< Amosi 1 >
1 Haya ni mambo yanayoihusu Israeli ambayo Amosi, mmoja wa wachungaji katika Tekoa, aliyapokea katika ufunuo. Alipokea haya mambo katika siku za Uzia mfalme wa Yuda, na pia katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la aridhi.
Las palabras de Amos, que estaba entre los pastores de Tecoa; lo que vio de Israel en los días de Uzías, rey de Judá, y en los días de Jeroboam, hijo de Joás, rey de Israel, dos años antes del terremoto.
2 Alisema, “Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu. Malisho ya wachungaji yatanyamaza kimya; kilele cha Karmeli kitanyauka.”
Y él dijo: El Señor dará un rugido de león desde Sión, su voz sonará desde Jerusalén; y los campos de los criadores de ovejas estarán de duelo, y la parte superior del Carmelo se secará.
3 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Damaskasi, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya chuma.
Estas son las palabras del Señor: por tres crímenes de Damasco, y por cuatro, no dejaré que cambie su destino; porque trillaron a Galaad con instrumentos de trituración de hierro.
4 Nitapeleka moto kwenye nyumba ya Hazaeli, na utaiteketeza ngome za Ben Hadadi.
Y enviaré fuego a la casa de Hazael, quemando las grandes casas de Ben Hadad.
5 Nitazivunja komeo za Damaskasi na kumkatilia mbali mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni, na pia yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni. Na watu wa shamu watakwenda utumwani hata Kiri,” asema Yahwe.
Y tendré las cerraduras de la puerta de Damasco rotas, y al que está sentado en el poder lo exterminare del valle de Avén, y aquel en cuya mano está gobierno de la casa del Edén; y la gente de Siria se irá como prisioneros a Kir, dice el Señor.
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu waliwachukua mateka watu wote, kuwaweka juu ya mkono wa Edomu.
Estas son las palabras del Señor: por tres crímenes de Gaza, y por cuatro, no dejaré que cambie su destino; porque se llevaron a toda la gente prisioneros, para entregarlos a Edom.
7 Nitatuma moto kwenye kuta za Gaza, na kuziteketeza ngome zake.
Y enviaré un incendio al muro de Gaza, quemando sus palacios.
8 Nitamkatilia mbali yule mtu aishiye katika Ashdodi na mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, na mabaki ya Wafilisti wataangamia,” asema Bwana Yahwe.
Al que está sentado en el poder, lo habré cortado de Asdod, y aquel que gobierna en Ascalon; y mi mano se volverá contra Ecrón, y el resto de los filisteos vendrán a la destrucción, dice el Señor Dios.
9 Hivi ndivyo Yhawe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa nne, sintobadili adhabu, kwa sababu waliwapelekea watu wote wa Edomu, na wamevunja agano lao la undugu.
Estas son las palabras del Señor: por tres crímenes de Tiro, y por cuatro, no dejaré que cambie su destino; porque entregaron a todos los prisioneros a Edom, sin pensar en el acuerdo de los hermanos entre ellos.
10 Nitapeleka moto kwenye kuta za Tiro, nao utaziteketeza ngome zake.”
Y enviaré fuego sobre el muro de Tiro, quemando sus palacios.
11 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake kwa upanga na kutupilia mbali huruma zote. Hasira yake ikaendelea kuwa kali, na ghadhabu yake ikabaki milele.
Estas son las palabras del Señor: por tres crímenes de Edom, y por cuatro, no dejaré que cambie su destino; porque su espada se volvió contra su hermano, sin piedad, y su ira ardía en todo momento, y estaba enojado para siempre.
12 Nitapeleka moto juu ya Temani, na utaziteketeza nyumb a za kifalme za Bozra.”
Y enviaré fuego a Teman, quemando los palacios de Bosra.
13 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za watu wa Amoni, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili waweze kupanua mipaka yao.
Estas son las palabras del Señor: por tres crímenes de los hijos de Amón, y por cuatro, no revocara su castigo; porque en Galaad abrían los vientres de las mujeres embarazadas, con el fin de ampliar los límites de sus tierras.
14 Nitawasha moto katika kuta za Raba, nao utaziteketeza nyumba za kifalme, pamoja na kupiga kelele katika siku ya vita, pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga.
Y haré un fuego en el muro de Rabá, quemando sus palacios, en medio de gritos en el día de la batalla, en medio de una tempestad, en el día de la tormenta.
15 Mfalme wao ataenda utumwani, yeye na maafisa wake pamoja,” asema Yahwe.
Y su rey será hecho prisionero, él y sus capitanes juntos, dice el Señor.