< Matendo 9 >
1 Lakini Sauli, aliendelea kusema vitisho hata vya kifo kwa wanafunzi wa Bwana, alikwenda kwa kuhani mkuu
Meanwhile Saul, still breathing out threats of murder against the disciples of the Lord, went to the high priest
2 na kumwomba barua kwa ajili ya masinagogi huko Dameski, ili kwamba akimpata mtu aliye katika Njia ile, awe mwanaume au mwanamke, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.
and begged of him letters addressed to the synagogues in Damascus, so that if he found any that were of the Way, either men or women, he could bind them and bring them to Jerusalem.
3 Hata alipokuwa akisafiri, ilitokea kwamba alipokaribia Dameski, ghafla ikamwangaza kotekote nuru kutoka mbinguni,'
And as he journeyed, when he was approaching Damascus, suddenly a light from heaven flashed round him.
4 naye akaanguka chini na akasikia sauti ikimwambia,”Sauli, Sauli, mbona wanitesa mimi?”
He fell to the ground, and heard a voice which said to him, "Saul, Saul, why are you persecuting me?"
5 Sauli akajibu, U nani wewe Bwana? Bwana akasema, “Mimi ndiye Yesu unayeniudhi;
And he said, "Who are you Lord?"
6 Lakini inuka, ingia mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda
"I am Jesus, whom you are persecuting," he said. "Stand up and go into the city, and there you shall be told what you must do."
7 Wale watu waliosafiri pamoja na Sauli wakatulia kimya, wakisikiliza sauti, wasione mtu.
Meanwhile the men who were his fellow travelers stood speechless, hearing indeed the voice, but beholding no one.
8 Sauli akainuka katika nchi na alipofungua macho yake, hakuweza kuona kitu, wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski.
And Saul got up from the ground, but although his eyes were open, he continued to perceive nothing; so they took him by the hand and led him into Damascus.
9 Kwa siku tatu haoni, hali, wala hanywi.
And he remained there three days, seeing nothing, and without eating or drinking.
10 Basi palikuwapo mwanafunzi Dameski jina lake Anania, Bwana alisema naye katika maono, “Anania.” Na akasema, “Tazama, nipo hapa, Bwana.
Now there was in Damascus a disciple named Ananias, and the Lord spoke to him in a vision, saying, "Ananias!" And he answered, "Lo, I am here, Lord."
11 “Bwana akamwambia, “Inuka uenda zako katika mtaa uitwao Nyofu, na katika nyumba ya Yuda na ukaulize mtu kutoka Tarso aitwaye Sauli; maana angali anaomba;
And the Lord said to him. "Arise, go into the street named ‘Straight,’ and make inquiries in the house of Judas for a man of Tarsus, one Saul.
12 na alimwona katika maono mtu jina lake Anania akiingia na kumwekea mikono juu yake ili kwamba apate kuona.
He is now praying, and has seen a man named Ananias enter and lay his hands on him to restore his sight."
13 Lakini Anania akajibu, “Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, kwa kiasi gani alivyowatendea mabaya watakatifu wa huko Yerusalemu;
"But, Lord," said Ananias, "I have heard from many about that man, and how much evil he did to the saints at Jerusalem!
14 Hapa ana mamlaka kutoka kwa kuhani mkuu kumkamata kila mmoja anayeliitia jina lako.
"In this city, too, he has authority from the chief priests to arrest all those who call upon thy name."
15 Lakini Bwana akamwambia, “Nenda, kwa maana yeye ni chombo teule kwangu, alichukue jina langu mbele ya Mataifa na wafalme na wana wa Israeli.
"Go," answered the Lord, "this man is chosen instrument of mine to bear my name before the nations and their kings, and before the Children of Israel also;
16 Maana nitawaonesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya jina langu”.
"for I am going to show him all he has to suffer for the sake of my name."
17 Anania akaenda, akaingia mle nyumbani; Akamwekea mikono akasema, Ndugu Sauli, Bwana Yesu, aliyekutokea katika njia ulipokuwa unakuja, amenituma upate kuona tena na ujazwe Roho Mtakatifu.
And so Ananias went and entered into the house, and laying his hands on him, said, "Brother Saul, the Lord, even Jesus, who appeared to you on your journey, has sent me that you may receive your sight, and be filled with the Holy Spirit."
18 Ghafla vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa; akala chakula na kupata nguvu.
Instantly something like scales fell from his eyes, and he received his sight. He arose and was baptized.
19 Akakaa pamoja na wanafunzi huko Dameski kwa siku nyingi.
Afterward he took food and was strengthened. And he remained for some time with the disciples at Damascus.
20 Wakati huo huo akamtangaza Yesu katika masinagogi, akisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.
And he began at once to proclaim in the synagogues Jesus as the Son of God.
21 Na wote waliosikia walishangaa na kusema, “Siyo mtu huyu aliyewaharibu wote walioita Jina hili huko Yerusalemu? Na hapa alikuja kwa kusudi la kuwafunga na kuwapeleka kwa makuhani.”
His hearers were all astonished, and began to say. "Is not this the very man who in Jerusalem made havoc of those who called upon the Name? Did he not come hither for the express purpose of carrying them all in chains to the high priests?"
22 Lakini Sauli aliwezeshwa kuhubiri na kuwafanya Wayahudi waliokaa Dameski wachanganyikiwe na kuthibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.
But Saul gained more and more influence, and kept putting the Jews who lived in Damascus to confusion by his proof that Jesus was the Christ.
