< Matendo 1 >

1 Kitabu cha zamani nilikiandika, Theofilo, nikisema yote Yesu aliyoanza kufanya na kufundisha,
The former account, indeed, I made concerning all things, O Theophilus, that Jesus began both to do and to teach,
2 mpaka siku ambayo Yeye alipokelewa juu. Hii ilikuwa baada ya kutoa amri kupitia Roho Mtakatifu kwa mitume aliokuwa amewachagua.
until the day in which, having given command through the Holy Spirit to the apostles whom He chose out, He was taken up,
3 Baada ya mateso yake, Yeye alionekana kwao akiwa hai pia na vithibitisho vingi vikishuhudia. Kwa siku arobaini alijidhihirisha kwao, na alizungumza kuhusu ufalme wa Mungu.
to whom He also presented Himself alive after His suffering, in many certain proofs, being seen by them through forty days, and speaking the things concerning the Kingdom of God.
4 Alipokuwa akikutana pamoja nao, aliwaamuru wasiondoke Yerusalemu, lakini wasubiri kwa ajili ya ahadi ya Baba, ambayo, alisema, “Mlisikia kutoka kwangu
And being assembled together with them, He commanded them not to depart from Jerusalem, but to wait for the promise of the Father, “Which you heard from Me;
5 kwamba Yohana alibatiza kabisa kwa maji, lakini mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku hizi chache.”
because John, indeed, immersed in water, but you will be immersed in the Holy Spirit not many days after these.”
6 Na walipokuwa wamekutanika pamoja walimuuliza, “Bwana, hivi huu ndio muda utakaowarudishia Israeli ufalme?”
They, therefore, indeed, having come together, were questioning Him, saying, “Lord, do You at this time restore the kingdom to Israel?”
7 Yeye akawaambia, “Siyo sawa kwenu kujua wakati au majira ambayo Baba amekusudia kwa mamlaka yake mwenyewe.”
And He said to them, “It is not yours to know times or seasons that the Father appointed in His own authority;
8 Lakini mtapokea nguvu, wakati Roho Mtakatifu atakapokuja juu yenu, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu kote katika Yerusalemu na Uyahudi yote na Samaria mpaka mwisho wa nchi.”
but you will receive power at the coming of the Holy Spirit on you, and you will be witnesses for Me both in Jerusalem, and in all Judea and Samaria, and to the end of the earth.”
9 Bwana Yesu alipokwisha yasema haya, wakiwa wanatazama juu, Yeye aliinuliwa juu, na wingu likamfunika wasimwone kwa macho yao.
And having said these things—they beholding—He was taken up, and a cloud received Him up from their sight;
10 Wakati wanatazama mbinguni kwa makini akienda, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi meupe.
and as they were looking steadfastly to the sky in His going on, then, behold, two men stood by them in white clothing,
11 Walisema, “Enyi watu wa Galilaya, kwa nini mnasimama hapa mkitazama mbinguni?” Huyu Yesu aliyepaa juu mbinguni atarudi kwa namna ile ile kama mlivyomuona akienda mbinguni.
who also said, “Men, Galileans, why do you stand gazing into the sky? This Jesus who was received up from you into Heaven, will so come in what manner you saw Him going on to Heaven.”
12 Ndipo wakarudi Yerusalemu kutoka kwenye mlima wa mizeituni, ambao uko karibu na Yerusalemu, mwendo wa siku ya Sabato.
Then they returned to Jerusalem from [that] called the Mount of Olives, that is near Jerusalem, a Sabbath’s journey;
13 Walipofika walikwenda ghorofani walikokuwa wakikaa. Nao ni Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Thomaso, Batholomayo, Mathayo, Yakobo Mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda Mwana wa Yakobo.
and when they came in, they went up into the upper room, where were abiding both Peter, and James, and John, and Andrew, Philip, and Thomas, Bartholomew, and Matthew, James, of Alphaeus, and Simon the Zealot, and Judas, of James;
14 Wote waliungana kama mtu mmoja, kwa juhudi walikuwa wakiendelea katika maombi. Pamoja na hao walikuwepo wanawake, Mariamu Mama yake Yesu, na kaka zake.
these were all continuing with one accord in prayer and supplication, with women, and Mary the mother of Jesus, and with His brothers.
15 Katika siku zile Petro alisimama katikati ya ndugu, kama watu 120, akasema,
And in these days, Peter having risen up in the midst of the disciples, said (also the multitude of the names at the same place was, as it were, one hundred and twenty),
16 Ndugu, ilikuwa lazima kwamba maandiko yatimizwe, ambapo zamani Roho Mtakatifu alisema kwa kinywa cha Daudi kuhusiana na Yuda, ambaye aliwaelekeza wale waliomkamata Yesu.
“Men, brothers, it was necessary [for] this Writing to be fulfilled that the Holy Spirit spoke beforehand through the mouth of David, concerning Judas, who became guide to those who took Jesus,
17 Kwa kuwa yeye alikuwa mmoja wetu na alipokea fungu lake la faida katika hii huduma.”
because he was numbered among us, and received the share in this ministry.
18 (Sasa mtu huyu alinunua eneo kwa kile alichokipokea kwa uovu wake na hapo alianguka akitanguliza kichwa, mwili ukapasuka na matumbo yake yote yakawa wazi yakamwagika.
(This one, indeed, then, purchased a field out of the reward of unrighteousness, and falling headlong, burst apart in the midst, and all his bowels gushed forth,
19 Wote walioishi Yerusalemu walisikia kuhusu hili, hivyo eneo hilo wakaliita kwa lugha yao “Akeldama” hilo ni “shamba la damu.”)
and it became known to all those dwelling in Jerusalem, insomuch that this place is called, in their proper dialect, Aceldama, that is, Field of Blood.)
20 “Kwenye kitabu cha Zaburi imeandikwa, 'Ngoja eneo lake liwe hame na isiruhusiwe hata mmoja kuishi pale;' na, 'Ruhusu mtu mwingine achukue nafasi yake ya uongozi.'
For it has been written in [the] Scroll of Psalms: Let his lodging-place become desolate, and let no one be dwelling in it, and let another take his oversight.
21 Hiyo ni muhimu, kwa hiyo, mmoja wa wanaume ambao waliambatana nasi wakati Bwana Yesu alipotoka na kuingia kati yetu,
It is necessary, therefore, of the men who went with us during all the time in which the Lord Jesus went in and went out among us,
22 kuanzia kwenye ubatizo wa Yohana mpaka siku ile alipotwaliwa juu, lazima awe shahidi wa ufufuo pamoja nasi.
beginning from the immersion of John, to the day in which He was received up from us, one of these to become with us a witness of His resurrection.”
23 “Wakaweka mbele wanaume wawili, Yusufu aitwaye Barnaba, ambaye pia aliitwa Yusto na Mathia.
And they set two, Joseph called Barsabas, who was surnamed Justus, and Matthias,
24 Wao waliomba wakisema, “Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, hivyo weka wazi yupi kati ya wawili hawa ambaye umemchagua
and having prayed, they said, “You, LORD, who are knowing the heart of all, show which one You chose of these two,
25 kuchukua nafasi katika huduma na utume, ambapo Yuda alitenda uovu na kwenda mahali pake.”
to receive the share of this ministry and apostleship, from which Judas, by transgression, fell, to go on to his proper place”;
26 Wakapiga kura kwa ajili yao, na kura ikamwangukia Mathia ambaye alihesabiwa pamoja na wale mitume kumi na moja.
and they gave their lots, and the lot fell on Matthias, and he was numbered with the eleven apostles.

< Matendo 1 >