< Matendo 1 >
1 Kitabu cha zamani nilikiandika, Theofilo, nikisema yote Yesu aliyoanza kufanya na kufundisha,
I have made the former treatise, O Theophilus, of al that Jesus began to doe and teach,
2 mpaka siku ambayo Yeye alipokelewa juu. Hii ilikuwa baada ya kutoa amri kupitia Roho Mtakatifu kwa mitume aliokuwa amewachagua.
Vntill the day that hee was taken vp, after that hee through the holy Ghost, had giuen commandements vnto the Apostles, whome hee had chosen:
3 Baada ya mateso yake, Yeye alionekana kwao akiwa hai pia na vithibitisho vingi vikishuhudia. Kwa siku arobaini alijidhihirisha kwao, na alizungumza kuhusu ufalme wa Mungu.
To whome also he presented himselfe aliue after that he had suffered, by many infallible tokens, being seene of them by the space of fourtie daies, and speaking of those thinges which appertaine to the kingdome of God.
4 Alipokuwa akikutana pamoja nao, aliwaamuru wasiondoke Yerusalemu, lakini wasubiri kwa ajili ya ahadi ya Baba, ambayo, alisema, “Mlisikia kutoka kwangu
And when he had gathered them together, he commanded them, that they should not depart from Hierusalem, but to waite for the promise of the Father, which sayde hee, yee haue heard of me.
5 kwamba Yohana alibatiza kabisa kwa maji, lakini mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku hizi chache.”
For Iohn in deede baptized with water, but ye shall be baptized with the holy Ghost within these fewe daies.
6 Na walipokuwa wamekutanika pamoja walimuuliza, “Bwana, hivi huu ndio muda utakaowarudishia Israeli ufalme?”
When they therefore were come together, they asked of him, saying, Lord, wilt thou at this time restore the kingdome to Israel?
7 Yeye akawaambia, “Siyo sawa kwenu kujua wakati au majira ambayo Baba amekusudia kwa mamlaka yake mwenyewe.”
And hee saide vnto them, It is not for you to know the times, or the seasons, which the Father hath put in his owne power,
8 Lakini mtapokea nguvu, wakati Roho Mtakatifu atakapokuja juu yenu, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu kote katika Yerusalemu na Uyahudi yote na Samaria mpaka mwisho wa nchi.”
But yee shall receiue power of the holy Ghost, when he shall come on you: and ye shalbe witnesses vnto me both in Hierusalem and in all Iudea, and in Samaria, and vnto the vttermost part of the earth.
9 Bwana Yesu alipokwisha yasema haya, wakiwa wanatazama juu, Yeye aliinuliwa juu, na wingu likamfunika wasimwone kwa macho yao.
And when he had spoken these things, while they behelde, he was taken vp: for a cloude tooke him vp out of their sight.
10 Wakati wanatazama mbinguni kwa makini akienda, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi meupe.
And while they looked stedfastly towarde heauen, as hee went, beholde, two men stoode by them in white apparell,
11 Walisema, “Enyi watu wa Galilaya, kwa nini mnasimama hapa mkitazama mbinguni?” Huyu Yesu aliyepaa juu mbinguni atarudi kwa namna ile ile kama mlivyomuona akienda mbinguni.
Which also sayde, Yee men of Galile, why stande yee gasing into heauen? This Iesus which is taken vp from you into heauen, shall so come, as yee haue seene him goe into heauen.
12 Ndipo wakarudi Yerusalemu kutoka kwenye mlima wa mizeituni, ambao uko karibu na Yerusalemu, mwendo wa siku ya Sabato.
Then returned they vnto Hierusalem from the mount that is called the mount of Oliues, which is neere to Hierusalem, being from it a Sabbath daies iourney.
13 Walipofika walikwenda ghorofani walikokuwa wakikaa. Nao ni Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Thomaso, Batholomayo, Mathayo, Yakobo Mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda Mwana wa Yakobo.
