the land of the Amorite.
11 Nimewainua manabii kutoka miongoni mwa watoto wanu wawe Wanadhiri kutoka vijana wenu. Je sio hivyo, watu wa Israeli? -hivi ndivyo Yahwe asemavyo.
And I raise of your sons for prophets, And of your choice ones for Nazarites, Is this not true, O sons of Israel?” A declaration of YHWH.
12 Lakini mmewashawishi Wanadhiri kunywa mvinyo na kuwaamuru manabii wasifanye unabii.
“And you cause the Nazarites to drink wine, And on the prophets you have laid a charge, Saying, Do not prophesy!
13 Tazama, nitawakanyaga kama mkokoteni uliojaa miganda inayoweza kumkanyaga mtu.
Behold, I am pressing you under, As the full cart presses a sheaf for itself.
14 Mtu akimbiaye hatapata kimbilio; mwenye nguvu hatoongeza nguvu zake mwenyewe; wala shujaa kujiokoa mwenyewe.
And refuge has perished from the swift, And the strong does not strengthens his power, And the mighty does not deliver his soul.
15 Apindaye upinde hatasimama; mkimbiaji sana hatakimbia; mwendesha farasi hatajiokoa mwenyewe.
And the handler of the bow does not stand, And the swift does not deliver [himself] with his feet, And the rider of the horse does not deliver his soul.
16 Hata wapiganaji shujaa watakimbia uchi katika siku hiyo -hivi ndivyo Yahwe asemavy.”
And the courageous of heart among the mighty, Flees naked in that day,” A declaration of YHWH!