< Matendo 9 >

1 Lakini Sauli, aliendelea kusema vitisho hata vya kifo kwa wanafunzi wa Bwana, alikwenda kwa kuhani mkuu
But Saul, still speaking threats even of murder against the disciples of the Lord, went to the high priest
2 na kumwomba barua kwa ajili ya masinagogi huko Dameski, ili kwamba akimpata mtu aliye katika Njia ile, awe mwanaume au mwanamke, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.
and asked him for letters for the synagogues in Damascus, so that if he found any who belonged to the Way, whether men or women, he might bring them bound to Jerusalem.
3 Hata alipokuwa akisafiri, ilitokea kwamba alipokaribia Dameski, ghafla ikamwangaza kotekote nuru kutoka mbinguni,'
As he was traveling, it happened that as he came near to Damascus, suddenly there shone all around him a light out of heaven;
4 naye akaanguka chini na akasikia sauti ikimwambia,”Sauli, Sauli, mbona wanitesa mimi?”
and he fell upon the ground and heard a voice saying to him, “Saul, Saul, why are you persecuting me?”
5 Sauli akajibu, U nani wewe Bwana? Bwana akasema, “Mimi ndiye Yesu unayeniudhi;
Saul replied, “Who are you, Lord?” The Lord said, “I am Jesus whom you are persecuting;
6 Lakini inuka, ingia mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda
but rise, enter into the city, and it will be told you what you must do.”
7 Wale watu waliosafiri pamoja na Sauli wakatulia kimya, wakisikiliza sauti, wasione mtu.
The men who traveled with Saul stood speechless, hearing the voice, but seeing no one.
8 Sauli akainuka katika nchi na alipofungua macho yake, hakuweza kuona kitu, wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski.
Saul arose from the ground, and when he opened his eyes, he could see nothing; so they led him by the hand and brought him into Damascus.
9 Kwa siku tatu haoni, hali, wala hanywi.
For three days he was without sight, and he neither ate nor drank.
10 Basi palikuwapo mwanafunzi Dameski jina lake Anania, Bwana alisema naye katika maono, “Anania.” Na akasema, “Tazama, nipo hapa, Bwana.
Now there was a disciple at Damascus named Ananias. The Lord said to him in a vision, “Ananias!” He said, “See, I am here, Lord.”
11 “Bwana akamwambia, “Inuka uenda zako katika mtaa uitwao Nyofu, na katika nyumba ya Yuda na ukaulize mtu kutoka Tarso aitwaye Sauli; maana angali anaomba;
The Lord said to him, “Arise, and go to the street which is called Straight, and at the house of Judas ask for a man from Tarsus named Saul, for he is praying.
12 na alimwona katika maono mtu jina lake Anania akiingia na kumwekea mikono juu yake ili kwamba apate kuona.
He has seen in a vision a man named Ananias coming in and laying his hands on him, so that he might see again.”
13 Lakini Anania akajibu, “Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, kwa kiasi gani alivyowatendea mabaya watakatifu wa huko Yerusalemu;
But Ananias answered, “Lord, I have heard from many about this man, how much harm he has done to your holy people in Jerusalem.
14 Hapa ana mamlaka kutoka kwa kuhani mkuu kumkamata kila mmoja anayeliitia jina lako.
He has authority from the chief priests to arrest everyone here who calls upon your name.”
15 Lakini Bwana akamwambia, “Nenda, kwa maana yeye ni chombo teule kwangu, alichukue jina langu mbele ya Mataifa na wafalme na wana wa Israeli.
But the Lord said to him, “Go, for he is a chosen instrument of mine, to carry my name before the Gentiles and kings and the children of Israel;
16 Maana nitawaonesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya jina langu”.
for I will show him how much he must suffer for the cause of my name.”
17 Anania akaenda, akaingia mle nyumbani; Akamwekea mikono akasema, Ndugu Sauli, Bwana Yesu, aliyekutokea katika njia ulipokuwa unakuja, amenituma upate kuona tena na ujazwe Roho Mtakatifu.
So Ananias departed, and entered into the house. Laying his hands on him, he said, “Brother Saul, the Lord Jesus, who appeared to you on the road when you were coming, has sent me so that you might receive your sight and be filled with the Holy Spirit.”
18 Ghafla vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa; akala chakula na kupata nguvu.
Immediately something like scales fell from Saul's eyes, and he received his sight; he arose and was baptized;
19 Akakaa pamoja na wanafunzi huko Dameski kwa siku nyingi.
and he ate and was strengthened. He stayed with the disciples in Damascus for several days.
20 Wakati huo huo akamtangaza Yesu katika masinagogi, akisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.
Right away he proclaimed Jesus in the synagogues, saying that he is the Son of God.
21 Na wote waliosikia walishangaa na kusema, “Siyo mtu huyu aliyewaharibu wote walioita Jina hili huko Yerusalemu? Na hapa alikuja kwa kusudi la kuwafunga na kuwapeleka kwa makuhani.”
All who heard him were amazed and said, “Is not this the man who destroyed those in Jerusalem who called on this name? He has come here to take them bound to the chief priests.”
22 Lakini Sauli aliwezeshwa kuhubiri na kuwafanya Wayahudi waliokaa Dameski wachanganyikiwe na kuthibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.
But Saul became more and more powerful, and he was causing distress among the Jews who lived in Damascus by proving that Jesus is the Christ.
23 Baada ya siku nyingi, Wayahudi wakafanya shauri pamoja ili wamuue.
After many days, the Jews planned together to kill him.