And when they were come in, they went vp into an vpper chamber, where abode both Peter and Iames, and Iohn, and Andrew, Philip, and Thomas, Bartlemew, and Matthewe, Iames the sonne of Alpheus, and Simon Zelotes, and Iudas Iames brother.
14 Wote waliungana kama mtu mmoja, kwa juhudi walikuwa wakiendelea katika maombi. Pamoja na hao walikuwepo wanawake, Mariamu Mama yake Yesu, na kaka zake.
These all continued with one accorde in prayer and supplication with the women, and Marie the mother of Iesus, and with his brethren.
15 Katika siku zile Petro alisimama katikati ya ndugu, kama watu 120, akasema,
And in those dayes Peter stoode vp in the middes of the disciples, and sayde (nowe the nomber of names that were in one place were about an hundreth and twentie.)
16 Ndugu, ilikuwa lazima kwamba maandiko yatimizwe, ambapo zamani Roho Mtakatifu alisema kwa kinywa cha Daudi kuhusiana na Yuda, ambaye aliwaelekeza wale waliomkamata Yesu.
Yee men and brethren, this scripture must needes haue beene fulfilled, which the holy Ghost by the mouth of Dauid spake before of Iudas, which was guide to them that tooke Iesus.
17 Kwa kuwa yeye alikuwa mmoja wetu na alipokea fungu lake la faida katika hii huduma.”
For hee was nombred with vs, and had obteined fellowship in this ministration.
18 (Sasa mtu huyu alinunua eneo kwa kile alichokipokea kwa uovu wake na hapo alianguka akitanguliza kichwa, mwili ukapasuka na matumbo yake yote yakawa wazi yakamwagika.
He therefore hath purchased a field with the reward of iniquitie: and when he had throwen downe himselfe headlong, hee brast asunder in the middes, and all his bowels gushed out.
19 Wote walioishi Yerusalemu walisikia kuhusu hili, hivyo eneo hilo wakaliita kwa lugha yao “Akeldama” hilo ni “shamba la damu.”)
And it is knowen vnto all the inhabitants of Hierusalem, in so much, that that field is called in their owne language, Aceldama, That is, the field of blood.
20 “Kwenye kitabu cha Zaburi imeandikwa, 'Ngoja eneo lake liwe hame na isiruhusiwe hata mmoja kuishi pale;' na, 'Ruhusu mtu mwingine achukue nafasi yake ya uongozi.'
For it is written in the booke of Psalmes, Let his habitation be void, and let no man dwel therein: also, Let another take his charge.
21 Hiyo ni muhimu, kwa hiyo, mmoja wa wanaume ambao waliambatana nasi wakati Bwana Yesu alipotoka na kuingia kati yetu,
Wherefore of these men which haue companied with vs, all the time that the Lord Iesus was conuersant among vs,
22 kuanzia kwenye ubatizo wa Yohana mpaka siku ile alipotwaliwa juu, lazima awe shahidi wa ufufuo pamoja nasi.
Beginning from the baptisme of Iohn vnto the day that hee was taken vp from vs, must one of them bee made a witnesse with vs of his resurrection.
23 “Wakaweka mbele wanaume wawili, Yusufu aitwaye Barnaba, ambaye pia aliitwa Yusto na Mathia.
And they presented two, Ioseph called Barsabas, whose surname was Iustus, and Matthias.
24 Wao waliomba wakisema, “Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, hivyo weka wazi yupi kati ya wawili hawa ambaye umemchagua
And they praied, saying, Thou Lord, which knowest the hearts of all men, shewe whether of these two thou hast chosen,
25 kuchukua nafasi katika huduma na utume, ambapo Yuda alitenda uovu na kwenda mahali pake.”
That he may take the roume of this ministration and Apostleship, from which Iudas hath gone astray, to goe to his owne place.
26 Wakapiga kura kwa ajili yao, na kura ikamwangukia Mathia ambaye alihesabiwa pamoja na wale mitume kumi na moja.
Then they gaue foorth their lottes: and the lotte fell on Matthias, and hee was by a common consent counted with the eleuen Apostles.