< Amosi 1 >
1 Haya ni mambo yanayoihusu Israeli ambayo Amosi, mmoja wa wachungaji katika Tekoa, aliyapokea katika ufunuo. Alipokea haya mambo katika siku za Uzia mfalme wa Yuda, na pia katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la aridhi.
The words of Amos, who was among herdsmen of Thecua: which he saw concerning Israel in the days of Ozias king of Juda, and in the days of Jeroboam the son of Joas king of Israel two years before the earthquake.
2 Alisema, “Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu. Malisho ya wachungaji yatanyamaza kimya; kilele cha Karmeli kitanyauka.”
And he said: The Lord will roar from Sion, and utter his voice from Jerusalem: and the beautiful places of the shepherds have mourned, and the top of Carmel is withered.
3 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Damaskasi, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya chuma.
Thus saith the Lord: For three crimes of Damascus, and for four I will not convert it: because they have thrashed Galaad with iron wains.
4 Nitapeleka moto kwenye nyumba ya Hazaeli, na utaiteketeza ngome za Ben Hadadi.
And I will send a fire into the house of Azael, and it shall devour the houses of Benadad.
5 Nitazivunja komeo za Damaskasi na kumkatilia mbali mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni, na pia yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni. Na watu wa shamu watakwenda utumwani hata Kiri,” asema Yahwe.
And I will break the bar of Damascus: and I will cut off the inhabitants from the plain of the idol, and him that holdeth the sceptre from the house of pleasure: and the people of Syria shall be carried away to Cyrene, saith the Lord.
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu waliwachukua mateka watu wote, kuwaweka juu ya mkono wa Edomu.
Thus saith the Lord: For three crimes of Gaza, and for four I will not convert it: because they have carried away a perfect captivity to shut them up in Edom.
7 Nitatuma moto kwenye kuta za Gaza, na kuziteketeza ngome zake.
And I will send a fire on the wall of Gaza, and it shall devour the houses thereof.
8 Nitamkatilia mbali yule mtu aishiye katika Ashdodi na mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, na mabaki ya Wafilisti wataangamia,” asema Bwana Yahwe.
And I will cut off the inhabitant from Azotus, and him that holdeth the sceptre from Ascalon: and I will turn my hand against Accaron, and the rest of the Philistines shall perish, saith the Lord God.
9 Hivi ndivyo Yhawe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa nne, sintobadili adhabu, kwa sababu waliwapelekea watu wote wa Edomu, na wamevunja agano lao la undugu.
Thus saith the Lord: For three crimes of Tyre, and for four I will not convert it: because they have shut up an entire captivity in Edom, and have not remembered the covenant of brethren.
10 Nitapeleka moto kwenye kuta za Tiro, nao utaziteketeza ngome zake.”
And I will send a fire upon the wall of Tyre, and it shall devour the houses thereof.
11 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake kwa upanga na kutupilia mbali huruma zote. Hasira yake ikaendelea kuwa kali, na ghadhabu yake ikabaki milele.
Thus saith the Lord: For three crimes of Edom, and for four I will not convert him: because he hath pursued his brother with the sword, and hath cast off all pity, and hath carried on his fury, and hath kept his wrath to the end.
12 Nitapeleka moto juu ya Temani, na utaziteketeza nyumb a za kifalme za Bozra.”
I will send a fire into Theman: and it shall devour the houses of Bosra.
13 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za watu wa Amoni, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili waweze kupanua mipaka yao.
Thus saith the Lord: For three crimes of the children of Ammon, and for four I will not convert him: because he hath ripped up the women with child of Galaad to enlarge his border.
14 Nitawasha moto katika kuta za Raba, nao utaziteketeza nyumba za kifalme, pamoja na kupiga kelele katika siku ya vita, pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga.
And I will kindle a fire in the wall of Rabba: and it shall devour the houses thereof with shouting in the day of battle, and with a whirlwind in the day of trouble.
15 Mfalme wao ataenda utumwani, yeye na maafisa wake pamoja,” asema Yahwe.
And Melchom shall go into captivity, both he, and his princes together, saith the Lord.