< Amosi 1 >

1 Haya ni mambo yanayoihusu Israeli ambayo Amosi, mmoja wa wachungaji katika Tekoa, aliyapokea katika ufunuo. Alipokea haya mambo katika siku za Uzia mfalme wa Yuda, na pia katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la aridhi.
Words of Amos—who has been among herdsmen of Tekoa—that he has seen concerning Israel, in the days of Uzziah king of Judah, and in the days of Jeroboam son of Joash king of Israel, two years before the shaking;
2 Alisema, “Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu. Malisho ya wachungaji yatanyamaza kimya; kilele cha Karmeli kitanyauka.”
and he says, “YHWH roars from Zion, And gives forth His voice from Jerusalem, And pastures of the shepherds have mourned, And the top of Carmel has withered!”
3 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Damaskasi, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya chuma.
And thus said YHWH: “For three transgressions of Damascus, And for four, I do not reverse it, Because of their threshing Gilead with sharp-pointed irons,
4 Nitapeleka moto kwenye nyumba ya Hazaeli, na utaiteketeza ngome za Ben Hadadi.
And I have sent a fire against the house of Hazael, And it has consumed the palaces of Ben-Hadad.
5 Nitazivunja komeo za Damaskasi na kumkatilia mbali mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni, na pia yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni. Na watu wa shamu watakwenda utumwani hata Kiri,” asema Yahwe.
And I have broken the bar of Damascus, And cut off the inhabitant from Bikat-Aven, And a holder of a scepter from Beth-Eden, And the people of Aram have been removed to Kir,” said YHWH.
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu waliwachukua mateka watu wote, kuwaweka juu ya mkono wa Edomu.
Thus said YHWH: “For three transgressions of Gaza, And for four, I do not reverse it, Because of their removing a complete captivity, To deliver up to Edom,
7 Nitatuma moto kwenye kuta za Gaza, na kuziteketeza ngome zake.
And I have sent a fire against the wall of Gaza, And it has consumed her palaces;
8 Nitamkatilia mbali yule mtu aishiye katika Ashdodi na mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, na mabaki ya Wafilisti wataangamia,” asema Bwana Yahwe.
And I have cut off the inhabitant from Ashdod, And a holder of a scepter from Ashkelon, And have turned back My hand against Ekron, And the remnant of the Philistines have perished,” said Lord YHWH.
9 Hivi ndivyo Yhawe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa nne, sintobadili adhabu, kwa sababu waliwapelekea watu wote wa Edomu, na wamevunja agano lao la undugu.
Thus said YHWH: “For three transgressions of Tyre, And for four, I do not reverse it, Because of their delivering up a complete captivity to Edom, And they did not remember the brotherly covenant,
10 Nitapeleka moto kwenye kuta za Tiro, nao utaziteketeza ngome zake.”
And I have sent a fire against the wall of Tyre, And it has consumed her palaces.”
11 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake kwa upanga na kutupilia mbali huruma zote. Hasira yake ikaendelea kuwa kali, na ghadhabu yake ikabaki milele.
Thus said YHWH: “For three transgressions of Edom, And for four, I do not reverse it, Because of his pursuing his brother with a sword, And he has destroyed his mercies, And his anger tears continuously, And his wrath—he has kept it forever,
12 Nitapeleka moto juu ya Temani, na utaziteketeza nyumb a za kifalme za Bozra.”
And I have sent a fire against Teman, And it has consumed palaces of Bozrah.”
13 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za watu wa Amoni, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili waweze kupanua mipaka yao.
Thus said YHWH: “For three transgressions of the sons of Ammon, And for four, I do not reverse it, Because of their ripping up the pregnant ones of Gilead, To enlarge their border,
14 Nitawasha moto katika kuta za Raba, nao utaziteketeza nyumba za kifalme, pamoja na kupiga kelele katika siku ya vita, pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga.
And I have kindled a fire against the wall of Rabbah, And it has consumed her palaces, With a shout in a day of battle, With a whirlwind in a day of windstorm,
15 Mfalme wao ataenda utumwani, yeye na maafisa wake pamoja,” asema Yahwe.
And their king has gone in a removal, He and his heads together,” said YHWH!

< Amosi 1 >