23 Baada ya siku nyingi, Wayahudi wakafanya shauri pamoja ili wamuue.
And when many days were fulfilled the Jews made a plot to kill Saul;
24 Lakini mpango wao ukajulikana na Sauli. Wakamvizia mlangoni mchana na usiku wapate kumuua.
but information of their plot was given Saul, and although they kept watch day and night on the gates, in order to make away with him,
25 Lakini wanafunzi wake wakamchukua usiku wakamshusha kupitia ukutani, wakamtelemsha chini katika kapu.
his disciples took him by night, and let him down over the wall, lowering him in a basket.
26 Na Sauli alipofika Yerusalemu, alijaribu kujiunga na wanafunzi lakini walikuwa wakimuogopa, wasisadiki kuwa yeye ni mwanafunzi.
So he came to Jerusalem, and attempted to join the disciples, but they were all afraid of him, because they did not believe that he was a disciple.
27 Lakini Barnaba akamchukua na kumpeleka kwa mitume, Na akawaeleza jinsi Sauli alivyomuona Bwana njiani na Bwana alivyosema nae, na jinsi Sauli alivyohubiri kwa ujasiri kwa jina la Yesu huko Dameski.
But Barnabas took him and brought him to the apostles, and told them how Saul had seen the Lord in the way, and that he had spoken to him; and also how he had preached the Name of the Lord Jesus boldly at Damascus.
28 Alikutana nao walipoingia na kutoka Yerusalemu. Akanena kwa ujasiri kwa jina la Bwana Yesu,
Henceforth Saul was one of them, going in and out of the city, and speaking fearlessly in the Name of the Lord.
29 akihojiana na Wayahudi wa Kiyunani lakini wakijaribu mara kwa mara kumuua.
He also used to hold conversations and debates with the Grecian Jews, but they kept trying to kill him.
30 Wakati ndugu walipojua jambo hilo, wakamchukua mpaka Kaisaria, na wampeleke aende Tarso.
When they learned this the brothers took him down to Caesarea, and then sent him forth to Tarsus.
31 Basi kanisa lote katika Uyahudi, Galilaya na Samaria, lilikuwa na amani, na likajengwa, na kutembea katika hofu ya Bwana na faraja ya Roho Mtakatifu, kanisa likakua kwa kuongezeka idadi.
Now throughout the whole of Judea, Galilee, and Samaria the Church continued to enjoy peace and to be spiritually built up. It was increasing in members also, as it kept walking in the fear of the Lord, and in the comfort of the Holy Spirit.
32 Kisha ilitokea Petro alipokuwa akizungukazunguka pande zote za mkoa, akawateremkia waumini waishio katika mji wa Lida.
Now Peter, as he was going from town to town, came down also to the saints who lived in Lydda.
33 Akamuona huko mtu mmoja jina lake Ainea, mtu huyo amekuwa kitandani miaka minane; maana alikuwa amepooza.
Here he found a man named Aeneas, bedridden for eight years, a paralytic.
34 Petro akamwambia, “Ainea, Yesu Kristo akuponye; Amka na ujitandikia kitanda chako,” Mara akaamka.
Peter said to him. "Aeneas, Jesus Christ cures you! Rise and make your own bed!"
35 Na watu wote waliokaa Lida na Sharoni walipomuona mtu huyo, walimgeukia Bwana.
At once he rose to his feet. All the people of Lydda and Sharon saw him, and they turned to the Lord.
36 Palikuwa na mwanafunzi Yafa aitwaye Tabitha, ambalo lilitafsiriwa kama “Dorcas” Huyu mwanamke alijaa kazi njema na matendo ya rehema aliyoyafanya kwa maskini.
Among the disciples at Joppa was a woman named Tabitha - which may be translated Dorcas or "Gazelle" - a woman whose life was full of good works and almsgiving, which she was doing continually.
37 Ilitokea katika siku hizo aliugua na akafa; walipomsafisha, walimpandisha chumba cha juu na kumlaza.
She, as it happened, was taken ill just at that time, and died. After washing her body, they laid it in an upper room.
38 Kwa vile Lida ilikuwa karibu na Yafa, na wanafunzi walisikia kwamba Petro alikuwa huko, waliwatuma watu wawili kwake, wakimsihi, “Njoo kwetu bila kuchelewa”.
And as Lydda was near Joppa, the disciples, when they heard that Peter was there, sent two men to him with the entreaty, "Delay not to come to us."
39 Petro akaamka na akaondoka pamoja nao. Alipofika, walimleta katika chumba cha juu. Na wajane wote walisimama karibu naye wakilia, wakimwonyesha koti na nguo ambazo Dorcas aliwashonea wakati akiwa pamoja nao.
So Peter arose and went with them. On his arrival they took him up- stairs, and all the widows stood near him, weeping, and showing him the cloaks and garments which Dorcas used to make, while she was still with them.
40 Petro akawatoa wote nje ya chumba, akapiga magoti akaomba, kisha akaugekia mwili, akasema, “Tabitha, amka”. Akafungua macho yake na alipomwona Petro akakaa chini.
But Peter put them all out, and kneeled down, and prayed; and then turning to the body, he said, "Tabitha, rise!" She opened her eyes, and on seeing Peter she sat up.
41 Kisha Petro akampa mkono wake akamwinua, na alipowaita waamini na wajane, akawakabidhi kwao akiwa hai
Then he gave her his hand and raised her up, and after calling the saints and the widows, he gave her back to them alive.
42 Jambo hili likajulikana Yafa yote, na watu wengi wakamwamini Bwana.
This incident became known throughout Joppa, and many believed in the Lord.
43 Ilitokea Petro akakaa siku nyingi Yafa pamoja na mtu aitwaye Simoni, mtengeneza ngozi.
Peter stayed for some time in Joppa, lodging in the house of Simon, the tanner.