24 Lakini mpango wao ukajulikana na Sauli. Wakamvizia mlangoni mchana na usiku wapate kumuua.
But their plan became known to Saul. They watched the gates day and night in order to kill him.
25 Lakini wanafunzi wake wakamchukua usiku wakamshusha kupitia ukutani, wakamtelemsha chini katika kapu.
But his disciples took him by night and let him down through the wall, lowering him in a basket.
26 Na Sauli alipofika Yerusalemu, alijaribu kujiunga na wanafunzi lakini walikuwa wakimuogopa, wasisadiki kuwa yeye ni mwanafunzi.
When he had come to Jerusalem, Saul attempted to join the disciples, but they were all afraid of him, not believing that he was a disciple.
27 Lakini Barnaba akamchukua na kumpeleka kwa mitume, Na akawaeleza jinsi Sauli alivyomuona Bwana njiani na Bwana alivyosema nae, na jinsi Sauli alivyohubiri kwa ujasiri kwa jina la Yesu huko Dameski.
But Barnabas took him and brought him to the apostles, and he told them how Saul had seen the Lord on the road and that the Lord had spoken to him, and how at Damascus Saul had spoken boldly in the name of Jesus.
28 Alikutana nao walipoingia na kutoka Yerusalemu. Akanena kwa ujasiri kwa jina la Bwana Yesu,
He met with them as they were coming in and going out of Jerusalem. He spoke boldly in the name of the Lord Jesus
29 akihojiana na Wayahudi wa Kiyunani lakini wakijaribu mara kwa mara kumuua.
and debated with the Grecian Jews; but they kept trying to kill him.
30 Wakati ndugu walipojua jambo hilo, wakamchukua mpaka Kaisaria, na wampeleke aende Tarso.
When the brothers learned of this, they brought him down to Caesarea and sent him away to Tarsus.
31 Basi kanisa lote katika Uyahudi, Galilaya na Samaria, lilikuwa na amani, na likajengwa, na kutembea katika hofu ya Bwana na faraja ya Roho Mtakatifu, kanisa likakua kwa kuongezeka idadi.
So then, the church throughout all Judea, Galilee, and Samaria had peace and was built up; and, walking in the fear of the Lord and in the comfort of the Holy Spirit, the church grew in numbers.
32 Kisha ilitokea Petro alipokuwa akizungukazunguka pande zote za mkoa, akawateremkia waumini waishio katika mji wa Lida.
Now it came about that, as Peter went throughout the whole region, he came down also to the believers who lived in the town of Lydda.
33 Akamuona huko mtu mmoja jina lake Ainea, mtu huyo amekuwa kitandani miaka minane; maana alikuwa amepooza.
There he found a certain man named Aeneas, who had been in his bed for eight years, for he was paralyzed.
34 Petro akamwambia, “Ainea, Yesu Kristo akuponye; Amka na ujitandikia kitanda chako,” Mara akaamka.
Peter said to him, “Aeneas, Jesus Christ heals you. Get up and make your bed,” and right away he got up.
35 Na watu wote waliokaa Lida na Sharoni walipomuona mtu huyo, walimgeukia Bwana.
So everyone who lived in Lydda and in Sharon saw the man and they turned to the Lord.
36 Palikuwa na mwanafunzi Yafa aitwaye Tabitha, ambalo lilitafsiriwa kama “Dorcas” Huyu mwanamke alijaa kazi njema na matendo ya rehema aliyoyafanya kwa maskini.
Now there was in Joppa a certain disciple named Tabitha, which is translated as “Dorcas.” This woman was full of good works and merciful deeds that she did for the poor.
37 Ilitokea katika siku hizo aliugua na akafa; walipomsafisha, walimpandisha chumba cha juu na kumlaza.
It came about in those days that she fell sick and died; when they had washed her, they laid her in an upper room.
38 Kwa vile Lida ilikuwa karibu na Yafa, na wanafunzi walisikia kwamba Petro alikuwa huko, waliwatuma watu wawili kwake, wakimsihi, “Njoo kwetu bila kuchelewa”.
Since Lydda was near Joppa, and the disciples had heard that Peter was there, they sent two men to him, begging him, “Come to us without delay.”
39 Petro akaamka na akaondoka pamoja nao. Alipofika, walimleta katika chumba cha juu. Na wajane wote walisimama karibu naye wakilia, wakimwonyesha koti na nguo ambazo Dorcas aliwashonea wakati akiwa pamoja nao.
Peter arose and went with them. When he had arrived, they brought him to the upper room, and all the widows stood by him weeping, showing him the coats and garments that Dorcas had made while she had been with them.
40 Petro akawatoa wote nje ya chumba, akapiga magoti akaomba, kisha akaugekia mwili, akasema, “Tabitha, amka”. Akafungua macho yake na alipomwona Petro akakaa chini.
Peter put them all out of the room, knelt down, and prayed; then, turning to the body, he said, “Tabitha, arise.” Then she opened her eyes, and seeing Peter she sat up.
41 Kisha Petro akampa mkono wake akamwinua, na alipowaita waamini na wajane, akawakabidhi kwao akiwa hai
Peter then gave her his hand and lifted her up; and when he called the believers and the widows, he presented her alive to them.
42 Jambo hili likajulikana Yafa yote, na watu wengi wakamwamini Bwana.
This matter became known throughout all Joppa, and many people believed on the Lord.
43 Ilitokea Petro akakaa siku nyingi Yafa pamoja na mtu aitwaye Simoni, mtengeneza ngozi.
It happened that Peter stayed for many days in Joppa with a man named Simon, a tanner.

< Matendo 9 >