< Matendo 1 >

1 Kitabu cha zamani nilikiandika, Theofilo, nikisema yote Yesu aliyoanza kufanya na kufundisha,
My first account, O Theophilus, dealt with all that Jesus began doing and teaching from the beginning down to the day when,
2 mpaka siku ambayo Yeye alipokelewa juu. Hii ilikuwa baada ya kutoa amri kupitia Roho Mtakatifu kwa mitume aliokuwa amewachagua.
after giving instructions through the Spirit to the apostles whom he had chosen, he was taken up to heaven.
3 Baada ya mateso yake, Yeye alionekana kwao akiwa hai pia na vithibitisho vingi vikishuhudia. Kwa siku arobaini alijidhihirisha kwao, na alizungumza kuhusu ufalme wa Mungu.
After his sufferings he had also shown himself alive to them in many convincing manifestations, revealing himself to them during forty days, and speaking of the kingdom of God.
4 Alipokuwa akikutana pamoja nao, aliwaamuru wasiondoke Yerusalemu, lakini wasubiri kwa ajili ya ahadi ya Baba, ambayo, alisema, “Mlisikia kutoka kwangu
And once when he was eating with them he charged them not to depart from Jerusalem, but to wait for the promise of the Father. "Of this," he said, "you have heard from me.
5 kwamba Yohana alibatiza kabisa kwa maji, lakini mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku hizi chache.”
"For John indeed baptized in water, but you shall be baptized in the Holy Spirit not many days hence."
6 Na walipokuwa wamekutanika pamoja walimuuliza, “Bwana, hivi huu ndio muda utakaowarudishia Israeli ufalme?”
So, when they came together, they began to ask him, "Master, are you at this time about to restore the kingdom of Israel?"
7 Yeye akawaambia, “Siyo sawa kwenu kujua wakati au majira ambayo Baba amekusudia kwa mamlaka yake mwenyewe.”
He answered. "It is not for you to know times and occasions which the Father has fixed in his own authority;
8 Lakini mtapokea nguvu, wakati Roho Mtakatifu atakapokuja juu yenu, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu kote katika Yerusalemu na Uyahudi yote na Samaria mpaka mwisho wa nchi.”
"yet you will receive power when the Holy Spirit comes upon you, and you are to be my witnesses both in Jerusalem and in all Judea, and in Samaria, and to the very ends of the earth."
9 Bwana Yesu alipokwisha yasema haya, wakiwa wanatazama juu, Yeye aliinuliwa juu, na wingu likamfunika wasimwone kwa macho yao.
When he had said this, and while they were looking at him, he was lifted up, and a cloud received him up out of their sight.
10 Wakati wanatazama mbinguni kwa makini akienda, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi meupe.
While they were gazing into the sky as he was going up, suddenly there were two men in white garments standing by them,
11 Walisema, “Enyi watu wa Galilaya, kwa nini mnasimama hapa mkitazama mbinguni?” Huyu Yesu aliyepaa juu mbinguni atarudi kwa namna ile ile kama mlivyomuona akienda mbinguni.
and they said. "Men of Galilee, why do you stand gazing into the sky? This same Jesus who has been taken up from you into the sky will come back in just the same way as you have seen him going into the sky."
12 Ndipo wakarudi Yerusalemu kutoka kwenye mlima wa mizeituni, ambao uko karibu na Yerusalemu, mwendo wa siku ya Sabato.
Then they returned to Jerusalem from the mountain called Olivet, which is near Jerusalem, about a Sabbath Day’s journey distant.
13 Walipofika walikwenda ghorofani walikokuwa wakikaa. Nao ni Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Thomaso, Batholomayo, Mathayo, Yakobo Mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda Mwana wa Yakobo.
On entering the city they went to the upper room where they were accustomed to meet. They were Peter and John and James and Andrew, Philip and Thomas, Bartholomew and Matthew, James, son of Alphaeus, and Simon the Zealot, and Judas the son of James.
14 Wote waliungana kama mtu mmoja, kwa juhudi walikuwa wakiendelea katika maombi. Pamoja na hao walikuwepo wanawake, Mariamu Mama yake Yesu, na kaka zake.
These all with one mind gave their constant attention to prayer, together with some women, and with Mary the mother of Jesus, and his brothers.
15 Katika siku zile Petro alisimama katikati ya ndugu, kama watu 120, akasema,
It was during these days that Peter stood up among the brothers - the whole number of persons present was about one hundred and twenty - and said.
16 Ndugu, ilikuwa lazima kwamba maandiko yatimizwe, ambapo zamani Roho Mtakatifu alisema kwa kinywa cha Daudi kuhusiana na Yuda, ambaye aliwaelekeza wale waliomkamata Yesu.
"Men and brothers, it was necessary for the Scripture to be fulfilled which the Holy Spirit uttered beforehand by the lips of David in regard to Judas who acted as guide to those who arrested Jesus.
17 Kwa kuwa yeye alikuwa mmoja wetu na alipokea fungu lake la faida katika hii huduma.”
"For he was numbered among us, and he did get his allotted share of this ministry.
18 (Sasa mtu huyu alinunua eneo kwa kile alichokipokea kwa uovu wake na hapo alianguka akitanguliza kichwa, mwili ukapasuka na matumbo yake yote yakawa wazi yakamwagika.
"Now this man bought a plot of ground with the price of his treachery, and falling there headlong he burst asunder and all his bowels gushed out.
19 Wote walioishi Yerusalemu walisikia kuhusu hili, hivyo eneo hilo wakaliita kwa lugha yao “Akeldama” hilo ni “shamba la damu.”)
"This fact became known to the people of Jerusalem so that the place was called in their language, Acheldamach, The Field of Blood.
20 “Kwenye kitabu cha Zaburi imeandikwa, 'Ngoja eneo lake liwe hame na isiruhusiwe hata mmoja kuishi pale;' na, 'Ruhusu mtu mwingine achukue nafasi yake ya uongozi.'
"For it is written in the Book of Psalms, Let his dwelling-place be desolate; Let no man dwell there, also, Let another take his work.
21 Hiyo ni muhimu, kwa hiyo, mmoja wa wanaume ambao waliambatana nasi wakati Bwana Yesu alipotoka na kuingia kati yetu,
"It is necessary then that, of the men who have been associated with us during the whole time in which the Lord Jesus went in and out among us,
22 kuanzia kwenye ubatizo wa Yohana mpaka siku ile alipotwaliwa juu, lazima awe shahidi wa ufufuo pamoja nasi.
from his baptism by John down to the day on which he was taken up from us, one should join us a witness to his resurrection."
23 “Wakaweka mbele wanaume wawili, Yusufu aitwaye Barnaba, ambaye pia aliitwa Yusto na Mathia.
So they placed two in nomination, Joseph called Bar-Sabbas (surnamed Justas) and Matthias;
24 Wao waliomba wakisema, “Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, hivyo weka wazi yupi kati ya wawili hawa ambaye umemchagua
and they prayed, saying. "Thou, O Lord, who knowest the hearts of all men, show clearly which of these two men thou hast chosen to fill the place
25 kuchukua nafasi katika huduma na utume, ambapo Yuda alitenda uovu na kwenda mahali pake.”
"in this ministry of this apostles from which Judas went out to go to his own place."
26 Wakapiga kura kwa ajili yao, na kura ikamwangukia Mathia ambaye alihesabiwa pamoja na wale mitume kumi na moja.
Then they cast lots for them, and the lot fell upon Matthias, and he was numbered with the eleven apostles.

< Matendo 1 >