< Amosi 2 >

1 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Moabu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu amechoma moto mifupa ya mfalme wa Edomu hadi kuwa chokaa.
Thus saith the Lord: For three crimes of Moab, and for four I will not convert him: because he hath burnt the bones of the king of Edom even to ashes.
2 Nitatuma moto juu ya Moabu, na utaangamiza ngome za Keriothi. Moabu atakufa katika gasia, pamoja na kelele na sauti ya tarumbeta.
And I will seed a fire into Moab, and it shall devour the houses of Carioth: and Moab shall die with a noise, with the sound of the trumpet:
3 Nitamuharibu mwamuzi kati yake, na nitawaua wana wa mfalme pamoja na yeye,” asema Yahwe.
And I will cut off the judge from the midst thereof, and will slay all his princes with him, saith the Lord.
4 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Yuda, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameikataa sheria ya Yahwe na hawakuzishika amri zake. Uongo wao umesababisha kupotea, ambao baba zao pia waliufuata.
Thus saith the Lord: For three crimes of Juda, and for four I will not convert him: because he hath cast away the law of the Lord, and hath not kept his commandments: for their idols have caused them to err, after which their fathers have walked.
5 Nitatuma moto juu ya Yuda, na utaimeza ngome ya Yerusalemu.”
And I will send a fire into Juda, and it shall devour the houses of Jerusalem.
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Israeli, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewauza wasio na hatia kwa fedha na maskini kwa jozi moja ya makubadhi.
Thus saith the Lord: For three crimes of Israel, and for four I will not convert him: because he hath sold the just man for silver, and the poor man for a pair of shoes.
7 Nao hukanyaga juu ya vichwa vya maskini kama kukanyaga kwenye mavumbi juu ya aridhi; wanasukuma kukandamiza. Mtu mmoja na baba yake walilala na msichana mmoja na hivyo kukufuru jina langu takatifu.
They bruise the heads of the poor upon the dust of the earth, and turn aside the way of the humble: and the son and his father have gone to the same young woman, to profane my holy name.
8 Nao hulala chini karibu na kila madhabahu kwenye nguo zilizowekwa dhamana, na katika nyumba ya Mungu wao hunywa divai ya wale ambao walitozwa faini.
And they sat down upon garments laid to pledge by every altar: and drank the wine of the condemned in the house of their God.
9 Bado nimemwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi; alikuwa na nguvu kama mialoni. Kisha nikaharibu matunda yake juu na mizizi yake chini.
Yet I cast out the Amorrhite before their face: whose height was like the height of cedars, and who was strong as an oak: and I destroyed his fruit from above, and his roots beneath.
10 Pia, niliwapandisha kutoka nchi ya Misri na kuwaongoza miaka arobaini nyikani ili mmiliki nchi ya Wamori.
It is I that brought you up out of the land of Egypt, and I led you forty years through the wilderness, that you might possess the land of the Amorrhite.
11 Nimewainua manabii kutoka miongoni mwa watoto wanu wawe Wanadhiri kutoka vijana wenu. Je sio hivyo, watu wa Israeli? -hivi ndivyo Yahwe asemavyo.
And I raised up of your sons for prophets, and of your young men for Nazarites. Is it not so, O ye children of Israel, saith the Lord?
12 Lakini mmewashawishi Wanadhiri kunywa mvinyo na kuwaamuru manabii wasifanye unabii.
And you will present wine to the Nazarites: and command the prophets, saying: Prophesy not.
13 Tazama, nitawakanyaga kama mkokoteni uliojaa miganda inayoweza kumkanyaga mtu.
Behold, I will screak under you as a wain screaketh that is laden with hay.
14 Mtu akimbiaye hatapata kimbilio; mwenye nguvu hatoongeza nguvu zake mwenyewe; wala shujaa kujiokoa mwenyewe.
And flight shall perish from the swift, and the valiant shall not possess his strength, neither shall the strong save his life.
15 Apindaye upinde hatasimama; mkimbiaji sana hatakimbia; mwendesha farasi hatajiokoa mwenyewe.
And he that holdeth the bow shall not stand, and the swift of foot shall not escape, neither shall the rider of the horse save his life.
16 Hata wapiganaji shujaa watakimbia uchi katika siku hiyo -hivi ndivyo Yahwe asemavy.”
And the stout of heart among the valiant shall flee away naked in that day, saith the Lord.

< Amosi 2 >